Picha: Hawa ndio walipuaji mabomu Arusha

Picha: Hawa ndio walipuaji mabomu Arusha

Binafsi siliamini kabisa jeshi LA polisi.
Henry Kilewo alibambikwa kesi ya ugaidi lkn mwisho Wa Sikh kesi ikayeyuka,pia yule Ambrose aliekamatwa kwa kulipua kanisa kesi take iliishia wapi?
Hats yule kada Wa CUF aliekamatwa kule Zanzibar nae ilikuwa kaonewa,
name waziri mkuu aliwahi kuwadanganya watanzania kuwa wamewakamata waarabu mpakani huko Arusha wakati alijua FINA kuwa wameonewa kwa sababu ya dini yao.
Huu ujinga unaofanyika ambapo amituhumiwa mtu mwenye imani ya kiislaam mnaita ugaidi name kunasibisha makosa take name dini ya kiislaam ,IPO Siku tutakuwa wakimbizi,
Ingekuwaje kama viungo vya binaadam vingekutwa taasisi ya kiislaam?
Ingekuwaje kama skendo ya mchungaji gwajima ingemkuta Shekh au Imaam?
Wale mnaokejeli ndevu name kizihusianisha name wislaam,mnataka kutuaminisha kuwa mungu we nu yesu alikuwa mwislaam? maana sanamu zote makanisani kwenu zinaonesha akiwa name ndevu za kutosha.
vipi Plato,Socrete na Aristotle NATO walikuwa waislaam kutokana name kuwa name ndevu nyigi?
ache I chuki

Unaweza kuwa na mchango mzuri ila usieleweke vizuri kwa ajili ya uchanganyaji wa lugha. Kwani kwako kuandika kiswahili fasaha kinachoeleweka na kukubalika kwa waungwana unapata shida gani? Hizi lugha za face book ukizileta jukwaa hili la great thinkers wengi hawatasoma post yako.Unaruhusiwa kuandika bandiko lako hata kwa lugha ya kiingereza ila uwe na uwezo nayo.
 
chadema semeni sasa;
Je kwa hilo nalo mtakataa?
Lema ukoo wa lema yaani familia ya lema godbless, looh.
Mngeweza huyo lema mngembadilisha jina mapema;
Ngoja nikuache tu maana niliyokupa ya moyoni yanatosha


Sent from my BlackBerry 9320 using JamiiForums
 
.
Vema kama wangeweza wangewatia vitanzi wote tuwasahau kabisa.
mkuu hao ni wanachama wa chadema?naana si tulisema chadema wamejilipua pale A town?na je vipi zile million Mia za Lukuvi zimeshatoka?
 
ugaidi_3.jpg

Sita washtakiwa kwa ugaidi Arusha
WATUHUMIWA sita wanaodaiwa kurusha bomu katika mgahawa wa Vama Tradition jijini Arusha, Julai 7, mwaka huu, na kusababisha watu wanane kujeruhiwa huku mmoja wao akikatwa mguu, wamepandishwa kizimbani na kusomewa mashtaka manne.

Watuhumiwa hao ambao walikamatwa juzi kwa nyakati tofauti, walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Arusha jana chini ya ulinzi mkali wa polisi, majira ya saa 7:30 mchana.
Baada ya kufikishwa mahakamani hapo, washtakiwa hao, Shabani Mmasa, Athumani Huseini, Mohamedi Nuru, Jafari Lema, Abdul Salum na Saidi Temba, walisomewa mashtaka manne na Mwanasheria wa Serikali, Augustino Kombe.

Mbele ya Hakimu Mkazi, Rose Ngoka, washtakiwa wote walisomewa shtaka la kwaza la kupanga njama za kufanya ugaidi kinyume na sheria ya ugaidi ya nchi.
Washtakiwa hao walidaiwa kuwa Februari na Julai mwaka huu, walipanga njama za kufanya ugaidi katika mgahawa wa Vama uliopo maeneo ya Gymkhana jirani na Mahakama Kuu jijini Arusha na kujeruhi watu wanane waliokuwemo ndani ya mgahawa huo.

Waliojeruhiwa katika kadhia hiyo ni Deepack Gupta aliyekatwa mguu wa kushoto, Manisha Gupta, Prateek Javey, Manci Gupta, Mahish Gupta, Ray Rajin, Ritwik Khandehral na Vinpd Suresh.
Katika kosa la pili, washtakiwa wanadiwa kufanya ugaidi ambapo mwanasheria Kombe alisema mnamo Julai 7, mwaka huu, walirusha bomu katika mgahawa huo na kusababisha
kujeruhi watu wanane waliokuwamo ndani ya mgahawa huo.

