jailos mrisho
JF-Expert Member
- Aug 22, 2012
- 644
- 1,360
Wewe nae ni muhuni muhuni tu wa mwanga huna unalojua. Kama unaona serikali ya awamu ya 5 na 6 zinatofauti ww ni muhuni pia. Mbowe anaozea ndani kesi ya kijinga mashahd wanajichanganya majaji ni wahuni wahuni alaf we mla makande unaongea pumba.Muogope sana mtu mkimya, muogope sana asiyeongea maneno mengi, ni ngumu kumjua hisia zake ni ngumu kumjua maumivu yake .. Ni ngumu zaidi kumjua anawaza nini
Mfurahie muongeaji sana, sometimes tunaita kubwabwaja,huyo katikati ya kujiachia kwake kuna mahali atajisahau na kuongea asivyotegemea au ambavyo hakupaswa kuvitamka hadharani! Ni katika kuongea kwake sana ataihabarisha hadhira bila kujua vitu na mambo mengi yaliyokuwa yamekosa majibu.. Muongeaji sana ni mropokaji na mropokaji ana faida nyingi nzuri na mbaya kutegemeana na upande
Vipindi vya Polepole kwenye vituo vya luninga bila kujali vinafadhiliwa na nani vinatupa somo muhimu sana ya kwamba binadamu ni nani katika uhalisia wake.. Hasa pale unapompoka hadhi na sahani yake!
Vipindi vyake vinamuumbua yeye mwenyewe na kumuacha uchi wa mbuzi kwa kiwango kikubwa cha unafiki anachoonesha kwakuwa anatambua wazi anachokifanya sasa, angetokea mwingine akakifanya wakati ule wa mwendazake pengine hata kaburi lake lisingeonekana, kama sio kupotezwa huko kwenye jela za mbali nknk
Maneno ya polepole yanafunua mengi mabovu na mabaya ya utawala uliopita na kwa sehemu yanaweza kutengeneza ushahidi siku itakapotokea huko mbeleni zikafunguliwa kesi za kikatiba na jinai..
Kwa kutokemewa wala kukaripiwa anapata mzuka na kufunguka zaidi na hapo ndio wengi wanapataka
Ameanza kuzungumzia kuhusu wahuni ambao walipaswa kumalizwa ndani ya chama lakini kwa bahati mbaya kudra za Mwenyezi Mungu zikapindua matokeo
Sasa Polepole atawajibika ikibidi awataje wahuni waliomalizwa na orodha ya wahuni ambao walikuwa 'hawajamalizwa'.. Na walitumia mbinu na njia gani 'kuwamaliza' wahuni ndani ya chama.. !
Anaupiga mwingi kwa raha zake, akimaliza mtori atazikuta nyama chini..Taharuki ni pale atakapokuta ni nyama ya fisi wakati keshakunywa mtori wote
Shame on you old man.



