Picha: Madenge, Pimbi, Komredi Kipepe

Picha: Madenge, Pimbi, Komredi Kipepe

dah ukipata gundu la pimbi unaweza kujiua aisee.

Nimeona wiki iliyopita tu kwenye gazeti la Sani Pimbi kamtembelea mshikaji wake ulipofika mda wa kuoga Pimbi akapelekewa maji na shemeji yake alipofika bafuni wacha amvutie bafuni Shemeji baada ya mda mshikaji wake akashituka mbona wife harudi? ikabidi avizie kule bafuni kilichotokea hukoo!!! Labda tusubirie Part II
 
kipepe2.jpg


madenge.gif


kipepe.gif


pimbi.gif


sani.gif


kipepe1.jpg
kumbusha mimi long time kitambo
 
Ehe Bwana nilikuwepo enzi hizo. Yes Chris Katembo alikuwa mchoraji mwenza na John Kaduma. John alifariki siku nyingi, zile bangi alikuwa anapuliza zisingemuweka hai muda mrefu. Lakini walikuwa wabunifu kweli kweli.

Tiba

Kumbe bangi ndio zilimuondoa John?alikuwa mtaalam sana kwenye sekta ya uchoraji. RIP JOHN.
 
Nimeona wiki iliyopita tu kwenye gazeti la Sani Pimbi kamtembelea mshikaji wake ulipofika mda wa kuoga Pimbi akapelekewa maji na shemeji yake alipofika bafuni wacha amvutie bafuni Shemeji baada ya mda mshikaji wake akashituka mbona wife harudi? ikabidi avizie kule bafuni kilichotokea hukoo!!! Labda tusubirie Part II
hatari sana....
 
Dah kuna game tulicheza na Born Town huku Meko akiwa South Afrika, kipindi hicho Mandela ndio amekuwa rais wa nchi na kina Meko ni baadhi ya watu walioombwa kwenda kuhamasisha soka South Africa. Kumbe meneja wa timu alimtumia tiketi ya ndege mzee meko bana, mara half time mzee katia timu huku tulishapigwa goli 2 safi.

Kama kawaida ya mzee Meko, goli zote zilirudi na tukashinda mechi.

NB: Mimi nilikuwa mnazi wa Bush Stars.

Hiyo mechi naikumbuka sana
 
mnakumbu gamutu, msosi please, ndumilakuwili alikuwa kiboko. Kuna timu za mpira bön town na bush stars ule mpambano ulikuwa noma. Kila mwezi gazeti likitoka linakuja na misemo mipya. Picha za totoz watamu mno! Ah enzi za mwalimu kuna vitu vilikuwa vinabudurudisha
 
Hivi vijarida virudi tena bwana mi nilikuwa na vipenda balaa
 
Mkuu! Nilikuwa nikitoka kijijini hadi Masasi mjini kuhemea hili jarida kila toleo jipya linapotoka. Wakati mwingine nilikumbana na karaha tele kulipata. Kipato kilikuwa duni nikitegemea ndg yangu aliyekuwa ananitumikisha kutwa 1 au 2 ktk Mgahawa wake kwa ujira wa hili Jarida. Lakini nikilitia mkononi inakuwa raha narudi kijijini mjanja mie.
 
Mkuu! Nilikuwa nikitoka kijijini hadi Masasi mjini kuhemea hili jarida kila toleo jipya linapotoka. Wakati mwingine nilikumbana na karaha tele kulipata. Kipato kilikuwa duni nikitegemea ndg yangu aliyekuwa ananitumikisha kutwa 1 au 2 ktk Mgahawa wake kwa ujira wa hili Jarida. Lakini nikilitia mkononi inakuwa raha narudi kijijini mjanja mie.

Mkuu bila shaka ulikuwa ukirudi kijijini wewe ndo unakuwa Aluatani
 
Nafikiri umaarufu na upinzani wa Mapung'o kwenye Bongo vs mwenzake chepe ulikuwa kama Ronaldo na Messi, kuna game Chepe alichomoka kwa spidi na mpira Beki akamvuta shati ikaavuka, akamvuta bukta ikavuka, akamvuta chup ikavuka pia, ilibidi beki akamate ngozi ya mgongo, nayo ikavutika huku Chepe anakimbia tu.

Baada ya hapo aliachia bonge la shuti, likagonga mwamba na kurudi ndani, refa ndiye aliyemalizia kupiga golini huku mwenyewe anasema "Hii move huwezi kuiacha iende hivi hivi.

Kweli hii move utapata dhambi kuiacha hvi hvi...
 
Mi nilipenda mazoez yao ya mech tu unaweza acha roho hivi hivi...
 
ila lile gazet la ambha sijui limepotea wap coz kuna stori nliipenda sana inaitwa ""ladha ya maisha""na ile ya kina mosha ngosha na mbasha
 
Bila kusahau hadithi yenye msisimko ya 'Maji Mazito' ndani kulikuwa Na Ommy Kiss yaani Omari kissila,mtoto wa maana Vicky Na boss shugadad simkumbuki jina,likitoka lazima baada ya miezi 6 lazima mtu ujifungie ndani mpaka linaisha unampokeza mwingine
 
Back
Top Bottom