Polisi apigwa risasi na kufa

RIP. Ninalaani kwa nguvu zote mauji ya mtu asiye na hatia awe polisi, mtuhumiwa wa ujambazi, raia anayeandamana kwa amani. Kamwe watanzania tusianze kushabikia vifo vya raia wasio na hatia. Nina hakika kuwa polisi ni ndugu zetu, kama huna ndugu polisi basi utakuwa na jamaa au jirani mwenye ndugu polisi. Kamwe tuache mkondo wa sheria uchukue njia yake. Tusishabikie mauaji maana huwezi jua kuwa next target will be you, hizi chuki zinazoanza kujengeka miongoni hatuna budi kuziacha na kuwa wachamungu sana. Ila pia huu ni wakati wa vyombo vya usalama kuhakikisha tu haviwafurahishi watawala pekee bali pia wanajenga imani ya wananchi juu yao. Tumeona ya Egypt jinsi jeshi lilivyopata heshima kubwa toka kwa waandamani kisa tu hawakutumia vibaya nguvu za virafu vyao. KATIBA MPYA SULUHISHO LA KUJENGA AMANI YA KUDUMU TANZANIA.
 
samaki mmoja akioza wote wameoza,mbona huwa wanasomba watu hata kama huusiki

mzee unasema kweli ila mie naomba tusifikie huko yaani bado kuna mda wa kuweka sawa haya mambo!!!kwasababu huyu polisi hana kosa yawezekana ni wa cheo cha chini sana au hana kabisa cheo!!mara zote hawa jamaa huwa wanaamrishwa na wakubwa zao so bora angefariki mkubwa wao kuliko huyu jamaa!!!
 
Wana JF tukio hili bado limejaa utata, mbona polisi ni wengi tu tena wanarandaranda tu mitaani lakini hawajapigwa risasi? Anyway kwa jinsi ninavyofahamu JF karibu yote ni wanamapinduzi na wanachuki sana dhidi ya ukatili wa Jeshi la Polisi hususani kwa jinsi wanavyozikabili vurugu za kisiasa! Nawaomba wana JF tusimhukumu marehemu ila baada ya kutambua ukweli.
 
There is no justification of killing. I don't care who kills who, lakini tuache upuuzi wa kushabikia mambo. Hatuwezi kushangilia mauaji period.
subiri siku polisi watakapo mmiminia ndugu yako risasi,ndio utawajuwa polisi ni nani,ama subiri siku watakapo kubambikia kesi ndio utawaeleza wao ni kinanani,hayajakukuta wewe,tuulize tukueleze mkuuu,polisi waone tu mitaani usije ingia ktk anga zao pale kituoni ama mahali popote pale utaeleza kilichomnyoa kanga manyoya,
 
When a system in equilibrium is subjected to a change,the system will also try to change so as to halt the effect of that changes until stability is re-attained.Tazama Iraq,Afghanistan etc

Mkuu naona una apply Le Chatelier's principle duh! umenikumbusha Chemistry enzi zangu nipo form two.
 
mhh watanzania tumefikia huku,pole yetu halafu majambazi yakituvamia tunataka msaada wa polis

Mkuu aliyekudanganya kuwa polisi wa bongo wanapambana na majambazi ni nani au wewe uko nje ya nchi? Hapa bongo kazi ya polisi ni kupamabana na wapinzani wa chama cha majambazi, na kazi yao nyingine ni ujambazi na kubambikia raia wema kesi. Au hukuwahi kusikia kesi ya Zombe na majambazi wenzake katika uniform walivyodhulumu roho za vijana wafanya biashara wa madini, waliwaua na kupora mamilioni yao kisha wakawageuzia kibao kuwa ni majambazi?
 
vifo vingine vya kujitakia

Kuna mtu ameleta hija ya kuwa dawa ya polisi wakiwaua wenye kuandamana basi na watu wakawaue ndugu zao mitaani! Nadhani hii haijakaa sawa maana polisi anaweza akawa anashabikia chama tawala lakini ndugu zake ni cdm kindakindaki!

Na hivi wewe kama una jamaa yako polisi upotayari ufanyie kitu sawa kama huyo hayawani anaeleta hoja! Nadhani hatujafikia huko na Mungu aepushe tusijekufikia huko Amin.
 
RIP...
tupinge mauaji ya aina yoyote yale,yawe polisi au raia wa kawaida.....kwa sababu ni ishara ya kuvurugika kwa amani.
 
Haijalishi ana hatia au hana... haijalishi ana cheo kidogo au la, haijalishi chochote, as long as ni polisi, he derseve wt he gt.
 
Hivyo vitakuwa ni visasi (personal issues) tafadhali yasiiingizwe kisiasa, hamkawiii kusema CDM imeua!
ni kweli lakini furaha yangu iko pale pale, Awe amepaliwa na mfupa akafa awe amepigwa risasi kafa kwa uzinzi imradi polisi...kwangu mimi naona safi tu.
 
RIP. Ninalaani kwa nguvu zote mauji ya mtu asiye na hatia awe polisi, mtuhumiwa wa ujambazi, raia anayeandamana kwa amani. Kamwe watanzania tusianze kushabikia vifo vya raia wasio na hatia. Nina hakika kuwa polisi ni ndugu zetu, kama huna ndugu polisi basi utakuwa na jamaa au jirani mwenye ndugu polisi. Kamwe tuache mkondo wa sheria uchukue njia yake. Tusishabikie mauaji maana huwezi jua kuwa next target will be you, hizi chuki zinazoanza kujengeka miongoni hatuna budi kuziacha na kuwa wachamungu sana. Ila pia huu ni wakati wa vyombo vya usalama kuhakikisha tu haviwafurahishi watawala pekee bali pia wanajenga imani ya wananchi juu yao. Tumeona ya Egypt jinsi jeshi lilivyopata heshima kubwa toka kwa waandamani kisa tu hawakutumia vibaya nguvu za virafu vyao. KATIBA MPYA SULUHISHO LA KUJENGA AMANI YA KUDUMU TANZANIA.
Mkuu umeongea kweli mtupu, na si kuwa watu wanafurahia kuuwawa kwa polisi huyu but hasila za wananchi bado zipo juu ya ubabe wa watu hawa, wanatumia nguvu na mabavu mengi hata sehemu ambayo haistahili kufanyika hivyo.
RIP afande!
 
Back
Top Bottom