Mimi nawaambia nyie Vijana hamuwajui ZITTO na Kitila Mkumbo,ndo mwanzo wa mwisho wa zama za CHADEMA hizo! Wapumbavu humu wanasema eti Nyota! Nyota ?! Hao watu wanatumia akili si ushabiki wa kijinga wa vijana wa CHADEMA waliojazana humu Jf.Kwa taarifa yenu hakuna mwanasiasa anayeweza kujenga hoja kwa sasa ndani ya CHADEMA anayeweza kumkaribia ZITTO wala Mkumbo,wengi wenu ni waropokaji tu kama akina Tundu Lissu, Mnyika n.k.
Ukweli ni kwamba kwa muda mrefu CHADEMA imekuwa na siasa za matukio na matusi na si siasa za hoja! Jiulizeni ni kweli CCM imewachosha wengi hapa nchini wakiwemo wazee wetu waasisi aina ya kina Joseph Warioba lakini hata mara moja hawajawahi kuifikiria CHADEMA kama Chama mbadala wa CCM! Ni kwa nini? Wazee hawa wanajua CHADEMA ni mkusanyiko fulani unaoongozwa na remote ya familia tokea Tengeru pale kwa Mzee Mtei kwa maslahi ya Familia hiyo na si Watanzania kama wanavyowadanganya majuha wao!
Unapo ona binti wa mtu makini kama Joseph Warioba anakimbilia kuchukua kadi ACT - Wazalendo ,kwani siku zote hakuona CHADEMA ipo kama chama cha siasa! jua kuna "consultations"!
CHADEMA hacheni kuweweseka,hata wana wa Israel walipoanza safari ya kutoka Misri wengi walijua Musa ndiye atakayewafikisha Nchi ya Ahadi lakini sivyo Musa alifia Njiani! Ni akini Haruni ndo waliwafikisha Kanaani Nchi ya Ahadi!
Leo mnambeza Zitto lakini amini nawaambia Zitto Zuberi Kabwe is a very smart and intelligent politician of our time!
Wakati CHADEMA wamejifunga kwenye ndoa ya Mkeka na CUF,NCCR,NLD ndo Zitto amewasoma na kuwapa big blow!
Kwanza umoja wa UKAWA ni umoja wa mashaka hilo halina ubishi kwa mtu makini.Zitto ameweka TEGO baya kote kwa CCM na UKAWA. Watakaokosa nafasi kote they are likely to join ACT - Wazalendo than any political Party. Kwahiyo msije shangaa baada ya Uchaguzi Mkuu Zitto ndo akawa na turufu ya Kuunda kambi rasmi ya Upinzani Bungeni! Ikitokea hivyo ndo CHADEMA mtawajua CUF ni nani after all mlishawaita Chama cha Mashoga na kejeli nyingi za akina Tundu Lissu za CCM B.
Lingine Tambueni kuwa Zitto hana cha Kupoteza kwa wakati huu anajijenga kama kiongozi makini wa upinzani ajaye hapa Nchini! Baada ya Uchaguzi huu Mkuu Dr. Slaa kwenda lala,John Cheyo kwenda lala,Mrema kwenda lala,Dr. Makaidi kwenda lala,Maalim Seif na Prof.Lipumba kwenda lala! Wanabaki "ring leaders" Zitto Kabwe,James Mbatia na Mbowe! Kati yao who can be trusted ?! Ni obvious kuwa ZITTO ndo anakwenda kuwa Icon wa siasa za upinzani hapa Nchini very soon! Na mwisho kwa sasa hakuna mwanasiasa wa upinzani aliyejijenga Kimataifa na kwa taasisi za ndani kuliko ZittO Zuberi Kabwe! KAMA UNABISHA ACHA MATUSI JENGA HOJA.