BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,006
JK amteua mwenyekiti mpya TANESCO
na Hamisi Mwesi na Shehe Semtawa
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
RAIS Jakaya Kikwete amemteua Peter Ngumbullu kuwa mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
Taarifa hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini kuwa uteuzi huo unaanzia Oktoba 27, 2008 hadi Oktoba 26, 2011.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa Ngumbullu amewahi kulitumikia taifa katika nyadhifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwa mkurugenzi mtendaji katika Shirika la Fedha Duniani (IMF) akiwakilisha nchi 21 za Afrika.
Nyadhifa nyingine alizowahi kushika ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha; Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais; Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais; Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maendeleo ya Mifugo; Naibu Katibu Mkuu na Naibu Katibu wa Tume ya Mipango; Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha; Msaidizi wa Katibu Baraza la Mawaziri; na Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uchumi katika Sekretarieti ya Baraza ya Mawaziri.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa kitaaluma Ngumbullu ana shahada ya uzamili katika uchumi wa maendeleo ya Chuo Kikuu cha Williams, kilichoko nchini Marekani, Diploma katika uchumi ya Chuo Kikuu cha Colorado, nchini Marekani na shahada ya kwanza ya uchumi, uongozi na utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Aidha, taarifa hiyo ilieleza kutokana na uteuzi huo Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja aliwateua wajumbe wa bodi hiyo ambao ni Victor Mwambalaswa, Adollar Mapunda, Agnes Bukuku, Juma Bakari, Vintan Mbiro, Semindu Pawa, Beatus Segeja na Ngosi Mwihava.
na Hamisi Mwesi na Shehe Semtawa
Tanzania Daima~Sauti ya Watu
RAIS Jakaya Kikwete amemteua Peter Ngumbullu kuwa mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO).
Taarifa hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na msemaji wa Wizara ya Nishati na Madini kuwa uteuzi huo unaanzia Oktoba 27, 2008 hadi Oktoba 26, 2011.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa Ngumbullu amewahi kulitumikia taifa katika nyadhifa mbalimbali ikiwa ni pamoja na kuwa mkurugenzi mtendaji katika Shirika la Fedha Duniani (IMF) akiwakilisha nchi 21 za Afrika.
Nyadhifa nyingine alizowahi kushika ni Katibu Mkuu Wizara ya Fedha; Katibu Mkuu wa Ofisi ya Makamu wa Rais; Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu na Makamu wa Kwanza wa Rais; Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo na Maendeleo ya Mifugo; Naibu Katibu Mkuu na Naibu Katibu wa Tume ya Mipango; Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha; Msaidizi wa Katibu Baraza la Mawaziri; na Mkuu wa Kitengo cha Fedha na Uchumi katika Sekretarieti ya Baraza ya Mawaziri.
Taarifa hiyo ilieleza kuwa kitaaluma Ngumbullu ana shahada ya uzamili katika uchumi wa maendeleo ya Chuo Kikuu cha Williams, kilichoko nchini Marekani, Diploma katika uchumi ya Chuo Kikuu cha Colorado, nchini Marekani na shahada ya kwanza ya uchumi, uongozi na utawala ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.
Aidha, taarifa hiyo ilieleza kutokana na uteuzi huo Waziri wa Nishati na Madini William Ngeleja aliwateua wajumbe wa bodi hiyo ambao ni Victor Mwambalaswa, Adollar Mapunda, Agnes Bukuku, Juma Bakari, Vintan Mbiro, Semindu Pawa, Beatus Segeja na Ngosi Mwihava.