PLAZA ACCORD-Mkataba uliotumiwa na Marekani kuishusha Japan kiuchumi miaka ya 1980

Xi Jinping

JF-Expert Member
Jun 14, 2023
525
1,816
Jinsi tunavyoiona leo teknolojia na uchumi wa China ukipaa na kuitishia Marekani, ndivyo ambavyo Japan ilikuwa na uchumi unaokua kwa kasi na kiteknolojia karibu kuifikia Marekani miaka ya 1980.

Marekani akaja na mkataba ulioitwa PLAZA ACCORD. Mkataba huu Marekani alisaini na mataifa ya Japan, Uingereza, Ufaransa na West Germany. Wakati huo haya ndiyo yalikuwa mataifa yenye uchumi mkubwa duniani na kiviwanda.

Wakati huo dollar ya Marekani ilikuwa na thamani kubwa sana kiasi kwamba export (mauzo ya nje) ya bidhaa za Marekani ilipungua sana duniani, kwa sababu watu wengi duniani walishindwa kuhimili bei za bidhaa za Marekani.

Yen ya Japan ilikuwa na thamani ndogo ukilinganisha na dollar hivyo ilisaidia sana kwenye export ya bidhaa zake. Wakati huo makampuni ya Japan kama TOYOTA, TOSHIBA n.k yalitawala soko la dunia huku makampuni ya Marekani yakiwa na export ndogo, hii ilikuwa hatari kwa uchumi wa Marekani.

Kwa sababu ya kushuka sana kwa mauzo ya nje ilipelekea trade deficit kwa uchumi wa Marekani. (Trade deficit ni pale taifa linapotumia pesa nyingi kuagiza bidhaa kutoka nje kuliko mapato wanayopata kwa kuuza bidhaa nje. Sikuzote hii huwa ni sign mbaya kwa uchumi wa nchi)

Tarehe 22 September 1985 katika hoteli ya New York City's Plaza Hotel, nchini Marekani mawaziri wa fedha wa nchi za Japan, Ufaransa, Uingereza, West Germany na mwenyeji Marekani wakakutana.

Marekani aliyashinikiza mataifa hayo manne yapandishe thamani ya sarafu zao dhidi ya dollar ya Marekani.

Mataifa hayo yakakubaliana na Marekani matokeo ni kwamba kwenye soko la dunia Marekani akaanza kuuza zaidi bidhaa zake kuliko mataifa mengine ya kiviwanda

Nchi hizo ziliathirika sana kiuchumi lakini hasahasa Japan kwa sababu exportation ya bidhaa zao katika soko la duniani zilipungua sana.

Nafikiri katika vitu ambavyo Wajapani hawatakuja kusahau ni kuingia mkataba huu wa kimangungo na Marekani na kuwashusha.

China imekataa kuwa kama Japan imekataa kutikiswa na Marekani anapigwa vikwazo lakini anakuja na mbinu mbadala. Kuna la kujifunza kutoka China tofauti na Japan.

Marekani ni kutunishiana naye misuli tu kibabe kama Urusi na China wanavyofanya sio watu wazuri.

Japan na EU wametepeta wamechagua kuwa chawa wa Marekani.
 
Jinsi tunavyoiona leo teknolojia na uchumi wa China ukipaa na kuitishia Marekani, ndivyo ambavyo Japan ilikuwa na uchumi unaokua kwa kasi na kiteknolojia karibu kuifikia Marekani miaka ya 1980.

Marekani akaja na mkataba ulioitwa PLAZA ACCORD. Mkataba huu Marekani alisaini na mataifa ya Japan, Uingereza, Ufaransa na West Germany. Wakati huo haya ndiyo yalikuwa mataifa yenye uchumi mkubwa duniani na kiviwanda.

Wakati huo dollar ya Marekani ilikuwa na thamani kubwa sana kiasi kwamba export (mauzo ya nje) ya bidhaa za Marekani ilipungua sana duniani, kwa sababu watu wengi duniani walishindwa kuhimili bei za bidhaa za Marekani.

Yen ya Japan ilikuwa na thamani ndogo ukilinganisha na dollar hivyo ilisaidia sana kwenye export ya bidhaa zake. Wakati huo makampuni ya Japan kama TOYOTA, TOSHIBA n.k yalitawala soko la dunia huku makampuni ya Marekani yakiwa na export ndogo, hii ilikuwa hatari kwa uchumi wa Marekani.

Kwa sababu ya kushuka sana kwa mauzo ya nje ilipelekea trade deficit kwa uchumi wa Marekani. (Trade deficit ni pale taifa linapotumia pesa nyingi kuagiza bidhaa kutoka nje kuliko mapato wanayopata kwa kuuza bidhaa nje. Sikuzote hii huwa ni sign mbaya kwa uchumi wa nchi)

Tarehe 22 September 1985 katika hoteli ya New York City's Plaza Hotel, chini Marekani mawaziri wa fedha wa nchi za Japan, Ufaransa, Uingereza, West Germany na mwenyeji Marekani wakakutana.

Marekani aliyashinikiza mataifa hayo manne yapandishe thamani ya sarafu zao dhidi ya dollar ya Marekani.

Mataifa hayo yakakubaliana na Marekani matokeo ni kwamba kwenye soko la dunia Marekani akaanza kuuza zaidi bidhaa zake kuliko mataifa mengine ya kiviwanda

Nchi hizo ziliathirika sana kiuchumi lakini hasahasa Japan kwa sababu exportation ya bidhaa zao katika soko la duniani zilipungua sana.

Nafikiri katika vitu ambavyo Wajapani hawatakuja kusahau ni kuingia mkataba huu wa kimangungo na Marekani na kuwashusha.

China imekataa kuwa kama Japan imekataa kutikiswa na Marekani anapigwa vikwazo lakini anakuja na mbinu mbadala. Kuna la kujifunza kutoka China tofauti na Japan.

Marekani ni kutunishiana naye misuli tu kibabe kama Urusi na China wanavyofanya sio watu wazuri.

Japan na EU wametepeta wamechagua kuwa chawa wa Marekani
 
Mataifa ya Ulaya, Japan na South Korea inapoKuja suala la geopolitical na uchumi wanapenda sana kusimamia sera za Marekani, hawajiamini kabisa. Wataishia kuwa nyuma ya Marekani miaka yote
Kuna haya mataifa ya Far East Asia; China/Taiwan, Japan, South Korea na North Korea kama yangekuwa na ushirikiano wako mbali sana kiteknolojia na kiuchumi wangekuwa na ushawishi sana
 
USA ni wajanja....wanapiga hesabu za mbele

Lakini Kwa Dunia hii Kila nchi inaenda kimahesabu
Ujanja ambao mataifa mengine wameshasanuka. Ila sijajua hao mawaziri wa fedha wa hIzo nchi waliingia huo mkataba wakiwa na akili timamu au walihongwa na Marekani. Maana kwa kusaini mkataba huo walikuwa wanajua nini kitaikumbuka uchumi wa mataifa yao
 
Suala la Japan, SK, EU kuwa upande wa marekani katika mambo mengi inachangizwa na mambo kadhaa kama.

Usaidizi wa kiuchumi wa marekani kwa ulaya katika vita ya dunia.

Usaidizi wa marekani kiulinzi kwa SK katika vita vya Korea.

Athari ya vita vya pili kwa Japan dhidi ya marekani
 
Mkataba wa Saudia na USA wa kuuza mafuta kwa dollar(petrodollar) unazishua nchi za far east na kuinyanyua Marekani.

Siku wakishtuka Marekani atakuwa sawa na South Sudan
Miaka ya karibuni China na Saudi Arabia wamekuwa wakifanya biashara ya mafuta kwa kutumia Yuan. Wiki hii nimeona wamesaini mkataba mwingine wa currency swap
20231123_185541.jpg
 
Suala la Japan, SK, EU kuwa upande wa marekani katika mambo mengi inachangizwa na mambo kadhaa kama.

Usaidizi wa kiuchumi wa marekani kwa ulaya katika vita ya dunia.

Usaidizi wa marekani kiulinzi kwa SK katika vita vya Korea.

Athari ya vita vya pili kwa Japan dhidi ya marekani
Wanaishi kwa historia kitu ambacho China alishakataa, anyway ila potential wanazo wangetakiwa kukaza kama China in short wao wamekubali watabaki kuwa nyuma ya Marekani miaka yao yote

Leo hii Japan imepigwa gap la kwenda na China katika soko la dunia kila kona iwe ni electronics, automobile, shipping industry n.k kwa sababu ya kutekeleza sera za Marekani
 
Wanaishi kwa historia kitu ambacho China alishakataa, anyway ila potential wanazo wangetakiwa kukaza kama China in short wao wamekubali watabaki kuwa nyuma ya Marekani miaka yao yote

Leo hii Japan imepigwa gap la kwenda na China katika soko la dunia kila kona iwe ni electronics, automobile, shipping industry n.k kwa sababu ya kutekeleza sera za Marekani
Japan ana mikataba mingi inayo mfunga same kwa Germany hawa wanachangamoto kubwa.

