Shunie
JF-Expert Member
- Aug 14, 2016
- 157,054
- 463,869
- Thread starter
- #61
SEHEMU YA 21...
Hakukuwa na kipindi ambacho Peter alikuwa kwenye presha kubwa kama kipindi hicho, kila siku alikuwa mtu wa kusikilizia kama barua aliyokuwa akiihitaji ilikuwa imeingia au la. Yeye ndiye aliyemwambia baba yake kwamba katika kipindi ambacho atakuwa hapo nyumbani, basi apewe ufunguo wa posta ili aweze kuwa nao.
Hilo halikuwa tatizo, kila siku ilikuwa ni lazima aende kuangalia kwenye sanduku la posta ili kuona kama ametumiwa barua na msichana huyo au hakuweza kuandika kwa kuwa alikuwa kipofu.
Baada ya wiki moja, alipokwenda kufungua sanduku la barua, macho yake yakatua katika bahasha moja ndogo, ilikuwa na karatasi huku kwa juu ya ile bahasha kukiwa na jina lake. Moyo ukamlipuka, hakuamini kama ile barua alikuwa ametumiwa yeye au aliona vibaya, akaichukua na kuanza kuiangalia vizuri, liliandikwa jina lake.
Hakutaka kuchelewa, nyumbani alipaona mbali, alichokifanya, hapohapo akaifungua barua ile, kitu cha kwanza kukutana nacho ilikuwa ni harufu nzuri ya manukato yaliyoichezesha pua yake na kumfanya kusahau kama alikuwa posta kulipokuwa na watu wengi.
“Mungu wangu! Mpaka kopa,” alisema Peter huku akiwa ameifungua bahasha ile na kukutana na mchoro wa kopa.
Nyumbani kulikuwa mbali, hakutaka kwenda kuisoma barua hiyo nyumbani kwao, alichokifanya ni kwenda pembeni na kisha kuifungua.
“Naweza nikanyeshewa na mvua au kugongwa na gari na barua nisiiisome, ngoja niisome hapahapa,” alisema Peter na kukaa chini, pembeni kidogo na sehemu iliyokuwa na masanduku yale ya posta.
Kwako Peter.
Nashukuru kwa barua yako iliyonisisimua, imenifanya kujiona nikiingia kwenye ulimwengu mpya ambao sikuwa nikiutarajia kwamba ningeingia. Siwezi kuandika mengi, ila kila kitu tumshirikishe Mungu kwani yeye ndiye wa kutufanya tuje kuoana.
Nakutakia maisha mema, nakupenda.
Tatiana Sangiwa.
Peter akashusha pumzi nzito, japokuwa mwandiko ulikuwa umepinda kidogo lakini aliyaelewa vizuri maneno yaliyokuwa yameandikwa. Pasipo kutarajia akajikuta akiibusu barua ile huku akiwa amekenua meno yake.
Hakukuwa na kipindi ambacho Peter alikuwa kwenye presha kubwa kama kipindi hicho, kila siku alikuwa mtu wa kusikilizia kama barua aliyokuwa akiihitaji ilikuwa imeingia au la. Yeye ndiye aliyemwambia baba yake kwamba katika kipindi ambacho atakuwa hapo nyumbani, basi apewe ufunguo wa posta ili aweze kuwa nao.
Hilo halikuwa tatizo, kila siku ilikuwa ni lazima aende kuangalia kwenye sanduku la posta ili kuona kama ametumiwa barua na msichana huyo au hakuweza kuandika kwa kuwa alikuwa kipofu.
Baada ya wiki moja, alipokwenda kufungua sanduku la barua, macho yake yakatua katika bahasha moja ndogo, ilikuwa na karatasi huku kwa juu ya ile bahasha kukiwa na jina lake. Moyo ukamlipuka, hakuamini kama ile barua alikuwa ametumiwa yeye au aliona vibaya, akaichukua na kuanza kuiangalia vizuri, liliandikwa jina lake.
Hakutaka kuchelewa, nyumbani alipaona mbali, alichokifanya, hapohapo akaifungua barua ile, kitu cha kwanza kukutana nacho ilikuwa ni harufu nzuri ya manukato yaliyoichezesha pua yake na kumfanya kusahau kama alikuwa posta kulipokuwa na watu wengi.
“Mungu wangu! Mpaka kopa,” alisema Peter huku akiwa ameifungua bahasha ile na kukutana na mchoro wa kopa.
Nyumbani kulikuwa mbali, hakutaka kwenda kuisoma barua hiyo nyumbani kwao, alichokifanya ni kwenda pembeni na kisha kuifungua.
“Naweza nikanyeshewa na mvua au kugongwa na gari na barua nisiiisome, ngoja niisome hapahapa,” alisema Peter na kukaa chini, pembeni kidogo na sehemu iliyokuwa na masanduku yale ya posta.
Kwako Peter.
Nashukuru kwa barua yako iliyonisisimua, imenifanya kujiona nikiingia kwenye ulimwengu mpya ambao sikuwa nikiutarajia kwamba ningeingia. Siwezi kuandika mengi, ila kila kitu tumshirikishe Mungu kwani yeye ndiye wa kutufanya tuje kuoana.
Nakutakia maisha mema, nakupenda.
Tatiana Sangiwa.
Peter akashusha pumzi nzito, japokuwa mwandiko ulikuwa umepinda kidogo lakini aliyaelewa vizuri maneno yaliyokuwa yameandikwa. Pasipo kutarajia akajikuta akiibusu barua ile huku akiwa amekenua meno yake.
