Babylon
JF-Expert Member
- Feb 5, 2009
- 1,332
- 82
Pinda kwa mara nyinge amejitokeza na kuwadhihirisha wazanzibari nini kina ajiria katika akili yake,kwani siku zote inapofika wazanzibar kupigania haki yao anakuwa hafurahi ni zahiri shahiri haya yote hutokea pale tu wazanzibari wanapodai haki zao kwa mfano mambo kujiunga na mashirika ya kisilamu ,michezo mengineno ,binafsi nakushukuru kwa kauli yako kwani ndizo zinazo waamsha waliolala, kwa mara nyinge tena nasema asanta mzee pinda (lakuvunda halina Ubani) endelea kuwafokea,na vitisho vya hapa napale.
Imeandikwa na Mgaya Kingoba;
Tarehe: 23rd July 2009
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewatolea uvivu Wazanzibari kwa kuwaeleza kuwa, wanaotaka kuvunja Muungano au kutaka kujiunga na jumuiya za kimataifa nje kama nchi wajaribu na wataona matokeo yake.
Pinda leo ametoa majibu yanayoashiria kuwa haridhishwi na namna baadhi ya watu wakiwamo wabunge na viongozi wa Zanzibar wanavyojaribu kutaka kupata uwakilishi wa kimataifa nje bila kuihusisha Tanzania.
Kwa namna alivyojibu bungeni,wanaochokonoa Muungano kwa visingizio mbalimbali vikiwamo vya mgawanyo wa rasilimali pia wanamuudhi.
Ametoa msimamo huo wakati anajibu swali la papo kwa hapo la Mbunge wa Chwaka, Yahya Kassim Issa ikiwa ni utaratibu wa Bunge kila Alhamisi kabla ya kipindi cha maswali na majibu.
"Si mjaribu basi huko mnakotaka kwenda, kisha tujajua kama mmepata au la amesema Waziri Mkuu.
Wakati anauliza swali hilo, Mbunge huyo alieleza kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazungumzia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kama mwakilishi wa masuala ya nje, lakini vipi Zanzibar isiwe na uwakilishi wake?
Waziri Mkuu amesema, sijui Mheshimiwa Yahya anataka nini kwa swali hili? Kama ni nje tunawakilishwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Wizara hii ni kiungo cha nchi yetu na mataifa mengine.
Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM), alisema kazi ya Mbunge ni kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na hivi karibuni kumekuwa na kauli zinazoashiria uchochezi wa kuvunja
Muungano kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar na hakuna kiongozi ye yote mwandamizi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Rais wala Waziri Kiongozi aliyetoa kauli, hivyo alitaka kupata kauli ya Waziri Mkuu, Pinda.
Pinda alisema, nilikuwa nikisubiri sana swali hili, nilijua litakuja kutoka kwa akina Mnyaa (Mohamed Habib, Mbunge Mkanyageni), lakini wamekaa kimya kama wameshabikia yale yaliyotokea.
Waziri Mkuu alisema msingi wote wa mjadala huo wa wabunge wa Baraza la Wawakilishi ni suala la mafuta na gesi, ambalo aliongeza kuwa Rais Jakaya Kikwete alishalitolea kauli katika hotuba yake ya miezi michache iliyopita kwa Taifa.
Waziri Mkuu alisema suala la mafuta na gesi limekuwapo katika mambo ya Muungano tangu mwaka 1968, lakini kutokana na kauli ya Rais, suala hilo halipaswi kuwagawa Watanzania kwa sababu mafuta yenyewe hayajagundulika; hivyo hakuna sababu ya kutupiana maneno makali.
Pia suala hili halina tatizo, ni moja ya mambo yaliyoonekana yazungumzwe kwenye Kamati ya Pamoja chini ya Makamu wa Rais. Tukateua Mshauri Mwelekezi ambaye Juni 27 mwaka huu, alikabidhi ripoti yake kwa pande mbili ingekuwa vyema kupitia hiyo taarifa na kuona jinsi ya kushughulikia suala hili katika Muungano, amesema Waziri Mkuu.
Alimshukuru kwa dhati Selelii kuuliza swali hilo, akisema ametiwa simanzi na kauli za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliotoa kauli kama Wakoloni na wezi wa mchana ambazo Waziri Mkuu alieleza kuwa zimemshangaza.
Ni mawazo yangu kuwa Muungano ni mzuri ipo siku tutafarakana otherwise(vinginevyo) muwe tayari kujua ni upande gani utaathirika zaidi, amesema Waziri Mkuu akihitimisha kujibu swali la Selelii.
Hivi karibuni, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walitangaza kuwa suala la mafuta na gesi linaondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano na Zanzibar itasimamia yenyewe masuala hayo
Pinda awapasha wazanzibari
Imeandikwa na Mgaya Kingoba;
Tarehe: 23rd July 2009
Waziri Mkuu Mizengo Pinda amewatolea uvivu Wazanzibari kwa kuwaeleza kuwa, wanaotaka kuvunja Muungano au kutaka kujiunga na jumuiya za kimataifa nje kama nchi wajaribu na wataona matokeo yake.
Pinda leo ametoa majibu yanayoashiria kuwa haridhishwi na namna baadhi ya watu wakiwamo wabunge na viongozi wa Zanzibar wanavyojaribu kutaka kupata uwakilishi wa kimataifa nje bila kuihusisha Tanzania.
Kwa namna alivyojibu bungeni,wanaochokonoa Muungano kwa visingizio mbalimbali vikiwamo vya mgawanyo wa rasilimali pia wanamuudhi.
Ametoa msimamo huo wakati anajibu swali la papo kwa hapo la Mbunge wa Chwaka, Yahya Kassim Issa ikiwa ni utaratibu wa Bunge kila Alhamisi kabla ya kipindi cha maswali na majibu.
"Si mjaribu basi huko mnakotaka kwenda, kisha tujajua kama mmepata au la amesema Waziri Mkuu.
Wakati anauliza swali hilo, Mbunge huyo alieleza kuwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazungumzia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kama mwakilishi wa masuala ya nje, lakini vipi Zanzibar isiwe na uwakilishi wake?
Waziri Mkuu amesema, sijui Mheshimiwa Yahya anataka nini kwa swali hili? Kama ni nje tunawakilishwa na Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa. Wizara hii ni kiungo cha nchi yetu na mataifa mengine.
Mbunge wa Nzega, Lucas Selelii (CCM), alisema kazi ya Mbunge ni kuilinda na kuitetea Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, na hivi karibuni kumekuwa na kauli zinazoashiria uchochezi wa kuvunja
Muungano kutoka Baraza la Wawakilishi Zanzibar na hakuna kiongozi ye yote mwandamizi wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Rais wala Waziri Kiongozi aliyetoa kauli, hivyo alitaka kupata kauli ya Waziri Mkuu, Pinda.
Pinda alisema, nilikuwa nikisubiri sana swali hili, nilijua litakuja kutoka kwa akina Mnyaa (Mohamed Habib, Mbunge Mkanyageni), lakini wamekaa kimya kama wameshabikia yale yaliyotokea.
Waziri Mkuu alisema msingi wote wa mjadala huo wa wabunge wa Baraza la Wawakilishi ni suala la mafuta na gesi, ambalo aliongeza kuwa Rais Jakaya Kikwete alishalitolea kauli katika hotuba yake ya miezi michache iliyopita kwa Taifa.
Waziri Mkuu alisema suala la mafuta na gesi limekuwapo katika mambo ya Muungano tangu mwaka 1968, lakini kutokana na kauli ya Rais, suala hilo halipaswi kuwagawa Watanzania kwa sababu mafuta yenyewe hayajagundulika; hivyo hakuna sababu ya kutupiana maneno makali.
Pia suala hili halina tatizo, ni moja ya mambo yaliyoonekana yazungumzwe kwenye Kamati ya Pamoja chini ya Makamu wa Rais. Tukateua Mshauri Mwelekezi ambaye Juni 27 mwaka huu, alikabidhi ripoti yake kwa pande mbili ingekuwa vyema kupitia hiyo taarifa na kuona jinsi ya kushughulikia suala hili katika Muungano, amesema Waziri Mkuu.
Alimshukuru kwa dhati Selelii kuuliza swali hilo, akisema ametiwa simanzi na kauli za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waliotoa kauli kama Wakoloni na wezi wa mchana ambazo Waziri Mkuu alieleza kuwa zimemshangaza.
Ni mawazo yangu kuwa Muungano ni mzuri ipo siku tutafarakana otherwise(vinginevyo) muwe tayari kujua ni upande gani utaathirika zaidi, amesema Waziri Mkuu akihitimisha kujibu swali la Selelii.
Hivi karibuni, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi walitangaza kuwa suala la mafuta na gesi linaondolewa katika orodha ya mambo ya Muungano na Zanzibar itasimamia yenyewe masuala hayo
Last edited by a moderator: