Please...sema hata neno tu, waweza kumuokoa huyu mama!

Maty,

Huyu dada anasema ni muumini mzuri sana na amekuwa akiomba kipindi chote cha matatizo yake. Na bado anaendelea kuomba. Kwa sasa ameamua kutulia na kuendelea kusali kanisa lake la zamani..Katoliki.

Swali ambalo binafsi linanisumbua...aendelee kusali, kuomba na kufunga hadi lini?

anaomba sana lakini hana imani kaka DC mimi nishawahi kutokewa na matatizo yaliyonisumbua nikawa naomba kwa imani na kila ambacho nilimuomba mungu alifanya tena bila mimi kutarajia wakati mwingine mungu anapokaribia kufanya jambo unaona dunia yote ndio inaanguka kumbe ndio wakati ambao mungu anataka kufanya vitu vyake. Asikate tamaa najua ni ngumu sana ila ajitahidi
 
Kama ni hivyo aangalie tabia yake imebadilika kwa kiasi gani pengine hafanyii chochote mumewe kama zamani.

DA kwani ukibadilika ndiyo tiketi ya mume kuzira? Kinachoonekana kwa sasa ni kuwa mume amezira karibia kila kitu cha huyu dada. Halafu mazungumzo ndani ya hiyo nyumba kwa sasa yanaanzia kwa mama tu vinginevyo inakuwa kama shetani anapita wakati wote, ni zaidi ya library!!

Yaani mume akiingia ndani na mke akaamua kunyamaza ndo imetoka. Lazima mke amsalimie siku zote. Hii ni sawa jamani?

Halafu kinachonishangaza, kwa upande wangu mimi ndo huanzisha mazungumzo mara nyingi na hata nikiwa mbali na wife napiga simu nyingi na sms nyingi zaidi yake? Hii kitu imenitisha sana!
 
anaomba sana lakini hana imani kaka DC mimi nishawahi kutokewa na matatizo yaliyonisumbua nikawa naomba kwa imani na kila ambacho nilimuomba mungu alifanya tena bila mimi kutarajia wakati mwingine mungu anapokaribia kufanya jambo unaona dunia yote ndio inaanguka kumbe ndio wakati ambao mungu anataka kufanya vitu vyake. Asikate tamaa najua ni ngumu sana ila ajitahidi

Nitaku-PM kwa maelezo zaidi. Nahitaji sana msaada zaidi ili niweze ku-update package yangu ya counselling.
 
kulingana na hii habari...mama ndo ana matatizo japo inaonekana kama mama anaonewa.......

wewe fikiria huyu jamaa hampigi....hamnyimi chakula.....mavazi nk.... kuna kitu huyo mama amemfanyia mumewe sasa mumewe akaweka level of access....yaani kama ni database mama anaruhusiwa kuona ile interphase tu.... na baba anabaki yuko kwenye schema......

sasa ili upate mwafaka wa jambo hili na wewe msuluhishi usuje onekana mbaya badae......natural justice inatakiwa....muulize mume wa huyu dada......

kuna kitu huyo dada kakuficha......yaani ni kama mwanamke anayefanya abortion halafu akienda kuungama anaungama dhambi zingine tuu... na ile moja kubwa kabisa anaiaccha......muulize vizuri nini amemfanyia mume wake
 
Asante FL,

Nitamfikishia ujumbe wako. Ila kwa maelezo yake..yeye ndiye humsalimia na kumpokea mume akirudi home na nyumba waliyonayo ina maji ya kutosha ikiwa ni pamoja na heater. Ila mume ni mpenzi wa kuchat na simu na kuangalia movie peke yake. Hataki usumbu wa mke. Hapo ndio anapouliza, afanye nini?

hizi ndoa bwana, kichomi kitupu!...alishawahi kukaa nea na kuongea nae kirafiki zaidi? coz watakapotulia na kuongea pamoja kimapenzi huyu mama ndio atapata suluhu na kujua wapi amekosea wapi arekebishe!...amshirikishe wenie kwa hili.
 
Hii ni story ya mwanamke mmoja ambaye nimekutana naye katika harakati za kupeana ushauri wa kutatua matatizo yanayotusibu katika mahusiano. Amekubali niiweke hapa ili kupata maoni ya wadau. Matatizo yake ni mengi sana ila kwa ufupi ni kama ifuatavyo:

1. Suala na unyumba katika ndoa yao yenye umri wa karibia miaka 4 wakiwa na watoto 2, limekumbwa na ukame wa ajabu. Wanashiriki tendo la ndoa kama mara 2 tu kwa mwezi na ni lazima mume atake. Mwanamke akiomba anaambiwa kuwa mume hawezi kufanya tendo la ndoa mara kwa mara. Wakati wa uchumba wao na siku za awali za ndoa yao, walikuwa wakishiriki tendo la ndoa hata zaidi ya mara 2 kwa week na wote waliliridhika na kufurahia tendo hilo. Hali ilianza kubadilika baada ya kama miaka 2 hivi. Mbaya zaidi hata kama mmoja akirudi safari baada ya kukaa kwa muda mrefu kiasi cha week nzima au zaidi, bado hakuna uhakika wa tendo la ndoa!

