Peter Msigwa apiga mil. 200 za Lowassa, Iringa Mjini mpo?

Peter Msigwa apiga mil. 200 za Lowassa, Iringa Mjini mpo?

Mleta uzi analalama hofu tele! haisaidii tulia si mafuriko tena ni zaidi ya sunami laja Iringa, hata ukipanda miti mirefu au kujificha litakufikia na utashuhudia utakubali kuwa Lowasa ndiye rais.
 
Kama LOWASSA anahonga hivi namhitaji kwa kuwa hana njaa.

Maelezo ya mleta mada yanatoka ktk mipango yao ya ccm maana huwa wanafanya ivyo.
 
Ulivyo kilaza wa hesabu labda kama ni billioni 200. Lakini millioni 200 haziwezi kutosha kwa mgawo wako huo.
 
mnavyo zidi msema vibaya, kumchafua kwa hoja nyepesi kama hii ndio nyota yake inavyo zidi ku ng'aa.
 
Mkuu kweli umefanya utafiti jamaa yangu anapikipiki sita amewaambia wawalipe elfu 15 lazima hela ya kifisadi itumike hivyo
 
haya wanabodaboda wakati wa kula ndo huu...
ukiona bodaboda kavaa kikadi shingoni ujue huyo analipwa kuwa pale.
wananchi msikubali kuhudhuria bure mikutanoni,sikuhizi unalipwa pesa......
 
Ambacho hakina ubishi ni kuwa kuandaa mkutano wowote lazima uwe na fedha si kwa Ukawa tu Bali hata CCM!

Zingine ulizoandika zote ni porojo tu na chuki zako dhidi ya EL!
 
Kalewa pombe na amefungiwa makufuli huyooo
 
Kwani mgombea wenu magamba kapata wapi pesa za kampeni?
 
kweli...yani nlipita Iringa juzi Msigwa kachokwa.
 
Duh, hivi hampewi semina ya jinsi ya kuandaa propaganda.....
Mara mil 200 ya kuandalia mkutano, tena ikabadirika hongo kwa Msigwa kwa kumtetetea kwa pole pole, ikaja 50 mil ya hongo kwa Msigwa halafu ikatumika kutengeneza ma bango......inaonekana hata maana ya Hongo huijui....hueleweki, kajipange
 
Chama kinachokufa kina wendawazimu wengi,na hapo ni kabla ya uchaguzi,tutefemee kuzika kwa mamia
 
Wewe kima acha kutuongelea wana iringa mjini au hujui ccm ni wapinzani hapo tulishawazika Rasmi wewe endelea kutoka povu
 
Picha picha
Maana uongo mumezidi tumewachoka jamani. Mumeiba kila kitu bado mnataka kutuaminisha kuwa ni wema nyinyi.
Sisi Wapumbavu tuliowachagua kwa miaka 53 inatisha tuacheni na ulofa wetu.
Sisi hatuangali kapokea shilling ngapi au katoa shilling ngapi bali tunataka kuandika history tu ya kukiondoa CCM
 
Ccm mnajitahidi kwa propoganda, bahati mbaya ni za kipuuzi

Sasa kama Mwenyekiti mzima anaweza kusema picha za mnato na video ni photoshop unadhani mfagizi wa ofisi za Lumumba kama TataMadiba atasemaje? Hawa ni full kuropoka ndio maana eti Makomeo anasema atawafanya Waalimu waishi maisha bora kama Mapadre. Sijui anamaana kuwa walimu wote watakuwa waseja na watakua wanaandaliwa breakfast ya soseji za kitimoto kila asubuhi au vipi? Kasahau kuwa katika walimu wapo wa dini tofauti.
Uongo ni jadi ya ccm
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom