KIM KARDASH
JF-Expert Member
- Sep 21, 2011
- 5,139
- 1,149
masonic faith?eti siku izi ndo fasheni..
Tatizo lenu watu wa ABRAHAMIC religions ni kujipenda kupita kiasi na kujiona nyie ndio mko sahihi zaidi ya wengine katika kuabudu,hili ni tatizo kubwa.
masonic faith?eti siku izi ndo fasheni..
Kuna uhakika huu:
1.Inawezekana Pengo ana fanya biashara ya unga
2.Inawezekana Pengo hafanyi biashara ya dawa za kulevya
Kati ya majibu hayo moja wapo ni sahihi
Kwa hiyo unataka kusema kila taarifa sahihi lazima itolewe na taasisi inayolishughurikia. Na vilevile hakuna taarifa inaweza kuvuja kabla haijatolewa na taasis hiyo na taarifa hiyo ikamfikia mlengwa, mlengwa huyo akaitoa na hivyo taarifa hiyo ikawa ni sahihi? Issue nyingine unataka tuamini kila taarifa inayotolewa na taasisi za serikali ni sahihi na hakuna foul play?
Baada ya sakata la viongozi wa dini na tuhumu za madawa ya kulevya kusimama kwa muda sasa limerejea tena baada ya Mwadhama Polycarp Cardinal Pengo kueleza jana masikitiko yake ya kutaka kunyamazishwa kwa kuhusishwa na sakata hilo kama njia ya kumnyamaziaha.
KUJIKANGANYA KWA SERIKALI 1. Wakati wa baraza la Idd, Rais Kikwete alisema kauli yake ilieleweka vibaya, akasema taarifa alizopewa ni za mchungaji mmoja wa Kanisa la Biafra Kinondoni na Shehe mmoja, na hakumaanisha viongozi wote.
2. Waziri Mkuu Pinda wakati akijibu swali la Susan Lyimo (MB.) alisema Rais alieleweka vibaya kwani waliokamatwa, kwa kauli yake ni "wachungaji waswahili wa vikanisa vidogo" na wala si maaskofu kama ilivyochukuliwa na vyombo vya habari. Wakati propaganda hii ikizidi kushika kasi, mtu yeyote makini lazima azingatie yafuatayo.
Kwanza, kwa mfumo wa Kanisa Katoliki, haliitaji kusubili intelijensia ya wabongo iwaambie kiongozi fulani amekengeuka.Kanisa lina intelijensia yake ambayo hata CIA pamoja na nguvu zote wanalitambua hilo.Kiongozi yeyote hata awe Papa akikengeuka kwa issue nyeti kama hii anathibitiwa mara moja,Kwa wale wanaomjua Askofu Koda wa Same waulize leo hii yuko wapi'
Pili, kwa mfumo wa kanisa Pengo kama kiongozi hata nguo zake hajui bei yake. Matunzo yake yote yanafanya na kanisa hadi anakufa, yeye kama yeye haruhusiwi kumiliki hata hela bali alichonacho chote ni mali ya kanisa na hakuna anachokosa.
Tatu, kanisa aligawi vyeo kwa kujuana wala promotion, ni integrity yake, kwa hiyo hadi Pengo anachaguliwa kuongoza kanisa la Tanzania, integrity yake ni beyond any reasonable doubt. Hata akikengeuka upo mfumo wa kudeal naye hata before intelijensia ya bingo kubaini. Kwa ufupi, Kanisa Katoliki limekuwepo takriban miaka 2000 na litaendelea kuwepo kwa sababu ya misingi yake kiimani na mfumo wake wa kumdhibiti yeyote.
Ni mwendawazimu tu atakayedhani serikali hii ya awamu ya nne itapambana nalo kwa kuzusha tuhuma za kitoto ili kuwanyamazisha viongozi wake. Kwa ushauri tu, serikali zote (na vyama vyao) zilizojidai kupambana na kanisa zimefall apart (revise your history), fanyeni tu wanayowakemea for your political survival.
Hii ndio tabu ya kufikiri kwa kutumia masaburi meusiii!!!
Nadhani hapa hoja ni kua je ni kweli....na je hawezi kujua haki zake Kama kiongozi mkubwa Kama yeye anasingiziwa na je kwanini wasijitokeze nyie mnaokataa kumtetea kuprove kwa umma jamani haya mambo yapo na Chombo cha haki na mahakama kama amechafuliwa na ni clean why tryin to sympathize with the public..... It is an issue that needs to be addresed well na sio kutafuta huruma ya jamii.... It's typical legal matter.....MPOOO?
