PILAU HUONGEZA NGUVU ZA KIUME

PILAU HUONGEZA NGUVU ZA KIUME

The only

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2011
Posts
11,132
Reaction score
14,637
Habarini wakuu !
Hivi karibuni kidume katika kutafuta pesa nilikutana na mganga mmoja wa tiba za asilia kwa majanga yangu ya kimaisha ya kuzindika mashamba ya kilimo (Wakulima mnanielewa) sasa kila nikienda kwake nakuta anakula pilau ,nikatanabahi ikabidi nimuulize ,akaniambia pilau inasidia kulinda heshima kwa mama yoyo nkamuuliza kivipi? mi mbona huwa naambiwa ni vyakula vya wanaume wa dar .

Akaniambia pilau halisi sio lile la kununua vikopo vya masala hutumia viungo ambavyo vina tibu kabisa nguvu za kiume akaniambia ndio maana wazanzibari hawana mazoezi ila kwenye kwachu kwachu huwa wanyama wabaya ulizia warembo juu ya wapemba wanoongoza kwa kujichana mapilau.

Basi nami bila ajizi nikaamua nije na sababu kisayansi ila za kugoogle (mi ni kilaza) twendage :

Irikii- ndani yake ina kikemikali kinaitwa cineole hiki huongeza kasi ya mzunguko wa damu hivyo kuongeza tamaa ya ngono na mtaimbo kusimama imara na kuwa mgumu kama nyundo ya muhunzi.

Kitunguu swaumu : Hii huwa na kemikali ambayo huitwa allicine hii huyeyusha mafuta mabaya kwenye damu na kufanya damu kutembea kwa spidi ,tofauti na iriki hii ikitumika kwa muda hutatua tatizo mazima.

mdalasini : hii huondoa uchovu wa mwili hasa misuri na kukupa hali ya kujiskia mpya kama umetoka kuamka ambayo ni nzuri kwa show kama zile za GuDume shem wa wazenji.

Karafuu-Hii ni kama tangawizi kwa wanaume huongeza homoni za udume testrone na kukomesha tatizo la kukojoa mapema kwani inapunguza uwezo wako wa kusikia utamu.

Tangawizi : Hii nzuri sana kwa kuzuia kuwahi kukojoa kwani yenyewe husafisha mitaro ya damu na kufanya ikimbie zaidi na inafahamika dushelele ili isimame macho yanapeleka tafsiri ya kingono kwa ubongo ubongo unatuma ujumbe kwa moyo kukimbiza damu sasa unakuta mishipa inamimafuta (lehamu mbaya ) mto usipoenda spidi kutokana na mvua basi umeme utazarishwa kidogo sawa

RAI : Wanaume wa Dar hebu kuleni pilau msisahau na makachumbali ila isiwe ile ya maunga ya masala iwe kitu halisi inapatikana sana pale magomeni mapipa kuna migahawa kama mitatu hivi wana pilau all the time natural.

NB: Sijihusishi na biashara ya viungo,sijui kupika pilau hilo,sitaki mtu inbox ,na sitangazi mgahawa wowote asnteni.

Kwa jinsi ya kupika pilau lenye tija hii soma comment namba 10 iliyokuwa copied toka kwa Rubi
 
Lipia tangazo tafadhali
Ningesema pilau hilo linapatikana mgahawa fulani hapo ningekuwa na yangu,au ningetoa namba ya simu ,nilichokisema hata mkeo mwambie akupikie natural basi ujumbe wangu kwako umetimia ,na pilau inapatikana mahali kwingi hata magomeni sjaspecify ni mahali kwingi ila unatakiwa uulize ni la viungo au vya masala
 
Utasababisha wanaume wagome kula ugali kabisa.
Ugali labda wa dona ,huo hupunguza IQ na kuleta woga,ona waarabu wala wali wanavyokimbiza wazungu utawafananisha na wasukuma
 
Awamu hii ya tano tutaona mengi kujusu nguvu za kiume na tiba zake.
 
