Mag3
Platinum Member
- May 31, 2008
- 13,064
- 22,757
Nimemfuatilia sana huyu jamaa kwenye mkutano wa Chadema uliokuwa unahutubiwa na Mh. Tundu Antiphas Lissu, alivyokuwa anahangaika, mara atoe kiredio chake mfukoni kama vile anawasiliana na mtu asiyeonekana, mara atafute namna ya kusogea karibu zaidi na alipo Mh. Lissu, mara atafute nafasi ya kusikia vizuri zaidi anayasema...lakini wana Chadema hata hawakuhangaika naye!
Sasa nikabaki najiuliza, je hali ingekuwaje kama mwana Chadema ndiye angetinga katika mkutano wa CCM na magwanda yake halafu mara anapiga picha, mara kama vile anawasiliana na mtu, mara anajaribu kusogea na alipo mgombea. Je, kweli angetoka salama?
Nawavulia kofia wana Chadema kwa kutomjali huyu na kutohangaika naye katika hizo juhudi zake hizo pamoja na kuvaa fulana ya hapa kazi tu na. kofia ambayo yawezekana ni ya wana Usalama au vijana wa UVCCM.
Sasa nikabaki najiuliza, je hali ingekuwaje kama mwana Chadema ndiye angetinga katika mkutano wa CCM na magwanda yake halafu mara anapiga picha, mara kama vile anawasiliana na mtu, mara anajaribu kusogea na alipo mgombea. Je, kweli angetoka salama?
Nawavulia kofia wana Chadema kwa kutomjali huyu na kutohangaika naye katika hizo juhudi zake hizo pamoja na kuvaa fulana ya hapa kazi tu na. kofia ambayo yawezekana ni ya wana Usalama au vijana wa UVCCM.