Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,476
- 39,995
Na. M. M. Mwanakijiji
Moyo ulianza kunienda kwa kasi, viganja vilianza kulowa jasho, na koo lilinikauka nilipokuwa nikikata kona kuingia katika eneo la Hospitali ya Bombo, mjini Tanga. Moyo wangu ulikuwa umegubikwa na ubaridi utadhani alfajiri katika mji wa Makambako kule Iringa. Nilishikwa na huzuni, hofu, na nilihisi kuchanganyikiwa. Akili yangu ilikuwa ikinizunguka utadhani mkokoteni wa kisambaa. Nikifikiri mara milioni ni kitu gani ningekifanya tofauti kukwepa ukweli ambao ulikuwa unanikabili. Nilikuwa natembea kama akili zimeniruka nilipoingia katika geti za hospitali hiyo na hatimaye kwenye wodi ya kina mama. Nilikaribishwa hospitalini hapo na Nesi aliyevalia sare nyeupe na kikofia cheupe chenye mistari ya rangi ya hudhurungi.
Tafadhali nifuate Aliniambia Nesi Fatma Ally, ambaye alikuwa amevaa beji yenye jina lake. Walikuwa wananitarajia kwani Nesi Fatma aliniambia walikuta namba yangu ya simu na jina langu kwenye pochi ya mgonjwa.
Bila kufanya ajizi au kuuliza maswali nilimfuata kwa haraka huku miguu yangu nikiihisi kunitetema utadhani miti ya mianzi ipagwapo na upepo. Tuliingia katika Wodi namba tatu ambayo madirisha yake yaliangalia bahari ya ya Hindi. Vitanda vya wagonjwa vilipangwa kinadhifu na wodi nzima ilikuwa inangara kufuatia matengenezo ya hivi karibuni kutoka msaada wa serikali ya Ujerumani. Toka mbali niliweza kuona ngalawa na mitumbwi ikipita, wavuvi wakiendelea na uvuviw, na upeo wa mbali wa bahari hiyo niliweza kuona meli iliyotia nanga katika Gati ya Ras Kazone.
Sista Fatma (kama manesi wanavyoitwa) alinielekeza hadi kitanda namba 11 kilichokuwa kwenye kona. Nilisogea na moyo wangu nusura unitoke kwani mpenzi wangu wa moyoni, wa ubani wangu na aliyekuwa nuru ya maisha yangu alikuwa amelala chali akizungukwa na mipira na machine za kila aina zilizomsaidia kunusuru maisha yake.
SOMA ZAIDI HAPA (USIMWAMBIE MTU - NO UNDER 18)
Moyo ulianza kunienda kwa kasi, viganja vilianza kulowa jasho, na koo lilinikauka nilipokuwa nikikata kona kuingia katika eneo la Hospitali ya Bombo, mjini Tanga. Moyo wangu ulikuwa umegubikwa na ubaridi utadhani alfajiri katika mji wa Makambako kule Iringa. Nilishikwa na huzuni, hofu, na nilihisi kuchanganyikiwa. Akili yangu ilikuwa ikinizunguka utadhani mkokoteni wa kisambaa. Nikifikiri mara milioni ni kitu gani ningekifanya tofauti kukwepa ukweli ambao ulikuwa unanikabili. Nilikuwa natembea kama akili zimeniruka nilipoingia katika geti za hospitali hiyo na hatimaye kwenye wodi ya kina mama. Nilikaribishwa hospitalini hapo na Nesi aliyevalia sare nyeupe na kikofia cheupe chenye mistari ya rangi ya hudhurungi.
Tafadhali nifuate Aliniambia Nesi Fatma Ally, ambaye alikuwa amevaa beji yenye jina lake. Walikuwa wananitarajia kwani Nesi Fatma aliniambia walikuta namba yangu ya simu na jina langu kwenye pochi ya mgonjwa.
Bila kufanya ajizi au kuuliza maswali nilimfuata kwa haraka huku miguu yangu nikiihisi kunitetema utadhani miti ya mianzi ipagwapo na upepo. Tuliingia katika Wodi namba tatu ambayo madirisha yake yaliangalia bahari ya ya Hindi. Vitanda vya wagonjwa vilipangwa kinadhifu na wodi nzima ilikuwa inangara kufuatia matengenezo ya hivi karibuni kutoka msaada wa serikali ya Ujerumani. Toka mbali niliweza kuona ngalawa na mitumbwi ikipita, wavuvi wakiendelea na uvuviw, na upeo wa mbali wa bahari hiyo niliweza kuona meli iliyotia nanga katika Gati ya Ras Kazone.
Sista Fatma (kama manesi wanavyoitwa) alinielekeza hadi kitanda namba 11 kilichokuwa kwenye kona. Nilisogea na moyo wangu nusura unitoke kwani mpenzi wangu wa moyoni, wa ubani wangu na aliyekuwa nuru ya maisha yangu alikuwa amelala chali akizungukwa na mipira na machine za kila aina zilizomsaidia kunusuru maisha yake.
SOMA ZAIDI HAPA (USIMWAMBIE MTU - NO UNDER 18)