The Khoisan
Platinum Member
- Jun 5, 2007
- 18,207
- 17,359
Wewe unafikiri kiongozi wa kanisa Katoliki Tanzania ni nani? Hapa hauko pekee yako. Watu wengi wanaamini Kadinali Pengo ndiyo mkuu wa Katoliki Tanzania. Je, nchi inapokuwa na nakadinali zaidi ya mmoja inakuwaje? kiongozi wa Kanisa Katoliki Tanzania ni Raisi wa TEC na mtendaji wake ni Katibu mkuu wake. Kadinali ni daraja la juu ktk madaraja ya utumishi ndani ya Katoliki, na kiongozi wa Katoliki ktk nchi aweza kuwa Askofu au Kadinali na Papa ni lazima awe Kadinali
Mkuu, Kadinali ndiye mkuu wa kanisa katoliki Tanzania. Maaskofu wanapewa kutokana na idadi ya waumini kwa jimbo. Kuna nchi kama Botswana au Namibia zina Askofu mmoja tu nchi nzima na hazina Kardinali, Kwa hiyo wako chini ya Kadinali wa South Africa. Kwenye nchi zenye zaidi ya kadinali mmoja then kila mmoja ana eneo lake la kuongoza. Kwa sasa Tanzania tunaye mmoja tu ndiyo maana akifa anateuliwa mwingine. Ukadinali hautolewi kama vyeo vya jeshini. Madaraka ya kanisa katoriki siyo ya kupokezana kama unavyofikiria. Hayo ya Rais wa TEC ni utaratibu tu waliojiwekea na siyo lazima unatumika kila mahali duniani.