Picha: Madenge, Pimbi, Komredi Kipepe

Picha: Madenge, Pimbi, Komredi Kipepe

Mtamile

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2011
Posts
2,838
Reaction score
1,274
kipepe2.jpg


madenge.gif


kipepe.gif


pimbi.gif


sani.gif


kipepe1.jpg


lodilofa1.jpg
 

Basi nakumbuka kuna toleo moja lilitoka miaka ya 80's, Kifimbocheza Apambana na Wachafuzi wa Lugha, aliwavizia vijana kijiweni na kuwasikia wanaelezana stori kama hivi:

A: BASI JANA LILIANGUKA VALANGATI KIJIWENI USISIKIE

B: EHE LIKUWAJE

A: ILIKUWA HEAVY, NIKAKUTANA NA PANGASPY, AKAANZA KUPAKAZA,. KANITIA LOBA, ANASEMA ETI NIMEMCHEZA FIX!

Yaani we ndugu yangu acha kabisa enzi za F1-F4 nilikuwa sikosi toleo la SANI japo hela hata shs 10/= ilikuwa mgogoro kipidi hicho. By the way, Said Bawji yuko wapi sasa? WAMASA hii kampuni ado ipo au ilkufa? Namkumbuka sana na kati ya maachapiho yake niliyotokea kuyapenda sana utotoni ni Kitabu chake kilichokuwa na kichwa USIKU WA BALAA. Humo alikwemo Mzee Ole, Kibibi Gula na wengine siwakmbuki vizuri majina, yaani ilikuwa n balaa tupu!
 
bila kumsahau bob Mazishi na sokomoko

Lodi Lofa pia, tena naona ndiyo yuko hapo kama mgeni mwalikwa wakiwa na Profesa Pimbi. Halafu kulikuwa na mechi ya mpira iliyokuwa inachezwa kati ya ma-Bush Stars na ma-Town stars, bila kusahau vita kati ya Zena na Betina.Acha kabisa, enzi hizo ilikuwa mtu bora achapwe viboko hajaenda prep usku kuliko kusoma SANI halafu akaishia njiani.
 
Dah kuna game tulicheza na Born Town huku Meko akiwa South Afrika, kipindi hicho Mandela ndio amekuwa rais wa nchi na kina Meko ni baadhi ya watu walioombwa kwenda kuhamasisha soka South Africa. Kumbe meneja wa timu alimtumia tiketi ya ndege mzee meko bana, mara half time mzee katia timu huku tulishapigwa goli 2 safi.

Kama kawaida ya mzee Meko, goli zote zilirudi na tukashinda mechi.

NB: Mimi nilikuwa mnazi wa Bush Stars.
 
Ahsante kwa kunikumbusha vya zamani. Enzi hizo nilikuwa sekondari, basi huwa sikosi kwenda Ngamia sokoni pale Tanga kununua gazeti la SANI.
 
hivi zena na betina ule ugomvi wao ulimalizika???
Ha ha ha !!
umenikumbusha mikasa hiyo nilikuwa nacheeeeka!
Mdogo wangu mmoja mtundu tukamwita komredi Kipepe, hakufurahi sana ukimwita lakini ilikuwa burudani tosha!
 
Umenikumbusha marehemu John Kaduma aliyekuwa anachora hizi picha.

Tiba

Kumbe Tiba na wewe ni wa enzi zetu...kumbe huyu jamaa alifariki aisee? RIP...kina Chris Katembo si walikuwa huko pia
 
Last edited by a moderator:
Kumbe Tiba na wewe ni wa enzi zetu...kumbe huyu jamaa alifariki aisee? RIP...kina Chris Katembo si walikuwa huko pia

Ehe Bwana nilikuwepo enzi hizo. Yes Chris Katembo alikuwa mchoraji mwenza na John Kaduma. John alifariki siku nyingi, zile bangi alikuwa anapuliza zisingemuweka hai muda mrefu. Lakini walikuwa wabunifu kweli kweli.

Tiba
 
Ehe Bwana nilikuwepo enzi hizo. Yes Chris Katembo alikuwa mchoraji mwenza na John Kaduma. John alifariki siku nyingi, zile bangi alikuwa anapuliza zisingemuweka hai muda mrefu. Lakini walikuwa wabunifu kweli kweli.

Tiba

Duh kumbe alikuwa akilipuliza eeeh? Nakumbuka tulikuwa tunasubiri kwa hamu sana toleo linalofuata...kikija tunashare kijiji kizima

Cc mwallu DEMBA Munkari Mentor Nicas Mtei Asprin
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom