Photo interpretation

Photo interpretation

Hess

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2012
Posts
593
Reaction score
675
Kwa wanaoweza kunisaidia ku-interpreter hii picha

CCM.jpg
i. Picha inamaanisha nini?
ii. Ilipigwa kipindi gani? Cha kampeni, baada ya kampeni au wakati mmiliki wa mjengo anajiunga au alipoachana na chama chetu?
iii. Mmiliki wa mjengo ni Mtanzania? ana maisha bora kama sisi wengine?
iv. Mpiga picha alidhamiria nini, Anatoa ujumbe gani kwa jamii?
v. Kitambaa/pazia la mlangoni liko sehemu sahihi hapo? Inaonyesha wamiliki wa hicho kitambaa wanafanana na jengo hilo au mmiliki ni kutoka kambi ya tofauti?

NAWASILISHA NATAKA HOJA TU, MATUSI HAPANA
 
ha ha ha hiyo kampuni ya kijani hauziki,ni sawa na blackbery
 
Hii inanikumbusha gazeti moja linalotoka kilasiku limeandika ASILIMIA KUBWA YA WATANZANIA WALIOCHAGUA HICHO CHAMA NA RAISI WAKE NI WASIOJUA KUSOMA NA KUANDIKA! Naomba mkalitafute hilo gazeti kama sikosei ni la jana au juzi!

(Sasa wanajuta sana)!
 
...Kweli CHADEMA imesheni ma - jobless , unapata wapi muda wa kuweka picha kama hizo mtandaoni?
 
Mwenye huo mjengo huyu hapa - bado ana matumaini ya maisha bora hadi kufikia 2015

umasikini.JPG
 
...Kweli CHADEMA imesheni ma - jobless , unapata wapi muda wa kuweka picha kama hizo mtandaoni?

kweli humu jamvini kuna viazi, una pata wapi MDA wa kuandika upuuz kama huo.
 
Kwa wanaoweza kunisaidia ku-interpreter hii picha

View attachment 117110
i. Picha inamaanisha nini?
ii. Ilipigwa kipindi gani? Cha kampeni, baada ya kampeni au wakati mmiliki wa mjengo anajiunga au alipoachana na chama chetu?
iii. Mmiliki wa mjengo ni Mtanzania? ana maisha bora kama sisi wengine?
iv. Mpiga picha alidhamiria nini, Anatoa ujumbe gani kwa jamii?
v. Kitambaa/pazia la mlangoni liko sehemu sahihi hapo? Inaonyesha wamiliki wa hicho kitambaa wanafanana na jengo hilo au mmiliki ni kutoka kambi ya tofauti?

NAWASILISHA NATAKA HOJA TU, MATUSI HAPANA

Mkuu,

Nitumie muda kidogo kujibu baadhi ya maswali yako, nikianza kukupongeza, you are real GT.

Picha hii yaweza kumaanisha yafuatato: 1) Umaskini wa kupindukia, huku aliyeweka kitambaa hicho hakiwa bado na matumaini ya maisha bora ktk miaka yake ya uzee (nahisi ni mzee wa miaka kama 60 hivi). 2) Upande mwingine wa tafsiri hapo kuna kiwanda cha ' sembe'. Kwa kufanya hivyo, aliyeweka kitambaa hicho ana %100 za uhakika kuwa si tiss wala polisi atakayefika hapo kwa ulevi wao wa ccm. Tafsiri inasadiwa na taarifa ya habari ya itv miezi kama miwili imepita, bangi iliyofunikwa na bendera ya ccm tayari kupelekwa sokoni.

3) Huyu mtu yamkini amafanya hivyo iliapate msaada haraka wa kiupendeleo zaidi ya wengine. Nieleze kidogo tafsiri hii, nyumba, vijiji, wilaya na mikoa ambayo imeonekana pinzani mwanzoni kabisa mwa vyama vingi, serikali iliwanyima misaada kama onyo la kwanini mlichagua upinzani. Hii hali sasa imepunguzwa na nguvu za umma. Hata hivyo, hiyo hali ilijengeka miongoni mwa wanachama wa chama tawara na kuendelea kudhani kuwa vipaumbele ni kwa wanachama wa ccm.

Kama picha hii ilipigwa wakati wa mafuriko jangwani na watu kupelekwa mabwepande basi mmoja wao alifikiri njia sahihi yakupata msaada wa haraka ni kujitambulisha kiivyo.


Picha hii itakuwa ilipigwa na mtu mwenye mapenzi mema na nchi yake. Aweza kuwa mwandishi au la. Na kama ni mwandishi, basi atakuwa miongoni mwa waandishi wazuri, mdadisi na critical thinker.Hata hivyo, picha hii inaweza kupigwa siku za campaign 2010 au hata baadae maana wengine walifikiri siasa za tnz ni za msimu kumbe hapana. Lengo la mpiga picha huyu si moja au mbili, kwa kutaja baadhi, niseme alichokusudia: 1) Maisha bora kwa kila mtanzania bado, 2) matumizi mabaya ya bendera na vitambaa vinavyogawiwa wakati wa uchaguzi, 3) mapenzi ya mtu na chama chake.....

Hata hivyo; tafsiri na matumuzi ya pazia hasa ktk kibanda kama hicho ni changamoto kwet sote, zaidi ccm na washirika wake.
 
Back
Top Bottom