Pengo: Nimesamehe

Pengo: Nimesamehe

Askofu mkuu wa jimbo kuu la Dar es salaam, Mwadhama Polcarp Kadinali Pengo amesema amemsamehe mchungaji Gwajima(hakuumtaja) na wote walioguswa ,ameyesema hayo wakati wa Misa Takatifu ya Jumapili ya matawi tarehe 29th March 2015 katika kanisa kuu la ST Joseph Cathedral .

"Naomba niseme kutokana na hali iliyopo kuwa kutoka moyoni kabisa nimesamehe yote yaliyosemwa na naomba tumuombee na kuwaombea wote walioguswa sina kinyongo chochote"

Waumini walilipuka kwa makofi baada ya kusikia kauli ya mwadhama.

Mytake:

Ushauri kwa Jamhuri, maadam Mwadhama ametamka tena huku akiwa amekalia kiti cha kiaskofu kwa sisi wakatoliki nadhani tunajua maana ya tamko linapotolewa huku Askofu akiwa amekalia kiti chake basi na wao wasikie mtukanwa kasemehe na wao watumie hekima kuachana na Gwajima ili kuipa uzito maana ya msamaha unless kama Jamhuri inataka kuendelea kwa mahojiano ya mambo mengine sio la kutukanwa,maana mtukanwa akitoa msahama huku mambo yanaendelea itaonekana hakuna msahama wa kweli kutoka kwa Mungu.

Chanzo mimi mwenyewe
.

Kama ni kweli amemsamehe, akamtembelee basi hospitali, akiiga mfano wa Pope John Paul II!

Papa John Paul II alimsamehe Mehmet Ali aliyetaka kumwua kwa risasi, na hata kumtembelea gerezani alikokuwa amefungwa!
 
Tunafundishwa kuwasamehe wakosaji. Japokuwa ni muhimu kuweka tafakari ya kutosha kabla ya kukurupuka kufyatua matusi hadharani. Siyo kwa wakubwa tu bali kwa yeyote yule, kwani Mungu anawapenda hata waovu
 
Halafu kumbe hata Cardinal Pengo ,Gwajima mwenyewe hamfahamu....(nimem quote kutoka kwenye kauli yake ya kumsamehe) so Gwajima ni opportunistic anataka kupanda chati kwa kumtukana Pengo
Katika hali ya kawaida maneno ya Gwajima kwangu ni uthibitisho tosha kabisa wa busara zake na tukio la kumkula mke wa mbasha
sikutegemea pengo awe muongo kiasi kile. anasema hamjui gwajima?hahaha. hapo ndipo utaujua unafiki wa pengo. ukitaka kumjua pengo, angalia hata maaskofu wenzie wa katoliki wamamchunia hawajamtetea baada ya matusi. kuna mgogoro mkubwa sana ndani ya katoliki hata maaskofu wenzie wamemchoka huyo jamaa.ila asifikiri pinda atakuwa waziri mkuu milele.
 
sikutegemea pengo awe muongo kiasi kile. anasema hamjui gwajima?hahaha. hapo ndipo utaujua unafiki wa pengo. ukitaka kumjua pengo, angalia hata maaskofu wenzie wa katoliki wamamchunia hawajamtetea baada ya matusi. kuna mgogoro mkubwa sana ndani ya katoliki hata maaskofu wenzie wamemchoka huyo jamaa.ila asifikiri pinda atakuwa waziri mkuu milele.
kumbe maaskofu na wao ni mashabiki wa kisiasa?There is a problem
 
well said maana lolote litalotokea kwa gwajima lazima jamii itamhusisha mwadhama

Hapo nitakuwa tofauti nawe,Gwajima ametenda kosa hasa kwa jamii nzima ya wakristu.Kama kiongozi wa dhehebu husika hakutakiwa kutoa matusi yale kwenye jumuia,alipaswa kwenda kumuona Askofu Pengo na kumwelezea juu ya maoni yake yanavyokinzana na wenzake na kwamba hakutenda kama anavyopaswa kiongozi kutenda

Gwajima ameudhalilisha UKRISTU sana tu hasa kwa kutoa matusi na mameno ya kudhalilisha kwa kiongozi mwenzake wa dini tena ameyafanya hayo mbele ya madhabahu.

HIvyo kwa haki kabisa anatakiwa ajilaumu mwenyewe.Na angeomba radhi hata kabla ya kufika alipofika.Tatizo amekosa BUSARA na UNYENYEKEVU kama kiongozi wa dini anavyopaswa kuwa
 
Wewe ndo hujui kitu kuhusiana na mfumo wa uongozi ndani ya Kanisa Katoliki. Mtu kuwa Kadinali haina maana ndiye kiongozi wa Kanisa Nchini mwake. Kuna Nchi hazi Kadinali na bado Kanisa Katoliki lipo katika Nchi hizo. Kwa sasa Afrika nzima kuna Makadinali wasiozidi 20 ilihali kuna Nchi zaidi ya 50 katika Afrika. Kadinali Pengo ni Kiongozi Mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Salaam pekee! Unaweza kuwa Kadinali hata kama wewe sio Askofu wala Padri! Soma Sheria za Kanisa Katoliki na taratibu zake. Usiwe Zero kiasi hicho!

Nyinyi ndiyo walewale akina Gwajima. Huwezi kuweka point yako bila kutukana .................... Hizo ibada zetu ni za matusi na kukashifu watu siyo!!??
 
kumbe maaskofu na wao ni mashabiki wa kisiasa?There is a problem
kwani pengo alipokuwa anaongea unafikiri alikuwa hatemi siasa pale? ni siasa ile aisee. pengo ni mwanasiasa mzuri tu, sema amekutana na wanasiasa wenzie halafu anajifanya yeye mpole kumbe nyuma ya pazia kuna mengi.
 
Gwajima kadinali pengo ni baba wa kiroho dunia nzima inatambua hivyo sio kama wewe ambaye hata huo uaskofu ulijipa mwenyewe. Angalia sasa umepigwa fimbo na mungu. Hata kama kad pengo alikosea kwa mtazamo wako hakustahili kutukanwa hadharani namna ile. Jifunze kuwa si kila mtu unaweza kumtukana na huo uaskofu wa kujipa. Mshukuru sana pengo ametoa msahama kwako vinginevyo ingekuwa kwaheri. Usimchezee mungu gwajima...ugua pole.

Kutukana si jambo zuri hasa kama ni kiongozi wa dini.Hata hivyo kiongozi wa dini lazima awe tayari kuusimamia ukweli bila unafiki na kukemea ubaya kwa nguvu zote.Na kama uovu /ubaya huo umetendwa na kiongozi mwenzake wa dini wajibu wa kukosoa na kukaripia ni halali kabisa maana katika Ukristo mwovu anakemewa bila kujali cheo chake.
aidha ninasikitishwa na mtizamo hasi ulionao juu ya viongozi wengine wa kiroho.Kwa mfano unaposema amejipa mwenyewe uaskofu huo ni uongo,chuki na inda.ni vema ukajua hata madhehebu mengine yana maaskofu.
 
Gwajima alisimama sambamba na maamuzi ya viongozi wa dini za Kikristo kama yalivyoainishwa kwenye waraka wa viongozi hao kwa makanisa. Pengo akiwa mmoja wa walioridhia. Hao viongozi wa dini wote ni mashetani kwa mujibuu wako?

Pengo aligeuzwa na kuropokeshwa maneno ya kuudhi na kuwasaliti viongozi wenzake ingawa hakuna alichokibadili kwa kuwa mwendo wa makanisa uko palepale. Habari zilizopo ni kwamba amejuta kwa kuwa hakujua Pinda si Mkristo tena na kwamba alimtumia kama pampas kuzuia ama kufuga harufu ya mahakama ya kadhi itikadi fake inayotumiwa na Salum Pinda kumpa uraisi akisaidiwa na kikwete. Kwa kuungama huku kwa pengo sasa amekuwa nani baada yakuwa shetani, halafu akawa mungu wako, na sasa tena karudikuwa shetani?

Kwa kuwa Gwajima na Pengo sasa wako upande wa shetani wako ambao ni umma wa Watanzania, wewe sasa unafurahia mauti ya Gwajima kwa ajili ya shetani pengo au una mashitaka mengine usiyoweza kuyasema ila unaegeshea kwa kesi ya mashetani hawa wawili ambao hawana ugomvi tena?

Uchungu ulionao wewe na Pinda, Kikwete, Kova, Membe dhidi ya Gwajima, viongozi wa dini zote za kikristo, wakristo wote, Pengo na umma wa watanzania wapenda haki, amani na maendeleo, unasababishwa na neno alilolisema Gwajima kumwonya Pengo ambaye tayari keshajitambua, au ni uchungu wa kazi inayofanywa na kundi ili kutetea maslahi ya Taifa na uhai wa Taifa la Tanzania?

Kwa hiyo wewe unaendesha mauji haya ya watu hawa kwa maslahi ya nani?

Naomba ufunguke ueleweke.



Gwajima ni shetani toka lini shetani akamshinda mungu.
 
Pengo hakumsame Gwajima kwamaana hakusema kama ame msamehe kwasababu hakumtaja jina la Gwajima ila alisema kuwa nimewasamehe wale wote wanao zusha maneno,
Sasa Gwajima hakuzusha maneno ila alitoa onyo au kalipio kwa Askofu mwenzake

Ivyo Pengo hajamsamehe Gwajima.
 
Nani kamsamehe na nani kwa lipi??????? huwezi kusamehe kama wewe hujatubu kosa lako.
 
Mimi nafikiri KOVA amechanganyikiwa sasa.

Hivi Gwajima atoroshwe hapo hospital kwa kosa gani hasa? Hilo la kutumia maneno ya kejeli na kashfa kwa Askofu Pengo? Mona ni kosa dogo sana ambalo linaweza kumaliza na makahama kwaa kulipa fidia tu

Nafikiri polisi walitakiwa waeleze umma hiyo bastola inamilikiwa isivyo halali au ameibiwa mtu? utaona akisha sema hilo anaishia hewani kama alivyoishia hewani yake ya Panya road. hatujajuzwa kama wale vijana 500 waliokamatwa walifikishwa mahakamani au la?

Mimi nafikiri angekuwa ameua au hata kuhujumu uchumi au madawa ya kulevya ndio ungekuwa mziki.

Nafikiri ni vizuri KOVA atulie kwani hilo ni suala la kisharia zaidi na sio propaganda za kisiasa.
 
Katika hali inayoonyesha Kiroho safi, askofu cardinal pengo amesema amemsamehe Mtu aliyemtukana bila kinyongo, hakumtaja kama ni askofu gwajima ila Mtu anayesemekana kumtukana kwa ujumbe unaozunguka mtandaoni ambaye ujumbe wake umewaudhi watu, si yeye. nimesali Catholic na pentecoste, na ninajua Kuna kitu kikubwa kilichopo makanisa ya pentecoste ambacho kingefaa sana ikiwa kingetumika vizuri, lakini bila upendeleo askofu pengo ata kama angekua na kosa ameonyesha mfano wa Kristo na kukomaa. Pongezi nyingi ziende kwake mimi asiyenijua, thank you so very much bishop.
Source:ipp media
 
Viongozi wa dini kuwa na kigeugeu haifai,Mmekaa pamoja na mmekubaliana halafu wewe unatoka kwenye kikao unasema vingine.
 
Hivi angetukanwa Sheikh Mkuu ingekuwaje? Police wangekwenda kumkamata? ..
 
Una point mkuu. Lakini hiyo sharia inafanya kazi hapo kwa Pengo tu? Mbona haikuwa na meno kwa wengine kama pale alipopigwa kofi Warioba na kutukanwa, na pale Lowasa anapotukanwa na kina Nape na yule Malecela motto na yule aliyezawadiwa ukuu wa wilaya ya Kinondoni? Au sharia inafanya kazi pale tu anayeguswa anapokuwa kipenzi cha waziri mkuu?


Pengo ni kiongozi wa kiroho na ni moja ya viongozi wakubwa sana hapa nchini. Haingii akilini umfananishe na mtoto aliyevaa pampasi halafu wakuache hivi hivi. Viongozi wa kisiasa mnaweza kutukana kama mnavyotukana lakini viongozi wa kiroho wanahitaji heshima hasa kwa mtu kama Pengo.
 
Back
Top Bottom