Ukipenda chongo huita kengeza:lol:
"kwa mfumo wa Kanisa Katoliki, haliitaji kusubili intelijensia ya wabongo iwaambie kiongozi fulani amekengeuka.Kanisa lina intelijensia yake ambayo hata CIA pamoja na nguvu zote wanalitambua hilo.Kiongozi yeyote hata awe Papa akikengeuka kwa issue nyeti kama hii anathibitiwa mara moja,Kwa wale wanaomjua Askofu Koda wa Same waulize leo hii yuko wapi'"
Mbona kwenye yale mauaji ya rwanda intelijensia ya kanisa katoliki haikuweza kuzibaini nyendo za yule kiongozi wakanisa hilo kujihusisha na mipango ya kuangamiza waumini wake (watutsi)mpaka mauaji yalipotokea?
MWASHAM BABA ASKOFU SI WEWE TU KUNA WATANZANIA WENYE FIKRA HURU KIBAO WAMEINGIZWA TAYARI KWENYE LISTI YA SIRI YA MIHADARATI NA ORIJINO KUENDELEA KUKUSANYA VUMBI MAGOGONI
Serikali ya Wauza Unga inapogeuzia santuri SAUTI HURU kwa tuhuma juu ya madhambi wayatendao wao wenyewe miaka nenda rudi!!
Idadi ya wauzaunga waliojipenyeza mjengoni Dodoma kwenda kutunga sheria inatisha! Lakini bahati tu ni kwamba tangu jumuiya ya kimataifa ifahamu picha zima, biashara yao imeyumba sana tena sana.
Na hilo ndilo siri mojawapo sehemu kubwa ya hao waliojiingiza kazi ya ubunge kwa maslahi ya kibiashara zaidi leo hii wakaamua kuliingizia taifa hasara kubwa kwa kudai kiwango cha posho ambacho hata kwa mataifa tajiri halipwi mtu.
Lengo ni kufidia kulikoyumba maana kujitoa ubunge kama Rostam Azizi kwa hivi sasa wanaona ni so.
Tangu Iran iingie hati hati ya kivita na Magharibi na Rostam Aziz kusogezewa tochi ya kimataifa kwa jirani zaidi na shingo lake, kuna uwezekano mkubwa sana kwamba vijana wetu wengi wakapona kwa kukosa madawa ya kulevya zaidi kwa kuwa usambazaji wake utaanguka zaidi na zaidi kote Afrika Mashariki, Kati na Kusini.
Mwasham Baba Askofu, jitulize roho yako. Ni wachache tu hdi hivi sasa ndio hawajui mchezo mzima na jinsi ambavyo serikali ya sasa inavyotumia tuhuma za mihadarati kama silaha ya kuwanyamazisha sauti huru.
Sera yao hivi sasa ni 'Kama vipi basi aheri Tukose wote'. Tutawaumbua wote wahusika halisi muda mwafaka utakapowadia na kuweka hadharani data lukuki hapa.
umeandika vizuri sana,watu inabidi tuamke sasa na tuelewe hakuna alie juu ya sheria!haki ya mtu hupatikani mahakamani kule ndio mbivu nambichi hujulikana na wala sio kwa kuongea na vijana ufukweni,haisaidii sana!
Hivi kuna ulingano wa kumbaini mtu aliyetoa mimba na aliyekunya? Tumia akili acha ushabiki bwana mdogo
Wewe umeandika vizuri zaidi. Nimefurahi kuona kuwa mpo baadhi yenu angalau mnajua mbivu na mbichi hupatikana mahakamani. Sasa kamwambie yule m kw ere aliyeacha kupeleka wahalifu mahakamani na badala yake kuanza kuhubiri majukwaani kuwa haki inapatkana mahakamani. Nakutuma ukamwambie kuwa, wahalifu hawaadhibiwi kwa kuandikwa list na kuihubiri hubiri in such a pathetic manner kwenye majukwaa, badala yake hufanyiwa uchunguzi kimya kimya na kukiwa na ushahidi, hupelekwa mahakamani.
Itakuwa waliamuwa kuliondoa...lol
Askofo pole.usifunge mdomo Mungu yu nawe endelea kupingania haki za waumini wako
Lile gari ni mali ya kanisa ndugu usipende kukurupuka ukadhani unaongea jambo la maana mbele za watu. Ni kama yale magari ya ikulu, ukiondoka unayaacha pale unless tuamue kukuzawadia. Hata chakula anachokula pale kinalipiwa na kanisa, njoo na lingine hilo la gari ni la jikoni.
Huna cha kuchangia hapa,kaa usome michango ya wachangiaji wengine ni njia bora ya kujifunza,wala sio dhambi ama kosa la jinai kutokua na mchango wowote!