Peter Msigwa: Kumbe sio Kila John ni Yohana

Peter Msigwa: Kumbe sio Kila John ni Yohana

nimesoma pia kwenye biblia na kukutana na jina la kimombo peter ambaye kwa kiswahili ni petro. peter wa kwenye biblia alikuwa mwanafunzi imara wa Yesu na alikuwa tayari kufa kuitangaza injili, hakuwa na tamaa za kisiasa, hakuwa mpotoshaji, hakuwa mropokaji , alijawa na hekima tele, alihubiri injili mpaka mauti yake. tofauti ya peter wa kwenye biblia na huyu tuliyenaye ni kwamba peter huyu ni mchunguji aliyetoka kwenye uchungaji kwa tamaa za kisiasa, hayupo radhi kufia kwenye dini akitangaza injili, ni mpotoshaji na ni mropokaji, na kapungukiwa hekima ya kuamua na kutenda.

nimetafakari na kujua kuwa sio kila peter ni petro wengine ni petroli
huyo ni mchungaji dhaifu saaaana , badala kupanda juu , anashuka duniani , hao ndio wachungaji ubwabwa a.k.a, wasaka tonge.,
 
Kila siku tunasema uongozi si kukurupuka bali huwa ni karama toka kwa mola; ukijiona huna sifa za kuongoza ni vizuri tu ukatafuta kazi nyingine, maana kama ukingangania na ukapewa unaweza kuwa kama kina mfalme Sauli.
Kama ilivyo kwa mchungaji peter , yamemshinda ya mbinguni,kwenye nira nyepesi , ataweza ya duniani.?
 
Back
Top Bottom