Picha: Mnara wa Babel, fumbo linaloishi

Picha: Mnara wa Babel, fumbo linaloishi

Bwana akashuka ili auone mji na mnara waliokua wakiujenga wanadamu; Bwana akasema, tazama watu hawa ni taifa moja,na lugha yao ni moja na haya ndio wanayotaka kuyafanya,wala sasa hawatazuiliwa neno wanalo kusudia kulifanya. Haya na tushuke huko tuwachafulie usemi wao ili wasisikilizane maneno wao kwa wao! Mungu tuna omba utusikie na hata adui zetu Ccm ukawa chafulie lugha ili wasielewane lugha wao kwa wao!

.....CCM sasa kila mtu anaongea lugha yake ....imetimia !!!
 
Hakika mnara wa Babeli unaporomoka kwa kasi ya kutisha.

Nitoe mfano mmoja tu kulithibitisha hilo, wakati wabunge wa Sisiem watupu kwenye BMK walipokuwa 'wakinyofoa' kila ibara iliyokuwemo kwenye Rasimu ya Tume ya Warioba, ambayo walikuwa wakiiona tishio kwa azma yao ya kuitawala nchi hii milele, vyama vya upinzani, wanaharakati na umma wa watanzania ulipaza sauti kwa nguvu sana kukemea 'mchezo' wao huo wa hatari wanaoucheza, lakini watawala wetu wakaamua kuziba masikio yao kwa pamba, wakijifanya kelele hizo hawazisikii.

Ilipotangazwa tarehe ya kura ya maoni kuwa tarehe 30 mwezi huu, umma wa watanzania napo ulipaza sana sauti zao kuwa hakuna uwezekano kwa tarehe hiyo iliyotangazwa, kuwezesha kura hiyo ya maoni kupigwa, napo watawala wetu wakajivika upofu, kujifanya hawaoni kelele hizo zinazopazwa.

Hatimaye Mungu wetu mkuu akaamua kuingilia kati kwa kumpa ujasiri mkubwa Jaji Lubuva wa Tume ya uchaguzi na akatangaza hadharani kuwa kura hiyo ya maoni haitapigwa katika tarehe hiyo 30 aliyoitangaza 'mfalme'

Hakika kabisa kwa mfano huo mmoja tu, ni dhahiri kwa sasa kuwa mnara wa Babeli unaporomoka kwa kasi ya kutisha na hitimisho lake litakuwa mwezi Oktoba ya mwaka huu!

....Hakika mkuu Babel ya Tanzania kuporomoka !!!
 
....nawahurumia walioko huko juu maana utakapo poromoka hakuna atakaye baki !!!

Maana sasa hivi naona na lugha yao ilishakorogana! lete BVR, BRN,EScrow, meremeta, Vitambulisho vya taifa, Mahela Uswisi, Trillion3, kura za katiba 30Apr oooh mara haijulikani tena, na mengine kama hayo!! Mnara wa Babeli ni LiCCM na litaanguka kishindo kikuu!!
 
Maana sasa hivi naona na lugha yao ilishakorogana! lete BVR, BRN,EScrow, meremeta, Vitambulisho vya taifa, Mahela Uswisi, Trillion3, kura za katiba 30Apr oooh mara haijulikani tena, na mengine kama hayo!! Mnara wa Babeli ni LiCCM na litaanguka kishindo kikuu!!

.....Kuangamia lazima waangamie Kiburi na dhambi vimewatawala !!!
 
....

...Kuanguka kwa Mnara wa Babel kutaambatana na matukio ya kisiasa yasiyo tarajiwa !!!
 
Na wengine wamejipachika majina ya Nyoka wa Makengeza! sijawahi muona nyoka wa namna hiyo labda kama anafugwa Gamboshi!??

.....wamejidhihirisha kwa matendo yao lakini tetemeko linakuja na watakuwa Historia
 
....na wote siku hiyo tutausukuma Mnara kwa sekunde moja

Yaani tena tuwape onyo kabisa wale wanojiandikisha halafu hawaendi kupiga KURA,maana hawa ndiyo wanaotoa mwanya wa kuchakachua KURA.........
 
Yaani tena tuwape onyo kabisa wale wanojiandikisha halafu hawaendi kupiga KURA,maana hawa ndiyo wanaotoa mwanya wa kuchakachua KURA.........

.....mpaka Oktoba kila mtu atakuwa ameshika position ya kusukuma Mnara
 
Back
Top Bottom