Ngaliba Dume
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,710
- 3,689
Hii ni twitter ya "propagandist" wa CCM,anasema huko Namibia kila akipita watu wanamuulizia JPM,JPM yaani kila kona ni Magufuli tu.
Polepole anasema Magufuli karudisha heshima ya Taifa letu,sasa sijui anataka kusema hii heshima inayorudishwa na JPM ilipotezwa na kina nani?
Kwa watu wa "logic" watakubaliana kuwa Polepole anamaanisha Ma-Rais wengine waliotangulia kuanzia Mwinyi mpaka Jakaya waliipoteza heshima ya nchi hii,sasa huyu aliyepo anajitahidi kurudisha pale tulipovuliwa nguo kimataifa kama Taifa.
Anasahau kuwa hao waliopoteza heshima ya Taifa ni wa chama hichohicho ambacho amekuwa anasema kimeliletea Taifa heshima kwa miaka 50 toka Uhuru.Hawa wanasiasa huwa wanajichanganya sana