Picha: ACT-Wazalendo Waitikisa Songea

Picha: ACT-Wazalendo Waitikisa Songea

Mimi nawaambia nyie Vijana hamuwajui ZITTO na Kitila Mkumbo,ndo mwanzo wa mwisho wa zama za CHADEMA hizo! Wapumbavu humu wanasema eti Nyota! Nyota ?! Hao watu wanatumia akili si ushabiki wa kijinga wa vijana wa CHADEMA waliojazana humu Jf.Kwa taarifa yenu hakuna mwanasiasa anayeweza kujenga hoja kwa sasa ndani ya CHADEMA anayeweza kumkaribia ZITTO wala Mkumbo,wengi wenu ni waropokaji tu kama akina Tundu Lissu, Mnyika n.k.

Ukweli ni kwamba kwa muda mrefu CHADEMA imekuwa na siasa za matukio na matusi na si siasa za hoja! Jiulizeni ni kweli CCM imewachosha wengi hapa nchini wakiwemo wazee wetu waasisi aina ya kina Joseph Warioba lakini hata mara moja hawajawahi kuifikiria CHADEMA kama Chama mbadala wa CCM! Ni kwa nini? Wazee hawa wanajua CHADEMA ni mkusanyiko fulani unaoongozwa na remote ya familia tokea Tengeru pale kwa Mzee Mtei kwa maslahi ya Familia hiyo na si Watanzania kama wanavyowadanganya majuha wao!
Unapo ona binti wa mtu makini kama Joseph Warioba anakimbilia kuchukua kadi ACT - Wazalendo ,kwani siku zote hakuona CHADEMA ipo kama chama cha siasa! jua kuna "consultations"!
CHADEMA hacheni kuweweseka,hata wana wa Israel walipoanza safari ya kutoka Misri wengi walijua Musa ndiye atakayewafikisha Nchi ya Ahadi lakini sivyo Musa alifia Njiani! Ni akini Haruni ndo waliwafikisha Kanaani Nchi ya Ahadi!
Leo mnambeza Zitto lakini amini nawaambia Zitto Zuberi Kabwe is a very smart and intelligent politician of our time!
Wakati CHADEMA wamejifunga kwenye ndoa ya Mkeka na CUF,NCCR,NLD ndo Zitto amewasoma na kuwapa big blow!
Kwanza umoja wa UKAWA ni umoja wa mashaka hilo halina ubishi kwa mtu makini.Zitto ameweka TEGO baya kote kwa CCM na UKAWA. Watakaokosa nafasi kote they are likely to join ACT - Wazalendo than any political Party. Kwahiyo msije shangaa baada ya Uchaguzi Mkuu Zitto ndo akawa na turufu ya Kuunda kambi rasmi ya Upinzani Bungeni! Ikitokea hivyo ndo CHADEMA mtawajua CUF ni nani after all mlishawaita Chama cha Mashoga na kejeli nyingi za akina Tundu Lissu za CCM B.
Lingine Tambueni kuwa Zitto hana cha Kupoteza kwa wakati huu anajijenga kama kiongozi makini wa upinzani ajaye hapa Nchini! Baada ya Uchaguzi huu Mkuu Dr. Slaa kwenda lala,John Cheyo kwenda lala,Mrema kwenda lala,Dr. Makaidi kwenda lala,Maalim Seif na Prof.Lipumba kwenda lala! Wanabaki "ring leaders" Zitto Kabwe,James Mbatia na Mbowe! Kati yao who can be trusted ?! Ni obvious kuwa ZITTO ndo anakwenda kuwa Icon wa siasa za upinzani hapa Nchini very soon! Na mwisho kwa sasa hakuna mwanasiasa wa upinzani aliyejijenga Kimataifa na kwa taasisi za ndani kuliko ZittO Zuberi Kabwe! KAMA UNABISHA ACHA MATUSI JENGA HOJA.

Siku zote muongo ni bingwa wa kuongea hatukatai zitto ni bingwa wa kujenga hoja sasa hizo hoja ndo zimemfanya kuwa msaliti?
 
Molemo accept the facts, we said mlituona wajinga......think tankers wa chadema mpaka ilipofika pale ni aina zito na prof Mkumbo. unless wewe sio frontier ndani ya chadema

Dealing with those people haikutakiwa wapayukaji kama akina Tundu Lissu, Godbless Lema na aina msigwa!! eti na za sugu!!

utaeneza chuki sana, utatumia nguvu nyingi, utatukana na kusonya, utauma meno....ila si kila unayemchukia wewe lazima achukiwe na wengine ndio siri na utashi ambao Mungu ametupa

Mbowe alitumia gharama kubwa mpaka kutunga hekaya za ajabu........ili zittto achukiwe ...lakini yako wapi?

wewe Molemo utaaandika sana habari za chuki; ila muda utakuonea aibu na kukutupa, uakimbia jukwaa

ukichukua siasa ni kama football game na timu yako imshindwa the best way ni kuangalia mmekosea wapi

Zitto kazaliwa 76 tu , ni mdogo mno na ana miaka mingi ya kuishi.....atasumbua tu, hata kama mtatumia gharama zote kumzimisha, ila ataamka tu

WIMBO WA MSALITI haulipi tena

Ninatamani sana, mbowe aseme....'zitto alienda kutoa siri hii na hii na hii kwa serikali, na CDM ikaathirika hivi na hivin na hivi'' hili hamuwezi kulisema wala kupima...............hatimaye kiasili wimbo wa usaliti unaanza kuchuja

November ACT itakuwa na wabunge wengi ( andika mahali) tena wengi kuliko chadema, kuliko nccr, kuliko cuf, etc.,ACT kitakuwa chama kikuu ch upinzani; chadema by then kitakufa tu...'maana hamna namna nyingine ya kukiokoa' kitakufa tu!

kwa nn? hamna mawazo mapya, hamna uongozi mpya, ni watu walewale, mawazo yale yale, wanafanya vile vile na kutegemea results tofauti???

Hivi kwa nini hata mara moja tukawa wakweli wa nafsi zetu kuwa Zitto alizushiwa yale kwa sababu ya mauongozi ndani ya chadema?

Hivi Lissu anajenga chama kweli??

Wimbo eti ni tawi la CCM....ni wa kujifariji tu..utachuja nao, andaa Lyrics za wimbo mwingine; utakosa utakaa kimya

Ongea uongeavyo hiyo ni ccm siyo ACT iliyosimama peke yake ccm walishakiandaa hicho chama walifikir zitto akienda Act bas wale wabunge vijana watamfuata saiv mmebaki kuwa watabir mala wabunge wengi watahamia sasa sijui watahaniaje wakiwa wabunge wakat bunge linavunjwa mwaka huu wanakua raia wa kawaida had waombe tena na hata hao wakienda chadema bado itateua watu makini na kauli hizo hazihitaj ufanunuz kwa nn act ipo.
Ipo kwa ajili ya kuisaidia ccm kwa kuvunja vyama vya upinzani mana kila siku zitto kauli yake kuna wabunge watakuja na mtawangoja sana.

Na kutuambia chadema imefika kwa ajili ya zitto na mkumbo labda wewe kwa mawazo yako kwani sisi hatuoni yanayofanywa na ccm? Hao ccm wangekuwa wasafi unafikir vyama vya upinzan vingepata nafasi? Sisi wenyewe raia ndo tunataka mabadiliko kuinusuru inchi ila sio kigezo cha mtu fulan tumeshaona na kusikia utendaji wa ccm mabadiliko ni ya watu sio mtu kama watu hawapo tayar hata uwe mjenga hoja vp bado utachemka tu

Pia unatuambia Act kitakuwa chama kikuu cha upinzabi lengo lake sio kuwaondoa ccm bali ni kuwa chama kikuu cha upinzani kwa hiyo furaha ya Act ni kuwa chama cha pili baada ya ccm na si kuwakomboa watanzania.
Ukituambia uongoz ulele watu walewale kwani zitto na kitila ni watu wapya na yule mama mwenyekit ktk medani za siasa? Halafu na ww unategemea mapya kwa hao lengo kuu la hao ni uongoz na usalit nani asiyewajua?
 
