The Palm Tree
JF-Expert Member
- Apr 13, 2013
- 7,951
- 12,535
Sielewi polisi wa mkoa wa Tabora na hususani Manispaa ya Tabora chini ya RPC wenu mnakwama wapi.
Tabora manispaa ya hatari ya miaka ya 1990s na kidogo 2000s iliyokuwa imejaa uhalifu na ujambazi ni kama inarudi taratibu.
Miaka hiyo majambazi hawakuwa na urafiki na taa za barabarani. Kila serikali ilipoweka taa za barabarani walikuwa wanazipiga kwa manati na kuzivunja vunja ili kuwe na giza kuwapa fursa ya kufanya uhalifu wao nyakati za usiku.
Hali ya usalama wetu raia na mali zetu uko mashakani sana ni kana kwamba hakuna jeshi la polisi hapa.
Kuna ongezeko la wimbi la vibaka na ujambazi wakifanya matukio ya uhalifu waziwazi kana kwamba mna ushirika nao.
Nitawapa mfano wa tukio moja.
Linawahusu walimu watatu wa kike na bodaboda wa pikipiki.
Hawa usiku wa kuamukia kuanza mitihani ya taifa drs la VII mwaka huu walioponea chupuchupu kutekwa na kunyang'anywa kila walichokuwa nacho usiku wa saa 8.
Tukio hili lilitokea barabara ya kutoka Uyui gerezani jirani na Shule ya Sekondari Isevya.
Ilikuwa ni wakati wa mitihani ya darasa la saba. Walimu hawa walitoka nyumbani kwao wakielekea ofisi za manispaa ili kupanda magari kusambazwa kwenye shule mbalimbali kwa zoezi la usimamizi mitihani hiyo ya drs la VII - 2020.
Kila mmoja alipanda bodaboda ya pikipiki kutoka eneo la Ipuli kwa Nyembo.
Walipofika eneo la Isevya Sekondari kwenye makutano ya barabara ya Uyui gerezani na Ipuli walikuta gari na pikipiki kama tatu na kundi la vijana kama 7 hivi wenye mapanga wamevaa black masks kufunika nyuso zao wakiwa wamezuia barabara kwa yeyote anayepita hapo.
Waliwapiga mkono. Bahati njema mita kama 150 hivi, bodaboda alitambua kuwa hao ni majambazi. Aligeuza pikipiki yake kwa kasi na kurudi alikotoka na kubadilisha njia.
Cha kushangaza majambazi haya yalianza kumfukuza mpaka karibu na ofisi za manispaa. Walipoona wameingia ndani getini yakaachana nao.
Sasa hii ni hatari sana. Ni kana kwamba polisi mko likizo na mmeshindwa kufanya kazi yenu.
Hili ni moja ya tukio la ujambazi lililofanyika kwa ujasiri sana kana kwamba hawa majambazi wana ushirika nanyi polisi.
Tunawaomba jeshi la polisi fanyeni kazi yenu.
Kuna wimbi kubwa sana la majambazi kuwatumia watoto wadogo wa miaka 10 hadi 15 kutenda ujambazi wao. Chunguzeni hili na mlifanyie kazi.
Sisi tunachotaka ni Tabora iliyo salama usiku na mchana.
Tabora manispaa ya hatari ya miaka ya 1990s na kidogo 2000s iliyokuwa imejaa uhalifu na ujambazi ni kama inarudi taratibu.
Miaka hiyo majambazi hawakuwa na urafiki na taa za barabarani. Kila serikali ilipoweka taa za barabarani walikuwa wanazipiga kwa manati na kuzivunja vunja ili kuwe na giza kuwapa fursa ya kufanya uhalifu wao nyakati za usiku.
Hali ya usalama wetu raia na mali zetu uko mashakani sana ni kana kwamba hakuna jeshi la polisi hapa.
Kuna ongezeko la wimbi la vibaka na ujambazi wakifanya matukio ya uhalifu waziwazi kana kwamba mna ushirika nao.
Nitawapa mfano wa tukio moja.
Linawahusu walimu watatu wa kike na bodaboda wa pikipiki.
Hawa usiku wa kuamukia kuanza mitihani ya taifa drs la VII mwaka huu walioponea chupuchupu kutekwa na kunyang'anywa kila walichokuwa nacho usiku wa saa 8.
Tukio hili lilitokea barabara ya kutoka Uyui gerezani jirani na Shule ya Sekondari Isevya.
Ilikuwa ni wakati wa mitihani ya darasa la saba. Walimu hawa walitoka nyumbani kwao wakielekea ofisi za manispaa ili kupanda magari kusambazwa kwenye shule mbalimbali kwa zoezi la usimamizi mitihani hiyo ya drs la VII - 2020.
Kila mmoja alipanda bodaboda ya pikipiki kutoka eneo la Ipuli kwa Nyembo.
Walipofika eneo la Isevya Sekondari kwenye makutano ya barabara ya Uyui gerezani na Ipuli walikuta gari na pikipiki kama tatu na kundi la vijana kama 7 hivi wenye mapanga wamevaa black masks kufunika nyuso zao wakiwa wamezuia barabara kwa yeyote anayepita hapo.
Waliwapiga mkono. Bahati njema mita kama 150 hivi, bodaboda alitambua kuwa hao ni majambazi. Aligeuza pikipiki yake kwa kasi na kurudi alikotoka na kubadilisha njia.
Cha kushangaza majambazi haya yalianza kumfukuza mpaka karibu na ofisi za manispaa. Walipoona wameingia ndani getini yakaachana nao.
Sasa hii ni hatari sana. Ni kana kwamba polisi mko likizo na mmeshindwa kufanya kazi yenu.
Hili ni moja ya tukio la ujambazi lililofanyika kwa ujasiri sana kana kwamba hawa majambazi wana ushirika nanyi polisi.
Tunawaomba jeshi la polisi fanyeni kazi yenu.
Kuna wimbi kubwa sana la majambazi kuwatumia watoto wadogo wa miaka 10 hadi 15 kutenda ujambazi wao. Chunguzeni hili na mlifanyie kazi.
Sisi tunachotaka ni Tabora iliyo salama usiku na mchana.