Kaka angalia huyu mwanamke anakutaka, kwa nini asizungumze na mwenzake anazungumza na wewe? Na wewe kwa nini usiende kuongea na wote wawili? mademu hata kama atakuwa anaishi kwake vizuri akikurtaka atazusha mambo mengi saaana ili kukupa wewe nafasi.
JF wengi hawaoneshi rangi zao za ukweli kuogopa kuwa judged.Wachache wetu tunatoa story zetu ili ziwe fundisho kwa wengine. Ushauri mwing humu huwa naona ni unafiki zaidi kuliko ukweli.Askudanganye mtu... wewe mwenyewe ndi muamuzi wa maisha yako unavyotaka yawe.Mengine ni ya kukuongezea tu.
Hahaaa jamani Maty thank you dear, si unajua inatubidi tutambue hayo kabla ya kuingia ndugu yangu.mamushka dia umemaliza kila kitu kaka DC mpelekee hii huyo dada na nakuambia ipo siku atakuja kutoa ushuhuda hapa yaani hata sina la kuongeza. MAMUSHKA WEWE NI NOMA
Tatizo ni watu kuvumilia vitu visivyovumilika. Yaani bora kuwa kwenye ndoa isiyo na raha wala amani kuliko kuwa mwenyewe?mbona hii ngumu sana..sasa kama hawawasiliani kabisa, watawezaje kutatua magumu kwenye ndoa zao?mwishowe inakuwa mazoea na kuwa kama maadui..
Mimi nampa tu pole na pia anaweza kuwa anampenda mumewe kumbe mumewe hana upendo nae. inauma sana hii!
Mimi napenda kusema neno juu ya mkasa huo...
Huyo dada anachotakiwa kufanya ni kuzungumza na mshenga wao ili aweze kupata msaada kwani mshenga ni mtu wa karibu sana na mumewe anaweza akamsikiliza na kujua kinachomsibu mumewe...
Endapo itashindikana anatakiwa awashirikishe watu wa dini ambao ndio waliowafungisha ndoa,kwa mfano sisi wakristo mtu kama atakuwa na tatizo kama hilo akienda kwa padre,mchungaji,muinjilisti au mzee wa kanisa huwa wana utaratibu wa kuwakutanisha na kuwapa mwelekeo mzuri ili kuweza kudumisha ndoa yao....
Nina Imani kama itashindikana basi ni vema kuwashirikisha wazazi pande wa kiume ili kuokoa jahazi...mimi nina imani kuwa mambo yatakuwa mazuri tu na utakuwa na furaha tena kwenye ndoa...
Hebu tupe ufafanuzi kidogo hapo..atachukuliaje kama hali ya kawaida wakati umri unaenda na yeye anatamani kupata raha, amani na furaha kama watu wengine?
Ndoa zinambo hizi wajameni. Eehhh atulie tu na aendelee kusali sana
Pole zake huyo Mama. Hivi ndoa ni ngumu kiasi hiki? Nitaogopa kuoa kwakweli
NiPM contacts zako kama uko serioustuoane tu. Sitokusumbua.
NiPM contacts zako kama uko serious
okey, i do understandha ha ha! Natania mwaya.
Mpaka pale mungu atakapojibu. Kumbuka mungu wetu ni mwaminifu hawahi wala hachelewi, ni kwa wakati wake ndipo atajibuMaty,
Huyu dada anasema ni muumini mzuri sana na amekuwa akiomba kipindi chote cha matatizo yake. Na bado anaendelea kuomba. Kwa sasa ameamua kutulia na kuendelea kusali kanisa lake la zamani..Katoliki.
Swali ambalo binafsi linanisumbua...aendelee kusali, kuomba na kufunga hadi lini?
Ni kweli ndugu yangu. Ila huyu mama nimekutana naye online kama wewe na mimi. Kwa hiyo hakuna jinsi ya kupata upande wa pili. Kama kina kitu tunaweza kumshauri basi tukitoe kutegemeana na hizi taarifa tulizonazo. Hata hivyo angalizo unalolitoa ni muhimu sana.
kulingana na hii habari...mama ndo ana matatizo japo inaonekana kama mama anaonewa.......
wewe fikiria huyu jamaa hampigi....hamnyimi chakula.....mavazi nk.... kuna kitu huyo mama amemfanyia mumewe sasa mumewe akaweka level of access....yaani kama ni database mama anaruhusiwa kuona ile interphase tu.... na baba anabaki yuko kwenye schema......
sasa ili upate mwafaka wa jambo hili na wewe msuluhishi usuje onekana mbaya badae......natural justice inatakiwa....muulize mume wa huyu dada......
kuna kitu huyo dada kakuficha......yaani ni kama mwanamke anayefanya abortion halafu akienda kuungama anaungama dhambi zingine tuu... na ile moja kubwa kabisa anaiaccha......muulize vizuri nini amemfanyia mume wake
Hapa mwanamama hana ndoa......