Pinda na Vita tata ya Mashangingi

Hiki kizee nacho kimezidi kukurupuka tu! Sasa kimesahau kuwa juzi chenyewe kimeletewa VX8 eti kikadhira! Nakusubiri Mh. na hayo maagizo yako yasiyokuwa na kichwa wala miguu mara nisione Afisa Kilimo na Mifugo amevaa vizuri/suti. UTANIKUTA UONE NITAKAVYOKUTOA MBIO! Kwani hao siyo maafisa? Huwezi kuwalazimisha wafanane na wakulima bwana!! Huo ni udharirishaji
 
Mimi nashauri sera ya ununuzi magari ya serikali iangaliwe upya. Napendekeza kusiwe na magari ya serikali. Kila kiongozi anunue gari lake kwa fedha zake mwenyewe. Pia anunue fuel - petrol/disel na amlipe dereva kwa gharama zake.
Hakuna maana kodi za wananchi zitumike kuwanunulia viongozi magari ya kifahali, kununua fuel, kuwalipa madereva mishahara.
Kama ambavyo sisi wananchi tunavyojigharimia usafiri wa kwenda kwenye shughuli za ujenzi wa taifa, vivyo hivyo na viongozi wajigharimie. Hiyo ni ajira yao na wanalipwa mishahara mikubwa kwa kazi zao. Fedha zitakazo okolewa ziboreshe huduma za kijamii kama elimu, matibatu, miundombinu etc

Hebu watanzania tufanye utafiti, katika nchi hii ni watu wangapi wanatumia magari ya serikali, wanalipiwa gharama za mafuta, kulipa dereva na matengenezo ya magari, kulipia wafanyakazi wao wa nyumbani, kulipia gharama za matibabu etc. Ni fedha kiasi gani zinapotea? Viongozi ni watanzania wenzetu. Wanafanya kazi serikalini na wanalipwa mishahara, hawajitolei. Hivyo wanapaswa kujigharimia wenyewe kama ambavyo watanzania wengine wanavyofanya.

Hayo ni mawazo yangu.

Mkuu, mawazo yako ni mazuri lakini ukumbuke kwamba wanaopitisha sera na sheria ndio hao hao wanaofanidi ujingwa wa watz, na ndio wanaofaidi hayo magari na maposho na masafari yasiyo na tija
 
usanii kwenye jumba la sanaa.kila siku biti za kutokununua ma-VX lakini utashangaa daily unakutana na VX jipya liko barabarani.Tz tulianza kuongelea kuachana na magari ya kifahari kabla hata ya Kenya lakini cha kushangaza Kenya wameshaimplement sisi waTz bado biti tu za mdomoni
 
Mimi nashauri sera ya ununuzi magari ya serikali iangaliwe upya. Napendekeza kusiwe na magari ya serikali. Kila kiongozi anunue gari lake kwa fedha zake mwenyewe. Pia anunue fuel - petrol/disel na amlipe dereva kwa gharama zake.
Hakuna maana kodi za wananchi zitumike kuwanunulia viongozi magari ya kifahali, kununua fuel, kuwalipa madereva mishahara.
Kama ambavyo sisi wananchi tunavyojigharimia usafiri wa kwenda kwenye shughuli za ujenzi wa taifa, vivyo hivyo na viongozi wajigharimie. Hiyo ni ajira yao na wanalipwa mishahara mikubwa kwa kazi zao. Fedha zitakazo okolewa ziboreshe huduma za kijamii kama elimu, matibatu, miundombinu etc
Hebu watanzania tufanye utafiti, katika nchi hii ni watu wangapi wanatumia magari ya serikali, wanalipiwa gharama za mafuta, kulipa dereva na matengenezo ya magari, kulipia wafanyakazi wao wa nyumbani, kulipia gharama za matibabu etc. Ni fedha kiasi gani zinapotea? Viongozi ni watanzania wenzetu. Wanafanya kazi serikalini na wanalipwa mishahara, hawajitolei. Hivyo wanapaswa kujigharimia wenyewe kama ambavyo watanzania wengine wanavyofanya.

Hayo ni mawazo yangu.
Mkuu umesema ukweli na tuko pamoja kwa hili 100%. hawa watu hata umeme hawalipi, maji, usafiri matibabu na mengineyo mengi hawalipii pia, zaidi wanatumia kodi zetu kutongozea dada zetu tu (inauma sana). wanamishahara mikubwa marupurupu mengi na posho kibao. huu ni ujinga kuwasaidia watu ambao tayari wanakula keki ya taifa.
 
Jamani mtoto wa mkulima hana lolote, utashi ni uleule mdogo... Heri hata EL wa Richmond, anaiba na anafanya kazi.. kulilo huyu haibi na hafanyi chochote zaidi ya kucha tuibiwe na Tunaibiwa sasa na watu wengi zaidi.

waziri mkuu hapaswi kusema tu mkuu wa mkoa, au mtu ambaye hana mamlaka --- mamlaka hayo yote wamepewa ya nini kama hawayatumiii.. mbona magufuli yeye anayatumia? tangu mwaka jana mtoto wa mkulima anasemakuhusu mashangingi na huku yananunuliwa... eti juzi alikataa shangingi... heri hataangelitumia maana lingeweza dumu, sasa linatumiwa na wezi wengine hapohapo wizarani kwa kwenda beach na kula bethidei.

yaani sitaki hata kuwasikia, juzi amesema eti atakwend akuongea na rais kuhusu katiba, sasa wameshaongea na wamefikai makuabliano, yeye anasema nitaongea na rais... yaani wametufanya sisi ni wananchi ni WANATANU kabisa..!

tuna viongozi wa kuchapa viboko eit, basi tu. wanataka uongozi lakini utashi wano ni mdogo kabisa katiak uongozi.

Basi, Mungu ibariki Tz na Afrika.
 
kwangu mimi naona ni kichekesho mtu anakuja na VX halafu anapiga marufuku kutumia VX

kwa upande wa central government ...wangeuziana yale magari na kuwapa watendaji fuel allowances uone kama hayo mashangingi yangekua yanatimua vumbi namna ile
 
Chanzo: Taarifa ya habari Star tv saa mbili usiku. Badala yake wanunue Hardtop. Hivi tofauti ya bei ya VX na Hardtop ni sh ngapi? Kama zoezi hili kweli likitekelezwa atakuwa ameokoa sh ngapi?
Alisema landcruiser na si hardtop. Au ndu gurudumu linazunguka? kuwa makini kuquote watu.
 
kwangu mimi naona ni kichekesho mtu anakuja na VX halafu anapiga marufuku kutumia VX

kwa upande wa central government ...wangeuziana yale magari na kuwapa watendaji fuel allowances uone kama hayo mashangingi yangekua yanatimua vumbi namna ile

mkuu wanauziana kwa bei za kutupwa. we acha tu. ungejua?
 
mkuu wanauziana kwa bei za kutupwa. we acha tu. ungejua?
at least its going to be a one time-loss maana kwa sasa hayo magari yanatumika kwa kila upupu... they are being abused and we pay the overheads plus all the abuse from those cars tukiwa kwenye corolla zetu

wacha tupate hasara mara moja kuliko daily
 
Cha kushangaza zaidi serikali hii itaenda kununua Land Cruseir Hard Top toleo la 2010 au 2011 ambapo utakuta bei zake pia ziko juu subiri muone
 
Faida kubwa itakayotokana na uamuzi huo ni katika upunguaji wa gharama za uendeshaji. Tatizo langu lipo katika kuchukua hatua nusu nusu; ningelitegemea uamuzi kama huo ungeliambana na mwongozo unao elekeza mashangingi yaliopo sasa yafanyiwe nini. Maana bila ya kusimamia jambo hilo wakubwa wataanza kuyakarabati kwa bei mbaya na baadaye kujiuzia kwa bei ya kutupwa.
 
Cha kushangaza zaidi serikali hii itaenda kununua Land Cruseir Hard Top toleo la 2010 au 2011 ambapo utakuta bei zake pia ziko juu subiri muone
well said cousin

labda nikwambie ukweli... mashirika yote yasiyo ya faida yananunua the same cars kwa $45,00 gilbratar lakini la serikali ni bei twice sababu kubwa ni kamishen na rushwa

we dont need those cars everywhere... we only need a few of them na hardpots plus other cheap cars

endapos erikali iko serious kwenye cost cutting basi wataangalia overheads nyingi sana including vikao, fuel, per diems and posho feki

kikubwa zaidi hapo nighost workers na fake supplies

Pinda sasa anasound kama frustrated dude
 
Serikali hii haina kiongozi mzalendo, mwenye uchungu na nchi yake...wote wako 'affected na sera mbovu za chama tawala'..huwezi ukawa mwanachama na bado ukabaki na akili timamu....ni mawazo yangu tu.
 
well said cousin

labda nikwambie ukweli... mashirika yote yasiyo ya faida yananunua the same cars kwa $45,00 gilbratar lakini la serikali ni bei twice sababu kubwa ni kamishen na rushwa

we dont need those cars everywhere... we only need a few of them na hardpots plus other cheap cars

endapos erikali iko serious kwenye cost cutting basi wataangalia overheads nyingi sana including vikao, fuel, per diems and posho feki

kikubwa zaidi hapo nighost workers na fake supplies

Pinda sasa anasound kama frustrated dude
Hilo la ghost workers na fake supplies inaonekana ni dili za watu tena hasa kwenye wizara ya elimu kila siku wanakwambia hasara waliyoingia kwa kuwalipa ghost workers lakini wanashindwa kuziba hiyo mianya
 
Back
Top Bottom