Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Ninavyoamini mimi ni kuwa, vitu mfano wa silaha za moto zinapaswa zibebwe na watu wenye akili timamu. Jioni ya leo nikiwa katika mitaa ya uhindini mjini Dodoma nimeshuhudia tukio ambalo limenifedhehesha sana. Nimekutana na askari mwenye umri mdogo, naweza kusema ni mtoto kwani kwa jinsi alivyo sidhani kama umri wake unafikia japo miaka 18. Katinga sare za kifidifosi, na bunduki yake begani. Kibaya zaidi mikononi kashika pakiti ya pombe maarufu aina ya kiroba huku akiendelea kunyonya taratibu. Tangu wakati huo mpaka sasa nahisi moyo wangu ukiwa na hofu. Hakuna asiyejua madhara ya pombe, kwa mtoto kama yule kulewa huku akiwa na SMG Begani ni hatari sana kwa usalama wa raia. Wanaohusika walitizame hili mapema kabla madhara hayajatokea siku moja..