2. Mawasiliano ndani ya nyumba hasa hasa yale ya kimahaba nalo limekuwa tatizo. Yaani ni kama vile wanaishi maktaba. Muda mwingi mume akiwa nyumbani anacheza na simu yake akituma na kupokea sms kutoka kwa watu tofauti. Pia mume akiwa nje na jamaa wengine anakuwa mchangamfu sana, akiongea na vicheko juu.
3. Vitu vingi vya mume vimefunigiwa katika mkoba (brief case) wenye password ambayo mke hajui. Pia mume anazo account za benki ambazo mke wake hazijui kabisa. Na simu za mume zimewekewa password ingawa vitu vyote vya mke ikiwemo simu, account za bank n.k viko wazi na mume anavivinjari wakati wowote anaopenda.

4. Ni nadra kwa mume kukubali na kusifia (to appreciate) kitu alichokifanya mke. Na mara nyingi anamkatisha tamaa katika mipango yake anayomshirikisha.

Kutokana na haya matatizo na mengine mengi, huyo mama amekosa raha muda mrefu na aliwahi kufikiria kujidhuru (got closer to attempt suicide) ila kwa sasa ameamua kutafuta ushauri ama wa kuokoa ndoa au maisha yake. Amesali sana, amfeunga sana na kubadili makanisa kama nguo za mashidano ya mavazi lakini bado nazunguka pale pale. Kwa hiyo wadau nawaomba ushauri wenu ili niongeze kwenye package ya counseling ninayoendelea nayo kwa sasa.

Wasalaam, ....Babu DC
dah! acha nifungue mafaili yangu, nitarejea.
 
DC hii quote hapo kwa signature yako inamfaa sana "WE ALWAYS DON'T CHANGE UNTIL THE COST OF STAYING THE SAME EXCEEDS THE COST OF CHANGE"

Mama anatakiwa kuvunja ukimya mara moja. Abadilike otherwise gharama za kutokubadilika zitazidi za kuwa alivyo.
 
Mawasiliano baina yao ni muhimu sana, mawasiliano katika ndoa ni kitu cha muhimu sana. Too bad huyo mume wake haonyeshi hata interest ya kutatua matatizo au mambo ambayo mke anafanya na hayampendezi. sasa mama wa watu maskini amebaki kuhangaika. Kama ni wakristu waende kanisani kwa mlezi wao mama aanzishe hiyo kama waislamu the same thing msikitini kwa sheikh aeleze matatizo hayo. na pia wawashirikishe wasimamizi wao wa ndoa katika hili.

Kama vipi, si lazima kukaa hapo bwana inaonekana mama anajiweza kimaisha ana kazi na anaweza kujitegemea bila huyo mume. aondoke zake tu taratibu bila kelele. abebe wanae akawalee. siku zote najisemeaga kuliko nikae kwenye ndoa isiyo na raha kila siku mtu upo kama haupo nobody gives a damn about what you doing, whatever you do to impress the other half hata hajali.....aaaaaaahhh wapi naondoka zangu sio lazima. si rahisi kukaa nyumba isiyo na mapenzi mnalala chumba kimoja lakini hamuongei whats the use....!!!uvumilivu nao una mwisho wake ati.

Asimsahau Mungu aendelee kumuomba na mpe pole sana mama yetu.

Nakubaliana na wewe JS ila suala la kuondoka mimi nalipinga kabisa asiondoke kama nyumba ni yao wote na watoto so akae alee wanae hapo hapo na inavyoonyesha huyo mwanaume familia anaitunza tatizo tu haelewani na mama, na kizuri huyo mama ana kazi nzuri mi naona kazi yake ni ndogo tu hapo uvumilivu na kumuomba mungu kwa imani na huko kuomba wala si lazima ulale kanisani kanisani unaenda tu kupata mwongozo halafu unaendelea mi namshauri asiondoke na wala asi giveup cha kufanya aanze kuchukulia hayo matatizo kama changamoto tu asiyaweke sana rohoni ingawa ni ngumu lakini ukiamua inawezekana
 
hizi ndoa bwana, kichomi kitupu!...alishawahi kukaa nea na kuongea nae kirafiki zaidi? coz watakapotulia na kuongea pamoja kimapenzi huyu mama ndio atapata suluhu na kujua wapi amekosea wapi arekebishe!...amshirikishe wenie kwa hili.

Dada Nyamayao, huyu mama anasema kila anapojaribu kuongea na mumewe anamuona kama nyau fulani tu anayemsumbua. Na mume anasisitaza kwamba yeye ndiye mume wake na kwa kuwa hajamnyima chakula au kumfukuza home atulie tu! Nadhani kuongea kimapenzi ni ngumu sana kwani mama anasema amejaribu kila njia ameshindwa.
 
DA kwani ukibadilika ndiyo tiketi ya mume kuzira? Kinachoonekana kwa sasa ni kuwa mume amezira karibia kila kitu cha huyu dada. Halafu mazungumzo ndani ya hiyo nyumba kwa sasa yanaanzia kwa mama tu vinginevyo inakuwa kama shetani anapita wakati wote, ni zaidi ya library!!

Yaani mume akiingia ndani na mke akaamua kunyamaza ndo imetoka. Lazima mke amsalimie siku zote. Hii ni sawa jamani?

Halafu kinachonishangaza, kwa upande wangu mimi ndo huanzisha mazungumzo mara nyingi na hata nikiwa mbali na wife napiga simu nyingi na sms nyingi zaidi yake? Hii kitu imenitisha sana!


Huyo mwanaume ana GUBU kisa cha kununa dume zima nini hapo bwana???
 
hizi ndoa bwana, kichomi kitupu!...alishawahi kukaa nea na kuongea nae kirafiki zaidi? coz watakapotulia na kuongea pamoja kimapenzi huyu mama ndio atapata suluhu na kujua wapi amekosea wapi arekebishe!...amshirikishe wenie kwa hili.

dearest upo umepotea mwe! karibu mwaya
 
hizi ndoa bwana, kichomi kitupu!...alishawahi kukaa nea na kuongea nae kirafiki zaidi? coz watakapotulia na kuongea pamoja kimapenzi huyu mama ndio atapata suluhu na kujua wapi amekosea wapi arekebishe!...amshirikishe wenie kwa hili.
nyamayao, kwanza hali yako sweety?
bek to yowa posti: mimi akili yangu inaniambia huyu jibaba kuna kitu anaficha na sio kwamba kuna kitu kakerwa na jimama, ningeshauri huyu mama awe spy kwa mume wake kwa muda ili aone nini kinaendelea, usishangae mume kaingia kwenye u bwabwa. kama ku spy itamuongezea presha acha akate one way tiket tu. hamna ndoa hapo. ndoa imekaa kama mchezo wa kihindi bana, mke anataka miguno mume anacheza na simu. gademu!
 
DA, mbona mama wa watu keshasali sana..aendelee hadi lini wakati mume ndo wala hana habari naye?

Asikate tamaa aendelee kusali huku akitafakari tatizo na namna ya kulitatua.
Kitu kingine hapa wadungu, akina dada wengi wa siku hizi hawajui maana halisi ya kuolewa, wanaona ukifikisha umri fulani tu lazima uolewe. Si ajabu kuona mchumba wako (wadada wa siku hizi) anadai kuolewa, unakuta anasema "Sasa dear utanioa lini maana rafiki zangu wote wameolewa halafu umri unakwenda...."

Mtu hakuoi kwa sababu ya rafiki zako wote kuolewa, wala wewe kuzeeka, ndoa ni sakrament. Dada zangu, kuolewa ni zaidi ya wewe kuhama kwenu kwenda kwa mchuchu wako, wala kulala kitanda kimoja na mme, timizeni matakwa ya ndoa, ndipo kesi nyingi zitapungua.

Mtaani kwetu kuna bint kaolewa mwezi wa sita mwaka huu (2010), Siku moja(last month) kashindwa kuelewana na bwana ake kachukua Canter kapakia vyombo vyote alivyopewa zawadi kwenye harusi karudisha nyumbani kwao. Hapa kuna mke kweli?. Na baada ya kushauriwa karudi kwa mme wake ila jamaa kampiga stop kurudisha tena vile vitu pale home, kweli ndoa itadumu hapa? (hii ni true story aminin usiamini)
 
kulingana na hii habari...mama ndo ana matatizo japo inaonekana kama mama anaonewa.......

wewe fikiria huyu jamaa hampigi....hamnyimi chakula.....mavazi nk.... kuna kitu huyo mama amemfanyia mumewe sasa mumewe akaweka level of access....yaani kama ni database mama anaruhusiwa kuona ile interphase tu.... na baba anabaki yuko kwenye schema......

sasa ili upate mwafaka wa jambo hili na wewe msuluhishi usuje onekana mbaya badae......natural justice inatakiwa....muulize mume wa huyu dada......

kuna kitu huyo dada kakuficha......yaani ni kama mwanamke anayefanya abortion halafu akienda kuungama anaungama dhambi zingine tuu... na ile moja kubwa kabisa anaiaccha......muulize vizuri nini amemfanyia mume wake

Edson, ni vigumu sana kumpata mume kwa kuwe huyu dada tumekutana online na sina hakika kama anaweza kuwa tayari kunikutanisha na mume wake. Hata hivyo upo uwezekano wa yeye kunificha baadhi ya vitu ambavyo labda anajua kuwa alifanya na vikamkatisha tamaa mume wake. Ila hata kafanya jambo lolote, anastahili adhabu harsh kiasi hicho? Kwa nini asimpe talaka akaanza maisha yake binafsi na mume akawa huru kuoa tena?
 
Dada Nyamayao, huyu mama anasema kila anapojaribu kuongea na mumewe anamuona kama nyau fulani tu anayemsumbua. Na mume anasisitaza kwamba yeye ndiye mume wake na kwa kuwa hajamnyima chakula au kumfukuza home atulie tu! Nadhani kuongea kimapenzi ni ngumu sana kwani mama anasema amejaribu kila njia ameshindwa.

hii ndoa imeingiwa na kidudu mtu kaka angu tena huyo dada ana afadhali mume anatoa matumizi wengine huwa wanakimbiwa kabisa hawapati matumizi wala watoto hawahudumiwi
 
Ni kweli ndugu yangu. Ila huyu mama nimekutana naye online kama wewe na mimi. Kwa hiyo hakuna jinsi ya kupata upande wa pili. Kama kina kitu tunaweza kumshauri basi tukitoe kutegemeana na hizi taarifa tulizonazo. Hata hivyo angalizo unalolitoa ni muhimu sana.

Sawa Dc, ningeweza kushauri hiki, ajiangalie ni wapi alipoanguka mpaka ikawa hivyo, maana yawezekana kuna mahali alifungua mlango yeye mwenyewe na kuruhusu hiyo hali, mwambie ajikague anaweza kugundua tatizo lilianzia wapi na ikiwa atagundua hilo ni vizuri akarekebisha.
 
Nakubaliana na wewe JS ila suala la kuondoka mimi nalipinga kabisa asiondoke kama nyumba ni yao wote na watoto so akae alee wanae hapo hapo na inavyoonyesha huyo mwanaume familia anaitunza tatizo tu haelewani na mama, na kizuri huyo mama ana kazi nzuri mi naona kazi yake ni ndogo tu hapo uvumilivu na kumuomba mungu kwa imani na huko kuomba wala si lazima ulale kanisani kanisani unaenda tu kupata mwongozo halafu unaendelea mi namshauri asiondoke na wala asi giveup cha kufanya aanze kuchukulia hayo matatizo kama changamoto tu asiyaweke sana rohoni ingawa ni ngumu lakini ukiamua inawezekana

Maty,

Una maana aendelee kukaa home na waendelee kuchangia kitanda kimoja kama maiti walioko kwenye friji ya mochuari?
 
Dada Nyamayao, huyu mama anasema kila anapojaribu kuongea na mumewe anamuona kama nyau fulani tu anayemsumbua. Na mume anasisitaza kwamba yeye ndiye mume wake na kwa kuwa hajamnyima chakula au kumfukuza home atulie tu! Nadhani kuongea kimapenzi ni ngumu sana kwani mama anasema amejaribu kila njia ameshindwa.

na chakula cha ucku anakipata?.....hizo ishu za kuondoka home ckubaliani nazo, y aondoke?
 
Maty,

Una maana aendelee kukaa home na waendelee kuchangia kitanda kimoja kama maiti walioko kwenye friji ya mochuari?

ishu za wamama cku hizi kukimbizana na watoto kuhama zimepitwa na wakakti, abanane hapo mpaka kieleweke...
 
Huyo mwanaume ana GUBU kisa cha kununa dume zima nini hapo bwana???

Dena Amsi, kuna wanaume wanajua kununa usiombe, kuna jamaa namfahamu kwa kununa ndo mwenyewe mpaka huwa najiuliza hivi huko nyumbani kwake inakuwaje kwa mke wake, kwa hiyo wala usimshangae huyo anaemnunia mkewe.
 
Back
Top Bottom