Nia hasa ya ACT ni kupingana na CHADEMA wala sio kuingoa CCM
 
ccm wanatumia hela nyingi uisabalatisha chadema.hawataweza kwani chadema imeshajiimalisha sana.hata hao wengi wao ni wana ccm. ccm inatumia wajumbe wa nyumba kumi kuhakikisha mikutano ya wasaliti inajaza watu. ccm imechokwa hata waje na rangi gani
 
Nia hasa ya ACT ni kupingana na CHADEMA wala sio kuingoa CCM

huo ndio mwisho waupeo wako wa kufiri.hulaumiwi nihaki yako.
wewe unaipenda sana cdm nakushauli na kuwashauli viongozi wenu msiwataje taje act.waacheni wafanye siasa act.
 
ccm wanatumia hela nyingi uisabalatisha chadema.hawataweza kwani chadema imeshajiimalisha sana.hata hao wengi wao ni wana ccm. ccm inatumia wajumbe wa nyumba kumi kuhakikisha mikutano ya wasaliti inajaza watu. ccm imechokwa hata waje na rangi gani

mtapona mwaka huu.zito kasema hao wabunge wasafi wenu wamefanya nini juu ya taifa hili? pia kasema hata yeye anaona nia nzuri ya kuidondosha ccm nikuungana lakini vyama viungane kwa maslahi ya wananchi wanyonge nasio viungane ili kugawana vyeo tu.
 
Mtaongozwa mara ngapi kwani na mapadre hujui kuwa katoliki ndio imeratibu hata uongozi uliopo madrakani sasa Kuanzia Rais mawaziri hadi BAKWATA.

CCM OYEEE

Tunalijua hilo.

Si ndiyo kwa maana tunasema nchi hii kuna mfumo kristo??

Lakin mfumo kristo huo ndani ya ccm ni nafuu na tunapambana nao na matokeo yanaonesha very positive.

Sasa kuwapa nchi chadema ni kana kwamba tumewapa kanisa moja kwa moja.

Wewe huoni mapadre walivyojaa Chadema.

Ikulu msahau nyinyi wazandiki.
 
CHADEMA walimfukuza Naibu Katibu Mkuu Zitto mwaka mmoja kabla ya uchaguzi mkuu!Badala ya kushikamana wao wanafukuzana kwa tuhuma za ki p u u zi kabisa!

ACT itampunguzia sana kura Dr Slaa

Nnyambara, nkulumba mwana ghwa Kyala

That was stupid move ever done by CDM! katika siasa unaweza ukajifanya mjinga kwa kutaka kikubwa zaidi, unaangalia lengo kwanza na sio mtu mdogo kama zitto, they spend all money, efforts, time, and brains kucheza na zitto; wakamkomaza na kumkuza mno

they failed wakaenda kujiunga na ukawa another stupid move ever....hadhi ya chadema muda ule haikuwa ya kuungana na Mbatia ( mbunge wa kuteuliwa wa Kikwete) haikuwa ya kuungana na CUF!!

Hivi wale wanachadema wanaoona wanajua siasa, hivi kweli mnamsaidia Mbowe kufikiri?

kama ningekuwa mimi CDM na intelijinsia inaonyesha kabisa Zitto atahama, ingekuwa muda mzuri wa kuiua ACT kwa kumpa zitto ukaribu!!!!!! tangaza mmemsamehe, mpe cheo ambacho hakipo; ACT isingekuwa threat hivi!!!!!!!!!


CDM mnafikiri kwa akili zenu hizi za kipuuzi mnaweza kupewa nchi?

mnafikiri Kikwete alikuwa mjinga kumweka mwakyembe na mwandosya karibu? au kumpa uenyekiti wa tume ya katiba warioba? watu ambao ni maadui zake? he knowa politics sana zaidi ya mbowe na slaa!! hata kama tunamwona mzembe kwenye issues zingine, lakini anavyo deal na maadui zake yuko juu kikwete


ACT ni mtoto wa chadema. period kama ambavyo vyama vingine vilivyozaliwa kutoka CCM! lakini makosa ya kuanzishwa NCCR, CHADEMA, UDP, n.k na wale waliokuwa maadui wa Nyerere, CCM imebadilika na kwa miaka 23 sasa hatujaona dalili ya kuanzishwa chama kingine kutoka CCM ndio maturity

CCJ ambayo wanzilishi ni akina sita na Nape....tumeona hawa watu CCM ilivyowapaisha na kukiua CCJ kifo cha asili

CDM ni nani aliyewaroga??


ACT itakuwa itapaa ita shine, yes tuko nyuma yao wengi tu na wengi hawako humu! ni wananchi wa kawaida kabisa kila kona ya Tanzania!

Tangu 2009 mlipoanza kumtenga zitto, kimbilio lake likawa kwa wananchi na kusema yale ya wananchi.......mlipoanza kushindana naye, kwa matusi na sauti kuuu....likuwa mnashindana na wananchi na sio Zitto

Zitto aliwapa muda wa nyie kujitafakari na kujirudi, hamkufanya hivyo


ACT for life!!!
 
Back
Top Bottom