Polisi Anapozimeza Pesa za Hongo Alizopokea

Polisi Anapozimeza Pesa za Hongo Alizopokea

Herbalist Dr MziziMkavu

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
43,069
Reaction score
34,839
4203042.jpg

Wednesday, March 10, 2010 10:03 AM
Polisi mmoja wa nchini Urusi ametiwa mbaroni kwa kupokea rushwa na kisha kujaribu kuzimeza noti za pesa alizopokea ili kupoteza ushahidi. Polisi mmoja wa nchini Urusi ameingia matatani kwa kupokea rushwa ya pesa za Kirusi ruble 2000 sawa na Tsh. 95,000 na kisha kujaribu kuzimeza noti za hongo hiyo ili kupoteza ushahidi.

Afisa wa polisi, Alexei Nikolayev, alichukua rushwa toka kwa dereva aliyemkata kwa makosa ya barabani ili asimchukulie hatua dereva huyo.

Lakini dereva wa gari hilo aliwapa taarifa polisi ambao walimkamata afisa huyo wa polisi wakati akipokea rushwa.

Ili kupoteza ushahidi afisa huyo wa polisi alijifungia kwenye gari la polisi na kuanza kuzitafuna noti za pesa hizo.

Afisa huyo anaendelea kuchunguzwa na atafikishwa mahakamani uchunguzi utakapokamilika.
 
Back
Top Bottom