Mimi namkubali. Alichofanya ni sahihiHili halitaishia kwa watumishi waliokuwa TMAA pekee, litaenda pakubwa sana. Taasisi zinazolipa CEO na DG zaidi ya 12M zipo za kutosha.
Ila mzee mkubwa anafanya kazi kwa mihemko sana, hii ni hatari sana!!!
Hahahaaa! Duuuu acha uongo bwasheeyan mim ningekua nasave 4.5m kila mwez.
Alioufyeka unakuja kwako?Kwa hili la kufyeka mishahara heko Jpm sisi walimu tunakupongeza
Rais yupo sahihi kabisa kwanini wengine wapate mamilioni na huku wengine wanapata vi laki tu!!!
Mzee tengeneza nchi ili watu tuheshimiane.
Zinakusanya zilizozalishwa na wazalishaji😆😆wajanja ni hao wanaolipwa milioni 15 na bodi moja hiyo hiyo inayolipa wengine 4mln.
wakati huo zote hazizalishi.
Sent from my ONEPLUS A3003 using JamiiForums mobile app
yaani maana yake kama tunaangalia kwa namna sawa,haitakiwi hawa walipwe mbuzi,wengine ng'ombe.Zinakusanya zilizozalishwa na wazalishaji
Na sisi wa Tsh.900,000/= tuelekee wapi?
...mkuu hii dhana sio sahihi..hakuna mtu asiye na umuhimu kwenye sekta ya kazi au Aliye muhimu kuliko wote..watumishi wote ni sawa uki-analyse critically...mfano mdogo huyo aliyeko kwenye mzunguko mkubwa wa pesa akiumwa anamhitaji daktari maana pesa anazosimamia haziwezi kumtibu..pia anahitaji ulinzi wa polisi na jeshi ili aishi kwa usalama&amani..kifupi tunategemeana kama viungo vya mwili hakuna anayemzidi wenzake kwa umuhimu
Naomba radhi mkuu, hahahaa!dah aisee expert tuombe radh watu wa tgsd.mbona tupo fresh tu na maisha yanaenda no posho no perdiem wala nin flengwa tu
Kuna sehemu kama taifa tuliyumba na kuachia watu mianya madhara ndio tunayaona sasa.Na huo ndio uzembe mwingine uliofanyika kwa nini taasisi za serikali zisiingizwe ktk scale za serikali(TGS) toka awali?
Hapana mkuu,NASA ni moja ya tasisi ambayo staff wake wanalipwa vizuri,wizara/taasisi zinazolipa vizuri USA zinafahamika wala sio kitu cha kuficha,hata katika jeshi,jeshi la anga la marekani wanafahamika kwa kuwa na malipo mazuri.hata training academy zao zipo classic sana tofauti na wengine,hiyo ipo wazi hata ukienda youtube utakuwa documentary kibao na videos zipo.Point yangu ni kwamba,tuangalie namna ya kulipa watu wetu mishahara kuendana na uhalisia wa maisha ili kusiwe na haya malalamiko,ila sio kupunguzia watu mishahara kwa nguvu..mkuu upo right kwenye baadhi ya maelezo but sio kweli kuwa usa watu wenye akili tu ndio wanaingia NASA...usa kuna best students wengi wanaenda kwenye fani ya upolisi, ufundi magari, usafi wa mazingira,etc na wanalipwa vizuri kuliko huko NASA..kule kazi ni passion kwanza kuliko salary.
Makusanyo yakiongezeka tena wajiongezee tena, yakiongezeka tena wajiongezee tena hawa wengine ambao sio wakusanyaji wabaki tu stagnant wakati wenzao wanapaa?Me naona ni wivu na umasikini tu kwa sababu sijaona mkiongelea kupunguza mishahara mikubwa na kuwaongezea wenye midogo
Lakini sijaelewa unavyosema mishahara iwe sawa unataka mkurugenzi wa TRA alipwe sawa na Askari wa level ya chini kabisa au mwalimu mweye certificate?
Ni kitu ambacho hakipo
Swala la kujiongezea mishahara ni kwamba kwa mfano mkurugenzi kapewa Taasisi ina wafanyakazi 1000 labda kawakuta na mishahara yao kama ilivyo lakini makusanyo ya Taasisi kwa mwezi labda ni bil10 na imekuwa hivyo kwa miaka mingi tu Sasa uongozi wa mkurugenzi huyu mpya ukawa wa tofauti kidogo
Makusanyo yakapanda mpaka kufikia bil20 kwa mwezi maana yake ufanyaji kazi lazima utakuwa umeongezeka kidogo miongoni mwa wafanyakazi
Wakaona tukiongeza watu 100 kwenye ajira majukumu yatakuwa sawa kwa sababu kazi zimekuwa nyingi kidogo
Sasa kwa sababu hiyo watu wakijiongeza mishahara kuna tatizo gani hapo?
Unabaki na sifuriKa.a ulikua na mkopo bank na wanakuachia ⅓ hapo itakua je