Pinda: Rais amenipa maagizo mapya

si ajabu rais anataka waanze kufanya uchunguzi kama kawaida watasema wanaunda kamati. kweli kuna haja ya mambo yote yaongozwe na katiba ya nchi si mtu moja.

Inakuwaje kiongozi wa serikali bungeni hana mamlaka ya kuwawajibisha anaowasimamia bungeni? nini maana ya kuwa kiongozi? And anyways tunajua Vasco alikua safarini, lakini si makamu wake yupo? Grrrrrr...... aah wacha niseme.wakati mwingine mimi naona bora Lowasa.

Atakuwa kaambiwa atulize mambo ikiwezekana ajaribu kuchakachua akili za wabunge bajeti ipite.

kwa vyovyote atakuwa amemwambia kuwa hata yeye anahusika.

nchi hii hatuna head of state....

Mimi sishangilii sana Jairo kutimuliwa kazi, hata kidogo.

Imani yangu na nitazidi kuamini hivyo mpaka siku ya Mwisho ni kwamba jairo hakuamka kitandani kwake na kuingia ofisini aandike ile barua.
Kama lilikua wazo lake Binafsi lazima walikaa vikao na kushauriana na waziri husika au mkubwa mwingine.

Kama sio wazo lake ni lazoma alipewa maelekezo na aliye juu yake.

Inaposemekana rais ametoa maagizo mapya nakubaliana mia kwa mia na na hilo kwasababu Ni issue kubwa ambayo hamhusu Jairo peke yake au haimhusu yeye kabisa.

Hivi katibu mkuu ndio anafanya maamuzi ya wizara?

Ubaya wa kurundika maamuzi kwa Rais ndio haya matokeo ya maneno ya Pinda, pamoja na kwamba rasimu ya katiba mpya inaandaliwa lakini kuna umuhimu wa kuujulisha uma kupitia scandali hii kwamba haki haitapatikana kwa mfumo huu tulionao hivi sasa na tegemeo letu ni vyama vya upinzani kutuunganisha kwa maandamano ili ujumbe ufike ndani na nje ya inchi

Anaposema mapya ni dhahiri sasa ni tofauti na lile lake la kumfukuza mara moja, na anaenda mbali zaidi kusema wanalifanyia kazi ina maana linahitaji muda si kam alivyosema kuwa kama ni yeye alikuwa ni kutamka tu! Mara moja. Swali linalobaki gizani ni mapya yapi hayo ambayo yanahitaji kufanyiwa kazi?

Kama ingelikuwa ni kumchunguza ni lazima wangemsimamisha kazi mara moja ili uchunguzi uanze, hivyo nachelea kusema kuwa wana mchunguza! Kama ni kujuwa wahusika wote hili wachukuliwe hatua kwa pamoja nadhani pia hisinge zuia yeye kusimamishwa kazi na kuchukuliwa maelezo na katika maelezo yake ndipo uchunguzi wa mwanzo unge baini njia ya kutambuwa walio nyuma yake.

Hivyo basi ni dhahiri wanatafuta jinsi ya kuchakachuwa hili jambo! au wanataka kummaliza aondoke na ushahidi wote? sidhani au wanataka kumuamisha haraka hili kumuepusha na janga ya kuzee kichaa, maana nimemuona kama mzee vile akifukuzwa leo Penshen ya Katibu Mkuu ambayo ndugu yake na Swahiba wake alikuwa anamtafutia hataipata! kwahiyo nadhani wanataka awe katibu Mkuu Mstafuu kama kawaida ya CCM badala ya Mtuhumiwa! This is fine watakuwa wamemsaidia sana, ila wajuwe kila upuuza watakaofanya katika hili jambo litakuwa Milestone ya kuikaanga CCM, waamue ama kuisaidia Chama au Mpuuzi mmoja!

Labda wanataka kubadili baraza la mawaziri kwahiyo kampa kazi ya kuunda jipya akija walifanyie kazi na kulitangaza? Hili litakuwa wazo zuri sana, lakini watapata wapi watu maana Wabunge wa CCM ni wale wale. Myt: wote hovyo wote Posho na Rushwa, wazo zuri lakini siyo feasible; Pole sana Kikwete, haya ni madhara ya kuchakachuwa wagombea ubunge majimboni, itabidi CCM kama si sikio la kufa ijifunze kuanzia hapa maana najuwa ni kazi ngumu sana kupata watu safi wenyewe uwezo wa kuongoza wizara zote zilizopo kutoka miongoni mwa wabunge wa CCM waliopo sasa, kazi ngumu sana labda waunganishe baadhi ya wizara.

Pinda tunasubiri, Muhimu waandishi wa habari warudi wamuulize tusubiri hadi lini?
 
najua jairo hawezi fukuzwa hivi hivi labda atafutiwe sehemu nyingine maana jairo na kiikwete ni watu waliokua pamoja wakati baba yake jairo akiwa katibu kule singida na jamaa ndo alikua anaingia pale sasa akawa anaishi kwao akina jairo hivyo kwa mahesabu ya kawaida ni kwamba walikua pamoja na nyumba moja sasa hapo unafikiri kuna kufuzana!!!! ha ha ha tumeliwa pia huo mchezo ni jambo la kawaida kwa serikali maana kuhonga ili bajeti ipite kwa jairo ni niksi tu aliamka vibaya
Watanzania tumeliwa kekundu!!!!! haha ha ha ha ha ha ha ha n.k......
 
Hata kama Ngeleja na Naibu wake walikuwa hawajui kilichotokea, wao watabidi kuwajibika kisiasa . Hatuwezi kukubali usemi kuwa alikuwa hawajui. Mwinyi na wenzake Kina Kisumo walijiuzulu kwa makosa ambayo wao (kiukweli) walikuwa hawajui.
Hivi itakuaje maelekezo yanatolewa kuwa ukisha deposit wa inform DAP. Inaonyesha kuwa admin ya wizara ilikuwa wanafahamu mpango huu.
21 CEO chini ya wizara yake , hata mmoja asimuulize??
 
yaani ni hivi kuna vitu ambavyo ni against sheria na kanuni na taratibu za kazzi lakini kwa sababu ya mazoea ndio inakuwa hivyo, yaani unaiba hadi unajikuta ule wizi unakuwa sehemu ya maisha ya kila siku sawa na ilivyokuwa kwa Takrima na upuuuzi mwingine, mimi naamini kuwa kilichotokea ni either Shelukindo alikosa mgawo au mtu wake wa karibu (pengine mmoja wa wana-kamati) alikosa mgawo au alipewa below mgao na akamtumia Shelukindo kuwalipua wenzie, hata hivyo hadi kuandikwa barua na Yoriyori sorry Jairo ina maana huu uchafu ulikuwa unatendeka siku nyingi na sehemu ya maisha ya kila siku ya bunge, wabunge, wizara na watendaji wake....anaebisha labda kakosa mgao.
Hayo mambo yanatendeka miaka yote, safari hii kuna watu wamekosa mgao. Mama Shelukindo analijua hilo sana kwa sababu mme wake alikuwa ni M/kiti wa kamati hiyo miaka 5 iliyopita; naye alikuwa anapata mgao kupitia mr. wake. Leo hii mr. wake hayupo mjengoni kwa hiyo mgao haumfikii ndo maana akalipuka!
 
UK Premier kakatiza ziara baada ya skandali ya News of the World,Huku kwetu mteule wa Rais katuhumiwa kuchanga fedha kwa matumizi yanayoelekea kuwa rushwa wakti huo huo nchi bado ingali katika giza totoro bila ya ufumbuzi wa kuaminika,Rais yuko SA anatembelea kisiwa cha Robben...napata taabu kujua vipaumbele vya Mkuu wetu...

Unaweza kufa kwa kihoro kama sio BP ukijua vipaumbele vyake!! nchi yetu inatia aibu ukianza na kiongozi wa Juu hadi wa mwisho wao kila jambo ni kanyaga twende hakuna jambo lenye umihimu kwao wala kipaumbele zaidi ya nafsi zao inakera sana but dawa yako iko jikoni inachemka ikiwiva tu watakiona cha moto!!
 
Hayo mambo yanatendeka miaka yote, safari hii kuna watu wamekosa mgao. Mama Shelukindo analijua hilo sana kwa sababu mme wake alikuwa ni M/kiti wa kamati hiyo miaka 5 iliyopita; naye alikuwa anapata mgao kupitia mr. wake. Leo hii mr. wake hayupo mjengoni kwa hiyo mgao haumfikii ndo maana akalipuka!


kwa kujua kwako kuwa huu upuuzi ulikuwa unatendeka miaka yote, ukaminya; utakuwa mmoja wao au uwajibike kwa kunyamazia uovu.

Amandla.
 
Mimi sishangilii sana Jairo kutimuliwa kazi, hata kidogo.

Imani yangu na nitazidi kuamini hivyo mpaka siku ya Mwisho ni kwamba jairo hakuamka kitandani kwake na kuingia ofisini aandike ile barua.
Kama lilikua wazo lake Binafsi lazima walikaa vikao na kushauriana na waziri husika au mkubwa mwingine.

Kama sio wazo lake ni lazoma alipewa maelekezo na aliye juu yake.

Inaposemekana rais ametoa maagizo mapya nakubaliana mia kwa mia na na hilo kwasababu Ni issue kubwa ambayo hamhusu Jairo peke yake au haimhusu yeye kabisa.

Hivi katibu mkuu ndio anafanya maamuzi ya wizara?
Swali zito hili. Kinahitajika chombo zaidi ya rais kuamua hili.
Katiba.
Pamoja na matobo yake.
Walau itumike basi.
 
wala sitashangaa, ukiona Jairo na Waziri wake wakaendelea tu kuifisadi nchi yetu, na wala hakuna la kufanyiwa! Hawako peke yao.............
 
maagizo mapya ina maana ni yale yanayoenda kinyume na mpango uliokuwepo wa kumfukuza kazi Jairo.
 
Kuomtoa kafara Jairo mwenyewe ni kosa maana kwa ufahamu wangu mdogo sana katibu mkuu hawezi chukua maamuzi mazito kama hayo bila ya mabosi zake kujua pamoja na hazina kwa maana hiyo basi Ngeleja,Malima na Mkulo wapo kwenye channel moja 50milioni kwa kila wizara 21 zilizo chini ya wizara ya nishati sio hela ndogo jamani!! hatakama wao wataona ni ndogo vipi wakaguzi wetu wanapopita kukakua watasema zimetumika kwa matumizi yapi Chai ama Soda za wageni???

Hii chaneli ni ndefu tusiiangalie kijuu juu tu tujaribu kuangalia kwa mapana zaidi tukiamua kuchunguza ndani zaidi waweza kuta hata CAG naye yumo kwenye mkumbo maana hii nchi imeoza, na pengine hata wizara nyingine wanatumia mkumbo huo huo wa kina Jairo kupitisha bajeti zao.

Sitoshangaa kumsikia JK akimkingia kifua Jairo mbali yakuwa ni maswaiba bali ni kuficha aibu ya kuumbua wengi kwa maana nyingine Jairo nikama kidagaa tu baharini kuna MIJISAMAKI mikubwa iko pembeni inasikilizia kinachoendelea.
 
Acheni kumsumbua JK wangu bado anakula bata kwa Madiba, Yaani akose utamu wa pilau la Sauz kisa wabongo?

Kwanza mimi ninavyomuelewa atasema angalieni msifanye uamuzi utakaowanufaisha wapinzani
 
HABARI ZA KUAMINIKA

JAIRO AMEJIUZURU WADHIFA WAKE .................

mchana huu.....
 
Mimi sishangilii sana Jairo kutimuliwa kazi, hata kidogo.Imani yangu na nitazidi kuamini hivyo mpaka siku ya Mwisho ni kwamba jairo hakuamka kitandani kwake na kuingia ofisini aandike ile barua.Kama lilikua wazo lake Binafsi lazima walikaa vikao na kushauriana na waziri husika au mkubwa mwingine.Kama sio wazo lake ni lazoma alipewa maelekezo na aliye juu yake. Inaposemekana rais ametoa maagizo mapya nakubaliana mia kwa mia na na hilo kwasababu Ni issue kubwa ambayo hamhusu Jairo peke yake au haimhusu yeye kabisa. Hivi katibu mkuu ndio anafanya maamuzi ya wizara?
Mi nilijua tu hapa tutapigiwa danadana alaf linapita, Jairo ataendelea kuwas katibu mkuu, si unajua tena mabo ya Magamba, kila kitu utasikia uchunguzi unafanywa, uchunguzi wa nn wakat jambo liko waz? mi nahis huu mchezo mtoto wa mkulima alikuwa haujui ndo maana akataka amfukuze yy lakin mkubwa wake inawezekana ndo alimwambia Jairo afanye mambo ndo maana akamwambia PM asimfukuze
 
Hivi Rais anaposafiri hakuna anayekaimu? Au hamuamini daktari mwenzie!??? Any way, inawezekana mtoto wa mkulima aliingia kichwa kichwa hakujua kwamba katika sakata hili na mzee mzima anahusika. Hapa ndipo tunapomkumbuka Lowassa.
 
attachment.php



na HABARI ZA UHAKIKA TAYARI AMEACHIA NGAZI MCHANA HUU
 
Back
Top Bottom