Picha: Hii imekaaje?

Picha: Hii imekaaje?

Status
Not open for further replies.
Kwani rais hajui kama akishasalimiana na mtu anatakiwa kuachia mkono? Pia sidhani kama ni sahihi kumwacha kila raia kushikana mkono na rais. Waachiwe wenye uelewa wa kiprotokali za kiusalama tu!
 
Kwani rais hajui kama akishasalimiana na mtu anatakiwa kuachia mkono? Pia sidhani kama ni sahihi kumwacha kila raia kushikana mkono na rais. Waachiwe wenye uelewa wa kiprotokali za kiusalama tu!
Mambo mengine anatia aibu
 
Sijui protocol za usalama lakini naona hii si nidhamu!Angalieni mkono wa huyo jamaa wa usalama!View attachment 394980 ulivyomshika mtu anayesalimiana na Rais!
Wadau mna maoni gani?Hii imetokea leo

Nadhani na hapa chini Bon angechelewa kidogo jamaa angeenda kumshika mkono aachie mkono wa Rais!Sio kwa jicho hilo analomkata aisee
View attachment 394999 View attachment 394980
Skiza nikuambie,watu wa usalama wa taifa wanajua kwanini kiongozi au viongozi wanaposalimiana kwa kushikana mikono walinzi wanakuwa makini mno,fuatilia picha nyingi alafu angalia macho au mikono ya walinzi utagundu.
 
Hana adabu huyo jamaa.
Upambe ndiyo unamsumbua zaidi ya kazi
 
Hiyo kitu hairuhusiwi ku hold/kumshika kiogozi wa juu kwa mda hiyo ipo popote pale duniani!

Kuna wengine wanatumia njia hiyo kumdhuru rais,

Hawa Jamaa wanajua sana majukumu yao hawabahatishi na rais hawezi kuhoji
Uko sawa sana ndugu,watu wanakimbilia kulaumu tuu...hehehe sisi wengine u layman wa masuala ya ulinzi unatusumbua.Baada ya kuuliza kwanza naona humu mtu anamuita mlinzi limbukeni.Sitaki kuhusisha siasa hapa ila wanaobeza naweza kuwatambua
 
Sasa Pasco kama Rais bado alikuwa anateta jambo na muhusika inakuwaje?Haya mambo sijaona sehemu nyingine
kama hujaona sehemu nyingine basi jua umechelewa ndo uingie google sasa wkati umefika ujue
 
Uko sawa sana ndugu,watu wanakimbilia kulaumu tuu...hehehe sisi wengine u layman wa masuala ya ulinzi unatusumbua.Baada ya kuuliza kwanza naona humu mtu anamuita mlinzi limbukeni.Sitaki kuhusisha siasa hapa ila wanaobeza naweza kuwatambua
Mtu huyo hakuwa amekaguliwa kabla ya kufika radius ambayo Rais atapita?
 
Skiza nikuambie,watu wa usalama wa taifa wanajua kwanini kiongozi au viongozi wanaposalimiana kwa kushikana mikono walinzi wanakuwa makini mno,fuatilia picha nyingi alafu angalia macho au mikono ya walinzi utagundu.
Weka hata picha!
 
Mtu huyo hakuwa amekaguliwa kabla ya kufika radius ambayo Rais atapita?
hata kama amekaguliwa au la ila dhamira ya mtu huwezi kuikagua sababu ipo moyoni kwake.Sijui ni swali umeniuliza au hyo question mark imekaa bahati mbaya?hahaha
 
Hujui ishu za usalama . hebu soma micro expresion, utagundua haikuwa moment nzuri, ilibore kama Mh. Rais nae alikuwa kama kamaindi hivi.

Hapo mlinzi wake lazima awe makini, maana ni kazi yake huwa hawakurupuki.

Katika huelewa wa haraka haraka yawezekana kulikuwa na misunderstanding na picha ya pili yaonyesha huyo jamaa mwingine aliye mshika mkon Mh.Rais alienda kuliua soo kiaina, ila mlinzi bado yupo atention.

( kwa mawazo yangu)
 
IMG-20160822-WA0022.jpg
IMG-20160822-WA0022.jpg
 
Hao mameya wa CDM si walitoa tamko la kutohudhuria shughuli zote zitakazomhusisha rais jijini DSM baada ya ile ya ufunguzi wa Daraja la Kigamboni kisa wanadhalilishwa na kuhujumiwa?

Imekuaje tena?
 
Mtu anayelindwa kwa mfano kiongozi wa nchi huwa wakati wa kusalimiana humpi mkono mpaka yeye aanze kukunyooshea. Kilichotokea hapo leo ni kwamba JPM alipomaliza shughuli aliteremka kwenda kuwapa mkono watu waliokuwa wameketi mstari wa mbele kabisa akiwemo Taslima.
Kutokana na kazi nzuri aliyoifanya wakili huyu JPM alipofika kwake alimpa mkono na Taslima alipoupokea JPM aliendelea kuongea naye akiwa bado ameushikilia. Sasa kwa minajili ya ustaarabu Taslima asingechomoa mkono wake mpaka pale JPM alipouachia.
Huyo mlinzi alizidisha munkari kidogo, maana hawa watu wetu wa idarani wana utamaduni wa kuzidisha mambo ya kazi yao mara nyingi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom