Physics ya A- Level inanitesa

Physics ya A- Level inanitesa

BARDIZBAH

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2017
Posts
5,906
Reaction score
11,728
Habari wanajamvi ??

Wanajamvi mimi ni mwanafunzi niliyemaliza kidato cha nne mwaka jana(2016), ufaulu wangu katika masomo ya sayansi ni mzuri hivyo nina mipango ya kwenda Advanced level comb PCB au PCM

Lakini tangu nilipo anza kusoma physics yaani nakata tamaa maana kuna ki subtopic kinaitwa PROJECTILE MOTION yaana kila nikifanya swali lake nakosa. Please wanajamvi naombeni ushauri wenu katika somo hili.

Maana kubadilisha comb siwez sababu nilisoma TECHNICAL SCHOOL hivyo siwez soma comb za art wala CBG.
 
Motivation yako kubwa iwe ni kutengeneza missiles guided by laser or gps. Ukiwaza hivyo, projectile motion ni kama kula nyanya. Pitia hapa, lakini lazima uwe na uwezo wa kufikiria mbali au kufanya mambo mengine kwa hisia mfano ukirusha jiwe linaendaje hadi kutua? Je ukirusha jiwe na mwenzako upande mwingine akarusha yakakutana angani, kitatokea nini?
https://www.khanacademy.org/science/physics
 
Naipenda physics kulikooooo ebu jaribu kucheki video YouTube za professor mmoja anaitwa Walter lewin halafu utakuja unipe mrejesho Fanya ivo kijana
Sasa mkuu baada ya kumsearch nifanyaje?
 
una raha sana unasoma kipindi ambacho kuna google,u tube una smart phone matuition yapo kibao walimu wa physics wapo kibao ila unasema bado inakusumbua dah aisee ungesoma kipindi chetu jee hi physics kaza kijana komaa acha kulialia...
 
Topic za mwanzo mwanzo zinakutia kiwewe ukifika za mbele mbele huko si ndio utakimbia shule....unasoma umalize topic au uelewe? Read it kwa pace yako...try and try several times mpaka uweze...kumbuka kukata tamaa ni dhambi.
Haimaanishi kila topic ya mwanzo ni nyepesi mkuu
 
Sasa mkuu baada ya kumsearch nifanyaje?
Msikilize ni moja ya professor wazuri wa physics anaweza kukuinspire na anavideo zake ambazo kafundisha sana physics kwangu mm he is the best aisee hutojuta kumsikiliza
 
Usikate tamaa Mkuu kaza buti sana. Usisite kuomba msaada kwa wanafunzi wenzio na Mwalimu pia. Kila la heri. Kumbuka penye nia pana njia.
 
duh....kama projectile ni ngumu bora utafute masomo mengine mapema.

Kuna madude mengine huko mbele utakutana nayo hayana hata uhusiano na maisha yako ya kila siku. Afadhali hiyo projectile.

😀😀😀

NB: nakutisha tu dogo.....komaa hivyo hivyo kitaeleweka tu.
 
duh....kama projectile ni ngumu bora utafute masomo mengine mapema.

Kuna madude mengine huko mbele utakutana nayo hayana hata uhusiano na maisha yako ya kila siku. Afadhali hiyo projectile.

😀😀😀

NB: nakutisha tu dogo.....komaa hivyo hivyo kitaeleweka tu.
Na tayari ushamtisha!! Hahahaha physics nouma ukianza kukata tamaa mapema.
 
Habari wanajamvi ??
Wanajamvi mimi ni mwanafunzi niliye maliza kidato cha nne mwaka jana(2016) . ufaulu wangu katika masomo ya sayansi ni mzuri hivyo ninamipango ya kwenda Advanced level comb PCB au PCM
Lakini tangu nilipo anza kusoma physics yaani nakata tamaa maana kuna ki subtopic kinaitwa PROJECTILE MOTION yaana kila nikifanya swali lake nakosa .please wanajamvi naombeni ushauri wenu katika somo hili .
Maana kubadilisha comb siwez sababu nilisoma TECHNICAL SCHOOL hivyo siwez soma comb za art wala CBG.
Wabongo bana, unasoma madude magumu namna hii alafu baadaye ukiisha wiva vizuri unagombea ubunge au Unapewa ukuu wa Wilaya badala ya kwenda kalakana au Hosptali
 
Msikilize ni moja ya professor wazuri wa physics anaweza kukuinspire na anavideo zake ambazo kafundisha sana physics kwangu mm he is the best aisee hutojuta kumsikiliza
Shukran mkuu
 
Naipenda physics kulikooooo ebu jaribu kucheki video YouTube za professor mmoja anaitwa Walter lewin halafu utakuja unipe mrejesho Fanya ivo kijana
moja ya maproffesor niliokua nafuatilia sana lectures zake, mzee yupo lafu lafu lakini deep vibayaaa
 
Back
Top Bottom