Kuhusu SK changamoto yao kubwa fear of NK haaaaaah 😄marekani anatumia fursa ila SK ni yeye mwenyewe kushindwa kujiimarisha zaidi
 
Wanaishi kwa historia kitu ambacho China alishakataa, anyway ila potential wanazo wangetakiwa kukaza kama China in short wao wamekubali watabaki kuwa nyuma ya Marekani miaka yao yote

Leo hii Japan imepigwa gap la kwenda na China katika soko la dunia kila kona iwe ni electronics, automobile, shipping industry n.k kwa sababu ya kutekeleza sera za Marekani
Kihalisi position aliyopo leo China ilikuwa iwe ya Japan, ila kaamua kurusha kitaulo kwa sababu ya kutii sera za Marekani

Marekani ni taifa ambalo sikuzote linalinda sana position yake hataki atoe mguu uweke mguu
 
Kihalisi position aliyopo leo China ilikuwa iwe ya Japan, ila kaamua kurusha kitaulo kwa sababu ya kutii sera za Marekani

Marekani ni taifa ambalo sikuzote linalinda sana position yake hataki atoe mguu uweke mguu
China anapigana vita kubwa sana tena zaidi ya Japan fight against American na allies wake economically sio kitu kidogo.

Napenda sera yao ya sasa ya kujitegemea kwa kila kitu wanewahi mapema kabisa katika hili kila sekta wanajitahidi kuwa top bila kufanya hivyo vikwazo vingi vingewarudisha nyuma sehemu nyingi.

Ni kama marekani anaweka vikwazo sehemu ambayo China tayari ameweka mbadala toka muda.
 
Japan ana mikataba mingi inayo mfunga same kwa Germany hawa wanachangamoto kubwa.

Kuhusu SK changamoto yao kubwa fear of NK haaaaaah 😄marekani anatumia fursa ila SK ni yeye mwenyewe kushindwa kujiimarisha zaidi
Na Marekani anawajaza sana hao Japan na South Korea hasa kuhusu ulinzi.

Marekani anatumia sana propaganda kuwaaminisha kuwa China, North Korea na Russia ni mtaifa adui kwao

Mwisho wa siku ndo hivyo wanaingia mikataba inayowafunga, wanaishia kununua silaha za Mmarekani na kufuata sera za kiuchumi na kisiasa za Marekani

Wamechagua kuwa watumwa wa Marekani
 
Na Marekani anawajaza sana hao Japan na South Korea hasa kuhusu ulinzi.

Marekani anatumia sana propaganda kuwaaminisha kuwa China, North Korea na Russia ni mtaifa adui kwao

Mwisho wa siku ndo hivyo wanaingia mikataba inayowafunga, wanaishia kununua silaha za Mmarekani na kufuata sera za kiuchumi na kisiasa za Marekani

Wamechagua kuwa watumwa wa Marekani
SK anapaswa kujiimarisha kiulinzi yeye binafsi kwanza kwa asilimia kubwa mwenzake NK anajaribu kufanya hivyo pamoja ya kwamba ana backup ya China na Russia.

Kutegemea watu wa nje na silaha za nje kiulinzi kwa kiasi kikubwa binafsi mimi huona sio sawa sijui wao wanatazama vipi ? Now Japan anajaribu kujiimarisha yeye binafsi ila mikataba inambana
 
China anapigana vita kubwa sana tena zaidi ya Japan fight against American na allies wake economically sio kitu kidogo.

Napenda sera yao ya sasa ya kujitegemea kwa kila kitu wanewahi mapema kabisa katika hili kila sekta wanajitahidi kuwa top bila kufanya hivyo vikwazo vingi vingewarudisha nyuma sehemu nyingi.

Ni kama marekani anaweka vikwazo sehemu ambayo China tayari ameweka mbadala toka muda.
Uko sahihi

Hii vita ngumu sana ila China kamdindia Marekani

Hii vita viongozi waliopita wa China sijui kama wangeiweza kama Hu Jintao na Jiang Zemin

Xi Jinping ni mwamba sana aisee Trump na Biden naamini wanakiri China chini ya Xi imeimarika sana

Xi kaja wakati China inamhitaji kiongozi wa kaliba yake ndio maana CPC wamempa uraisi wa kudumu

Biden anaishia kumuita dictator halafu mwamba hata hamjibu
 
Back
Top Bottom