shizukan
JF-Expert Member
- Jan 16, 2011
- 1,158
- 563
aliekwenda magazetini ni Pengo sio polisi
Hakwenda magazetini, alikuwa anaongea na vijana kwenye misa ya ufukweni.
Na umekimbilia kujibu kasentensi kamoja ili tu kuukimbia ukweli kuwa CCM ina lake katika hili. Mimi nilikupa na mfano wa Lowassa kukuonesha kuwa hakuna uhakika wa mambo yanayozungumzwa na CCM na vibaraka wake. Nikukumbushe jambo: Katika uchaguzi wa mwaka kama sio 1995 basi ni ule wa 2000, Kamanda Mahita alitoa tuhuma nzito dhidi ya CUF kuwa wameingiza nchini kontena la majambia ambayo yatagawiwa misikitini ili kufanyia vita. Unaweza kunipa muendelezo wa jambo hili?
Tusiwe wepesi wa kuwa fooled namna hii. Kama Askofu anatuhuma basi haikuwa sahihi kuzieneza, la muhimu lilikuwa kumuweka ndani kama wahalifu wengine. Huu ni uhuni tu ambao watu wenye akili zetu tumeshaubaini. Na wanaongea uhuni huu kwa kujua kiwango chetu cha kufikiri ni kidogo na ndio maana wengine wameanza hata kuona gari analotembelea Askofu kalinunua kwa pesa ya madawa, wakati lile ni mali ya kanisa. Tuwe wenye kufikiria ili tuweze kutoka hapa tulipo.
Waliothibitika kuwa wameiba kina Jairo wapo pale tunatend kuwasahau, huku akili zetu tunazielekeza kwenye uzushi. Walituambia Lowassa ni fisadi, mpk leo yupo uraiani kazi kubweka bweka kama mbwa koko, sitawaamini kwa maneno. Nitaamini nikiona Askofu kakamatwa na kufikishwa mahakamni kwa hilo. Tunaangamia kwa kukosa akili