Picha: Madenge, Pimbi, Komredi Kipepe

Picha: Madenge, Pimbi, Komredi Kipepe

Siku hizi gazeti la Sani limegeuka kuwa la udaku, pamoja na mambo mengine..kipindi hicho magazeti yalikuwa machache halafu mengi hayakuwa ya burudani, vilevile kulikuwa hakuna TV..hivyo basi burudani iliyobaki pekee ilikuwa ni ya gazeti la SANI acha kabisa
 
af nilikua nakatazwa kuyasoma..yatanifundisha tabia mbaya..kwa iyo nilikua nayasomea kwao rafiki yangu...namkumbuka sana madenge,zena na betina..lodi

Ndo kusema ulikuwa unakiuka maagizo ya wazazi.......eeeh?
 
enzi izo tulikua tunasema,sheria zimewekwa ili zivunjwe..hata ivo sani haikunifundisha tabia mbaya
Ndo kusema ulikuwa unakiuka maagizo ya wazazi.......eeeh?
 
Mapung'o alikuwa kwenye gazeti la Bongo

Nafikiri umaarufu na upinzani wa Mapung'o kwenye Bongo vs mwenzake chepe ulikuwa kama Ronaldo na Messi, kuna game Chepe alichomoka kwa spidi na mpira Beki akamvuta shati ikaavuka, akamvuta bukta ikavuka, akamvuta chup ikavuka pia, ilibidi beki akamate ngozi ya mgongo, nayo ikavutika huku Chepe anakimbia tu.

Baada ya hapo aliachia bonge la shuti, likagonga mwamba na kurudi ndani, refa ndiye aliyemalizia kupiga golini huku mwenyewe anasema "Hii move huwezi kuiacha iende hivi hivi.
 
Duh aisee, kweli maisha si mchezo, nakumbuka vichwa vya stori kama
1. Hata ukioga ...
2. Ukubwa wa Boflo ...
3. Unanawa, ...
4. Kula huli ...
5. Ukiona vyaelea ...
6. Sikio halizidi ...

Halafu kuna story za kipelelezi kwenye gazeti la Tabasamu and et Al
1. Wote Wamo
2. Sheshe la wajanja
etc
 
Hivi mechi ya Bush Stars vs Born Town iliimalizika?
 
Ah! Mmenikumbusha Dr. Love Pimbi ...
 
Tunajidanganya kuwa miaka hiyo Mwalimu 'alitufunga' na kushindwa kuwa exposed na dunia lakini kiukweli ukilinganisha wachoraji wa nyakati hizo walikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuonyesha wanachokusudia. Kwa wale wanaoweza kuziangalia hizi picha na kukumbuka zingine za nyakati hizo bila shaka watakubaliana nami, japo sasa wapo akina KP, Gayo, King Kinya nk.
Kitu kingine kinacholifanya badiko lako liwe na thamani ni ujinga wetu uliopelekea kuwa watu tusiopenda kusoma vitabu. Chukulia unahitaji machapisho kama haya au kama kitabu cha Sani, kuwachekesha fisi nk, ni vigumu sana kupatikana kwenye duka lolote la vitabu!
 
Back
Top Bottom