Awamu hii ya tano tutaona mengi kujusu nguvu za kiume na tiba zake.
Ni geni huku kwetu ila nchi zilizoendelea biashara ya nguvu za kiume , kisukali na uzito zinawapa watu utajiri mkubwa ,lakini ukweli masuluhisho yapo ndani ya maisha yetu hayahitaji kitu zaidi ya kujitambua
 
PILAU NAYOZUNGUMZIA NI ILIYOPIKWA HIVI

Nijuavyo Mimi pilau ina dizain nyingi za kupika hii ni kadri mtu apendavyo leo anataka pilau hii, au ile. tehetehe.

Sasa pilau yangu mimi kwa leo ni hii.

MAHITAJI:
- Mchele kg 1
- Nyama ya ngombe/Kuku 3/4 kg.
- vitunguu maji vikubwa 2.
- nyanya moja au mbili za wastani.
- ndimu/limao 1
- Unga wa pilau uliochanganywa vijiko vya chakula 2
- Jiira (binzari nyembamba) iliyosagwa vijiko vya chai 2
- Jiira nzima ambayo haijasagwa vijiko vya chai 2
- Pilipili manga nzima kijiko cha chakula 1 (au punje 15)
- Tangawizi iliyotwangwa kijiko cha chai 1/2 (ukipenda)
- vitunguu thomu (swaum)vilivyosagwa vijiko vya chakula ujazo wa wastani 3.
- chumvi (utaonja inayotosha)
- mafuta ya kupikia

JINSI YA KUANDAA.
- safisha nyama, kisha katakata vipande vya wastani, changanya na vitunguu swaumu kijiko kimoja, ndimu kipande, chunvi ya kutosha, tangawizi 1/2 kijiko cha chai na kisha weka jikoni. ikianza kushemka igeuzegeuze ili viungo vichanganyane vizuri (kama dk 5-7) kisha weka maji yafunike hiyo nyama acha ichemke kwa dk kama 10 - 15 (itategemea ni nyama ya aina gani na laini kiasi gani) mie napendelea ya ngombe au kuku wa kienyeji. hakikisha unapika kwa moto usio mkali sana na supu isikauke maana ndio utakayotumia pia kupikia pilau yako.

- Baada ya nyama kuwa tayari weka pembeni, injika sufuria ya kupikia pilau yako.
- weka mafuta ya kupikia 1/2 glass (au waweza kadria yanayotosha)
- menya, kata, na weka vitunguu maji kwenye mafuta yaliyopata moto kaanga kwa muda kidogo mpaka vilegee
- weka nyama (bila) supu kaanga mpaka nyama ianze kubadilika rangi kuwa ya brown kwa mbali,
- weka vitunguu thomu kaanga (mchanganyiko wako utaanza kuwa wa brown) hakikisha usiunguze
- weka jiira iliyonzima pamoja na iliyosagwa, pamoja na pilipili manga. kaanga kidogo vichanganyike vizuri
- weka unga wa pilau na kaanga ilivitu vyote vichanganyike vizuri na usiunguze (kama vyang'angania kwenye sufuria oneza supu ya nyama kidogo) kisha kamua ndimu kipande kiasi cha kupata kijiko kimoja cha chakula weka pamoja na nyanya endelea kukaanga vichanganyike vizuri.
- weka chunvi kiasi koroga vichanganyike vizuri
- weka mchele uliousafisha na kuuosha (angalizo mchele usiuoshe mapema sana maana utalainika - osha wakati unaanza kukaanga michanganyiko yako ya pilau.
- changanya vizuri mchele wako na viungo ulivyokaanga kisha weka supu uliyopikia nyama (badala ya maji) angalia usawa wa mchele na supu isiwe nyingi sana kiasi cha kufanya mchele uwe boko au ndogo kiasi cha kufanya uwe mbichi tegemea na aina ya mchele.

- ikianza kuchemka, punguza moto iive katika moto mdogo
- ikianza kukauka geuza funika kama dk 7 kisha geuza tena acha iive taratibu baada kama dk 20 iiangalie kama tayari ipua tayari kwa kuliwa na sosi, saladi uliyoiandaa.

Andiko hili ni kwa hisani ya Rubi
 
Kwa hiyo tunaohitaji nguvu za kutafuta ufalme wa Mbinguni tule nini ?
 
Huku tunakoelekea hata mavi ya kuku tutaambiwa yanaongeza nguvu za kiume. Hizi nguvu kwa kweli imekuwa janga la taifa. Hata madumu pia nasikia yanaongeza nguvu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom