Madame S
JF-Expert Member
- Mar 4, 2015
- 17,177
- 34,444
PENZI LENYE MAUMIVU-01
Mtunzi:Juma Hiza
0712988278
Katika maisha yangu yote ya ndoa sikuwa ni miongoni kati ya wale wanaume waliyotulia. Licha ya kuwa mke wangu, Lillian alinionyesha mapenzi ya dhati, alinijali pamoja na kunithamini lakini hilo sikuonekana kujali, isipokuwa nilikuwa bize kuwatongoza wasichana ambao mwisho wa siku nilitembea nao.
Kwa kuwa nilikuwa nikifanya biashara nyingi hapa mjini ambazo zilikuwa zikiniingizia kiasi kikubwa cha pesa, hivyo sikuona ugumu wowote kumfuata msichana mrembo niliyemtamani na kumtongoza.
Katika maisha yangu ya ndoa na Lillian nilibahatika kuzaa naye mtoto mmoja wa kiume ambaye tulimpa jina la Brighton. Kama ilivyozoeleka katika maisha ya ndoa nyingi pindi mtoto anapozaliwa basi furaha na upendo huongezeka ndani ya nyumba lakini hali hiyo haikuwa kwangu. Sijui niseme nilirogwa maana siamini kile kilichotokea. Kwanza nakumbuka kipindi nilipofunga ndoa na Lillian na rasmi kuutangazia umma kuwa mwili mmoja kama vitabu vya dini vilivyoandikwa, nilikuwa nina wivu sana, wala sidhani kama kuna mwanaume ambaye alikuwa na wivu kama niliyokuwa nao kwa mke wangu.
Sikutaka awe na ukaribu wowote na kiumbe kiitwacho mwanaume, yaani neno lolote la utani aliloambiwa hata na ndugu yake wa damu ambaye alinitambulisha kama kaka yake au mjomba wake mimi kwangu lilinikwaza na kusababisha ugomvi mkubwa kati yetu.
Wivu wangu wa kimapenzi ndiyo uliyosababisha nikamkataza Lillian asifanye biashara yoyote ile, sio kwamba sikuwa nina uwezo la, kama nilivyotoka kukisimulia kuwa nilikuwa nikifanya biashara nyingi tena zilizokuwa zikiniingizia kiasi kikubwa cha pesa lakini hofu yangu kubwa ilikuwa ni kama ningekubali kumfungulia biashara mke wangu aifanye basi nilikuwa nikijitengenezea mazingira ya kuja kumwaga machozi ya kusalitiwa baadae.
Hapo kabla niliwahi kuwashuhudia baadhi ya marafiki zangu waliyowahi kuoa kabla yangu wakisalitiwa na kuumizwa vibaya mno na mapenzi. Hilo sikutaka litokee kwangu na ndiyo sababu kitu nilichokiamini ni sahihi kukifanya ni kumkataza Lillian asifanye biashara yoyote. Nilikuwa nipo radhi kumuhudumia kila kitu alichokuwa akikihitaji lakini sio kuona akitoka nje na kwenda kufanya biashara.
Baada ya Lillian kubeba ujauzito wangu ndipo hapo mambo yalipoanza kubadilika. Ghalfa! nilianza kumdharau, nilimuona kuwa mwanamke wa kawaida mno, hakunivutia kwa chochote wala kwa lolote lile, kipindi hicho cha ujauzito kilikuwa ni kipindi ambacho nilimuona kuwa kama mwanaume mwenzangu.
*****
Siku moja majira ya saa 12:30 jioni nilipokuwa nikitoka Milimani City nikirudi nyumbani kwangu Mbezi Beach Africana, nilikuwa ndani ya gari langu aina ya Toyota Mark X lenye rangi nyeusi, nilikuwa nikitembelea mwendo wa kawaida sana kiasi kwamba kwa wakati huo niliweza kuona kila kitu kwa upande wa nje, japokuwa nilikuwa nimefunga vioo vyote kwani gari lilikuwa na kiyoyozi.
Nilipofika kituo cha Mwenge ilibidi nisimamishe gari, sio kwamba nilipata tatizo la isipokuwa nilimuona msichana mrembo akiwa amesimama kituoni hapo.
Siku hiyo usafiri ulikuwa ni wa shida sana, abiria wengi walionekana kusubiria usafiri kwa muda mrefu huku wengine wakionekana kukata tamaa.
Nilishusha kioo cha upande wa kushoto kisha nikapiga honi, halafu nikanyoosha kidole kuashiria nilikuwa nikimuita huyo msichana. Kijana mmoja ambaye na yeye alikuwa amesimama eneo hilo akamgusa na kumpa ishara kuwa nilimuita.
Haikuchukua sekunde nyingi baada ya kuguswa na kijana huyo nikamuona akinifuata.
"Samahani kaka angu nimeambiwa unaniita, sijui una shida gani?" aliniuliza huku akionekana kuwa mwenye wasiwasi.
"Ndiyo nimekuita, nataka nikupe lift kama hutojali, sijui unaelekea wapi nikupeleke mrembo," nilimjibu kisha nikatoa tabasamu pana, akaonekana kuogopa zaidi.
"Hapana kaka angu usijali asante nashukuru sana," aliniambia huku akijing'atang'ata.
"Kwahiyo umeona ukiniambia unaelekea wapi nitanenepa au?"
"Hapana."
"Kwani unaishi wapi?"
"Hapo Tank bovu."
"Kumbe hapo tu panda nikusogeze usiogope."
"Hapana asante nashukuru."
"Sikia embu jaribu kuukunjua moyo wako halafu niamini just a few minutes okay! I'm good man so don't be afraid," nilimwambia.
Japokuwa nilitumia zaidi ya dakika tano kuzungumza naye lakini mwisho wa siku alikubali nimpe lift, hapa ni baada ya kuona muda unazidi kwenda na daladala zilikuwa ni za tabu siku hiyo.
Kitendo cha msichana huyo kukubali nimpe lift kilinifanya nijisikie mwenye furaha kubwa mno moyoni mwangu.
Alionekana kuwa msichana mrembo wa sura, umbo matata, kwa kifupi nilipomtazama kwa mara ya kwanza nikajikuta nikimtamani.
"Unaitwa nani?" nilimuuliza, wakati huo nilikuwa nimefika Makongo, nikapunguza mwendo kwa makusudi, lengo langu lilikuwa ni maongezi yazidi kuwa mengi.
"Naitwa Coletha," alijitambulisha.
"Oooh! Una jina zuri sana mrembo," nilimwambia huku nikitabasamu.
"Asante sana na wewe unaitwa nani?"
"Naitwa Kelvin."
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kufahamiana na Coletha, kwenye gari tulizungumza mambo mengi mpaka kufikia hatua nikafahamu alikuwa ni mtoto wa pili kuzaliwa kati ya watoto watatu katika familia yao (Mtoto wa kwanza ni Dada yake ambaye alinitambulisha kwa jina la Caren na wa mwisho ni mdogo wake wa kiume ambaye alikuwa akiitwa Samwel) lakini pia alikuwa ni mwanafunzi wa chuo kikuu.
Ndani ya muda mfupi niliyokutana na Coletha mpaka nikafikia hatua ya kumpa lift, sikutaka mawasiliano yetu yaishie Tank bovu kituoni, nilichoamua kukifanya ni kubadilishana naye namba za simu na huo ndiyo ulikuwa muendelezo wa kuwasiliana.
Kila siku nilihakikisha namtumia meseji Coletha, nampigia simu na hata kumjali kushinda mke wangu ambaye alikuwa ni mjamzito.
Mawasiliano yangu na Coletha mwisho wa siku yalizaa penzi. Katika kipindi hicho sikujali kuhusu mke wangu Lillian ambaye nilikuwa nikimsaliti. Nilijiona kuwa sahihi kwa kila kitu nilichokuwa nikikifanya katika maisha yangu.
*
Mtunzi:Juma Hiza
0712988278
Katika maisha yangu yote ya ndoa sikuwa ni miongoni kati ya wale wanaume waliyotulia. Licha ya kuwa mke wangu, Lillian alinionyesha mapenzi ya dhati, alinijali pamoja na kunithamini lakini hilo sikuonekana kujali, isipokuwa nilikuwa bize kuwatongoza wasichana ambao mwisho wa siku nilitembea nao.
Kwa kuwa nilikuwa nikifanya biashara nyingi hapa mjini ambazo zilikuwa zikiniingizia kiasi kikubwa cha pesa, hivyo sikuona ugumu wowote kumfuata msichana mrembo niliyemtamani na kumtongoza.
Katika maisha yangu ya ndoa na Lillian nilibahatika kuzaa naye mtoto mmoja wa kiume ambaye tulimpa jina la Brighton. Kama ilivyozoeleka katika maisha ya ndoa nyingi pindi mtoto anapozaliwa basi furaha na upendo huongezeka ndani ya nyumba lakini hali hiyo haikuwa kwangu. Sijui niseme nilirogwa maana siamini kile kilichotokea. Kwanza nakumbuka kipindi nilipofunga ndoa na Lillian na rasmi kuutangazia umma kuwa mwili mmoja kama vitabu vya dini vilivyoandikwa, nilikuwa nina wivu sana, wala sidhani kama kuna mwanaume ambaye alikuwa na wivu kama niliyokuwa nao kwa mke wangu.
Sikutaka awe na ukaribu wowote na kiumbe kiitwacho mwanaume, yaani neno lolote la utani aliloambiwa hata na ndugu yake wa damu ambaye alinitambulisha kama kaka yake au mjomba wake mimi kwangu lilinikwaza na kusababisha ugomvi mkubwa kati yetu.
Wivu wangu wa kimapenzi ndiyo uliyosababisha nikamkataza Lillian asifanye biashara yoyote ile, sio kwamba sikuwa nina uwezo la, kama nilivyotoka kukisimulia kuwa nilikuwa nikifanya biashara nyingi tena zilizokuwa zikiniingizia kiasi kikubwa cha pesa lakini hofu yangu kubwa ilikuwa ni kama ningekubali kumfungulia biashara mke wangu aifanye basi nilikuwa nikijitengenezea mazingira ya kuja kumwaga machozi ya kusalitiwa baadae.
Hapo kabla niliwahi kuwashuhudia baadhi ya marafiki zangu waliyowahi kuoa kabla yangu wakisalitiwa na kuumizwa vibaya mno na mapenzi. Hilo sikutaka litokee kwangu na ndiyo sababu kitu nilichokiamini ni sahihi kukifanya ni kumkataza Lillian asifanye biashara yoyote. Nilikuwa nipo radhi kumuhudumia kila kitu alichokuwa akikihitaji lakini sio kuona akitoka nje na kwenda kufanya biashara.
Baada ya Lillian kubeba ujauzito wangu ndipo hapo mambo yalipoanza kubadilika. Ghalfa! nilianza kumdharau, nilimuona kuwa mwanamke wa kawaida mno, hakunivutia kwa chochote wala kwa lolote lile, kipindi hicho cha ujauzito kilikuwa ni kipindi ambacho nilimuona kuwa kama mwanaume mwenzangu.
*****
Siku moja majira ya saa 12:30 jioni nilipokuwa nikitoka Milimani City nikirudi nyumbani kwangu Mbezi Beach Africana, nilikuwa ndani ya gari langu aina ya Toyota Mark X lenye rangi nyeusi, nilikuwa nikitembelea mwendo wa kawaida sana kiasi kwamba kwa wakati huo niliweza kuona kila kitu kwa upande wa nje, japokuwa nilikuwa nimefunga vioo vyote kwani gari lilikuwa na kiyoyozi.
Nilipofika kituo cha Mwenge ilibidi nisimamishe gari, sio kwamba nilipata tatizo la isipokuwa nilimuona msichana mrembo akiwa amesimama kituoni hapo.
Siku hiyo usafiri ulikuwa ni wa shida sana, abiria wengi walionekana kusubiria usafiri kwa muda mrefu huku wengine wakionekana kukata tamaa.
Nilishusha kioo cha upande wa kushoto kisha nikapiga honi, halafu nikanyoosha kidole kuashiria nilikuwa nikimuita huyo msichana. Kijana mmoja ambaye na yeye alikuwa amesimama eneo hilo akamgusa na kumpa ishara kuwa nilimuita.
Haikuchukua sekunde nyingi baada ya kuguswa na kijana huyo nikamuona akinifuata.
"Samahani kaka angu nimeambiwa unaniita, sijui una shida gani?" aliniuliza huku akionekana kuwa mwenye wasiwasi.
"Ndiyo nimekuita, nataka nikupe lift kama hutojali, sijui unaelekea wapi nikupeleke mrembo," nilimjibu kisha nikatoa tabasamu pana, akaonekana kuogopa zaidi.
"Hapana kaka angu usijali asante nashukuru sana," aliniambia huku akijing'atang'ata.
"Kwahiyo umeona ukiniambia unaelekea wapi nitanenepa au?"
"Hapana."
"Kwani unaishi wapi?"
"Hapo Tank bovu."
"Kumbe hapo tu panda nikusogeze usiogope."
"Hapana asante nashukuru."
"Sikia embu jaribu kuukunjua moyo wako halafu niamini just a few minutes okay! I'm good man so don't be afraid," nilimwambia.
Japokuwa nilitumia zaidi ya dakika tano kuzungumza naye lakini mwisho wa siku alikubali nimpe lift, hapa ni baada ya kuona muda unazidi kwenda na daladala zilikuwa ni za tabu siku hiyo.
Kitendo cha msichana huyo kukubali nimpe lift kilinifanya nijisikie mwenye furaha kubwa mno moyoni mwangu.
Alionekana kuwa msichana mrembo wa sura, umbo matata, kwa kifupi nilipomtazama kwa mara ya kwanza nikajikuta nikimtamani.
"Unaitwa nani?" nilimuuliza, wakati huo nilikuwa nimefika Makongo, nikapunguza mwendo kwa makusudi, lengo langu lilikuwa ni maongezi yazidi kuwa mengi.
"Naitwa Coletha," alijitambulisha.
"Oooh! Una jina zuri sana mrembo," nilimwambia huku nikitabasamu.
"Asante sana na wewe unaitwa nani?"
"Naitwa Kelvin."
Huo ndiyo ulikuwa mwanzo wa kufahamiana na Coletha, kwenye gari tulizungumza mambo mengi mpaka kufikia hatua nikafahamu alikuwa ni mtoto wa pili kuzaliwa kati ya watoto watatu katika familia yao (Mtoto wa kwanza ni Dada yake ambaye alinitambulisha kwa jina la Caren na wa mwisho ni mdogo wake wa kiume ambaye alikuwa akiitwa Samwel) lakini pia alikuwa ni mwanafunzi wa chuo kikuu.
Ndani ya muda mfupi niliyokutana na Coletha mpaka nikafikia hatua ya kumpa lift, sikutaka mawasiliano yetu yaishie Tank bovu kituoni, nilichoamua kukifanya ni kubadilishana naye namba za simu na huo ndiyo ulikuwa muendelezo wa kuwasiliana.
Kila siku nilihakikisha namtumia meseji Coletha, nampigia simu na hata kumjali kushinda mke wangu ambaye alikuwa ni mjamzito.
Mawasiliano yangu na Coletha mwisho wa siku yalizaa penzi. Katika kipindi hicho sikujali kuhusu mke wangu Lillian ambaye nilikuwa nikimsaliti. Nilijiona kuwa sahihi kwa kila kitu nilichokuwa nikikifanya katika maisha yangu.
*