Kosa la tatu lilitajwa kwa washtakiwa Lema na Huseini ambao walidaiwa mahakamani hapo kuwa walihusika kutoa silaha ambazo ni bomu zilizohusika katika shambulio hilo.
Shtaka la nne liliwahusisha washtakiwa wote sita wakidaiwa kutoa ushirikiano katika kufanikisha kutendeka kwa kosa la ugaidi na kukiuka vifungu kadhaa vya sheria ya ugaidi vinavyokataza mtu yeyote kujihusisha na masuala ya ugaidi.

Hakimu Ngoka mara baada ya kutajwa kwa mashtaka hayo, aliwazuia wasijibu chochote kwa kuwa mahakama hiyo haina uwezo wa kusikiliza kesi hiyo.

Aidha, mwanasheria wa serikali, Kombe aliiambia mahakama hiyo kuwa upelelezi wa kesi hiyo bado haujakamailika, hivyo kuiomba ipange tarehe nyingine ya kutaja kesi hiyo.
Baada ya maombi hayo, hakimu Ngoka aliahirisha kesi hiyo hadi Agosti 6, mwaka huu, itakapokuja kwa ajili ya kutajwa tena, huku washtakiwa wakipelekwa rumande.
[/QUOTE ppl production 2014-Tz bwana mbinu zile zile,mambo Yale Yale yaani hata ubunifu hatuwezi?
 
Bado tunataka kujua ile milipuko ya olasiti na soweto. Isije kuwa haya ni kufunika tu mambo yaliko anzia. Mtoto wa mkulima alifikishwa mahakamani kwa kusema "wakileta fujo wapigeni" lakin aliyesema atahakikisha nchi hii haitawaliki na kisha kutokea milipuko ya mabomu na tindikali ka achwa na madhara yanatokea kama hivyo tusikiavyo na wengine wakiona madhara wazi wazi
 
Inshaalah haki itajulikana kama kweli wanahusika au ni usaniii mwingine polisi

kila mwenye akili timamu hawezi kuunga mkoni mauaji ya watu wasio na hatia na hawezi kuwahukumu au kuwatukana kundi la watu kwa makosa ya watu wengine.

Udini unaopandikizwa na baadhi ya watu utaleta maafa makubwa katika nchi yetu na duniani kwa ujumla.

Mwenyezimungu ibariki tanzania,

Movie nyingine ya ccm hiyo. Mtu kama wewe hawawezi kukusikiliza. Wao Wanataka maslahi yao kwanza. Sasa hivi wanajiweka sawa kwa uchaguzi mwakani kwani wanajua fika wataulizwa swali la usalama wa raia.
 
Ndevu ni Sunna. Walisema pia kuna Imamu,sijui ndio yupi hapo?
 
Inshaalah haki itajulikana kama kweli wanahusika au ni usaniii mwingine polisi

kila mwenye akili timamu hawezi kuunga mkoni mauaji ya watu wasio na hatia na hawezi kuwahukumu au kuwatukana kundi la watu kwa makosa ya watu wengine.

Udini unaopandikizwa na baadhi ya watu utaleta maafa makubwa katika nchi yetu na duniani kwa ujumla.

Mwenyezimungu ibariki tanzania,

Mkuu nashukuru kwa kulisema hili, maana watu wengi (reference majibu hapa JF) wanatumia miwa ya udini kusoma na vinywa tumelewa pombe ya udini tuliyonyweshwa na wanasihasa kwa malengo yao. Naona wamefanikiwa kutugawanya. Amka wewe mtanzania kamataa ubaguzi wa kila aina.
 
Kama kawa maustadh. Hapa hawana kazi na hawakusoma ila wanataka watu wote waishi kama wao. Hawa watu hawa jamani, hivi kwa nini wasipigwe mvua ya maisha jela?
 
ukitaka uwe gaidi au jambazi bila kushikwa haraka usiguse wahindi

kila aliyekorofisha wahindi tanzania hakufika hata wiki alidakwa na kushughulikiwa.... nilipata hiyo fact kutoka kwa mhindi mmoja alikua keshakunywa amelewa

na alitoa mifano zaidi ya kumi kwa kila aliyemdhuru mhindi, alishughulikiwa hata kama ni traffic offense...
 
Inshaalah haki itajulikana
kama kweli wanahusika au ni usaniii mwingine polisi

kila mwenye akili timamu hawezi kuunga mkoni mauaji ya watu wasio na
hatia na hawezi kuwahukumu au kuwatukana kundi la watu kwa makosa ya
watu wengine.

Udini unaopandikizwa na baadhi ya watu utaleta maafa makubwa katika nchi
yetu na duniani kwa ujumla.

Mwenyezimungu ibariki tanzania,

yani muuwe watu alafu ujifiche kwenye kivuli cha dini? Endeleeni na mabomu yenu kama hatujamuita Muisraeli!
 
Back
Top Bottom