Pendekezo: SLAA amrithi SUMARI Arumeru!

ok, nilikuwa sijamuelewa, kumbe antichadema ni CDM? hahahahahahahahaha


Mzee kutokana na uvivu wako wa kusoma na kukimbilia kudandia treni kwa mbele nimelazimika kurudi page ya 2 ambako ndiko kwenye chanzo la hiko unachoking'ang'ania,sasa soma jamaa yako alichokisema na mimi nilichokisema,unadhani mimi ni mtu wa kukurupuka?
 
...wazo zuri lakini litajenga kutoaminika kwa dr. Kuna vijana wengi wanaoweza kuwakilisha maeneo yao vizuri na wanakubalika pia. Joshua asimamishwe kama mgombea.
Mkuu yule kijana Joshua nilimuona kwenye mchakato majimboni enzi zile za kampeni, kwakweli alionyesha ukomavu wa hali ya juu wa kisiasa na upeo mkubwa wa uelewa wa mambo,
Nilisikitika sana aliposhindwa uchaguzi, kunahitajika kuwaacha vijana waonyeshe uwezo wao
 

kwa hiyo unataka kunishawishi ama kunilazimisha na mimi ni mjinga nyie kuamini eti slaa ndio rais?siwezi aisee!slaa sio rais na nyie mnaelewa hivyo na yeye analijua hilo,ndio mana tunamshauri akagombee ubunge kwanza!
 
siungi nkono hoja.Nassari apewe haki yake.Slaa ana kazi kubwa ya kuimarisha chadema nchi nzima akijiandaa kukamata dola 2015

Hata mimi siungi mkono hoja ya Dr. Silaa kugombea ubunge kwa sasa na sio 2015 anaweza kuchukua hata mapema zaidi ya hapo ila suala kumteua Nasari ni suala la Kamati kuu siyo la sisi kwenye keybord ni la kamati kuu.
 
Nikuonyeshe nini wakati una macho lakini huoni. Unasoma lakini huelewi.

Hoja zimekuishia, hakuna jipya hapa ngoja nisepe, ukikumbuka ulichosahau unifahamishe nitakuja kujibu.
jibu wapi nilipoandika au kuonyesha nina nasaba na hicho chama chenu cha kususa na kuandamana?mbona unaikwepa hii,sema tu ulikurupuka usione haya!
 

basi mkuu yaishe, japo sijaona mahali popote aliposema ww CDM zaidi yakuhoji. (''Katika wakati huu tulionao sitegemei kuona mwanachama hai wa Chadema mwenye mawazo kama yako.
Labda utakuwa ni mshabiki tu ama ni gamba linalohadaa watu kwamba ni chadema'')
 
mkuu kweli una viroja.
kwani hamkuwahi kuwa na ndoa na cuf?waulize wazoefu huko cdm nyie si mmeingia cdm baada ya slaa kugombea urais...this may be too big for you guyz but ndoa tena rasmi ilikuwepo kati yenu na cuf!
 
Acha kumkashifu mkuu wa nchi aliyenyang'anywa ushindi.
 

I think ufahamu wako hauna spd gavana so inabidi ulidi mirembe ili ubongo wako ufanyiwe upem buzi yakinifu" . Keep it up mbunge we2 NASSARI nd BRAVO.
 

mfumo wa demokrasia ya vyama vingi bado unawachanganya!hamlifahamu lengo lake,madhani ni kama ushabiki tu wa simba na yanga,poleni sana,kwa style hii wataendelea kunufaika nao wanasiasa kwa ruzuku na kujiongezea posho tofauti na lengo lake halisi la kutukwamua sisi wananchi!ndio mana mnaona jamaa kwenye nyongeza ya posho na marupurupu mengine wanakuwa kitu kimoja!endeleeni kulala usingizi mkiamini wanawaonea huruma na kuwapenda kama mnavyowashabikia kwa mapenzi!

 
KIM!
nilikuwa miongoni mwa walinzi wa kura wa john mnyika pale ubungo, kura zilizohesabiwa na kutangazwa majimboni ni tofauti na kura zilizotajwa na tume ya uchaguzi? upo hapo?

kwa hiyo unataka kusema mnyika hakushinda ubungo kwa mujibu wa kura ulizohesabu wewe?
 
mkuu utaenda msibani Arumeru kumpumzisha kwenye nyumba yake ya milele mzee wetu?

La hasha,ila kilombero nilikuwako!una lingine au ni hilo hilo tu?lakini cdm wakimsimamisha slaa ntakwenda kwa nauli yangu na gharama zangu arumeru kushiriki kampeni za kumpeleka bungeni kwa kishindo akafanye kazi za watanzania cuz mr slaa is a very honest men na anaipenda sana nchi yake kuliko mfanyabishara mbowe ambae ni rafiki wa mwenyekiti wa ccm,unaona unafiki wa wanasiasa,huyu hashikani mkono na mwenyekiti wa ccm huyu anakunywa nae chai ikulu!mzee wangu slaa ana kazi sana lakini kwa kuwa ni muaminifu kwa taifa atashinda tu
 

sasa mkuu huoni akianza kuwatumikia wana arumeru sisi wa huku mabwepande tutakosa utumishi wake?
 

kuhusu suala la tarime kama wangekua wanachagua mtu basi yule bwana ambae hakupata tiketi ya cdm na kuamua kusimama kwa tikiti ya chama kingine angeshinda..lakini haikua hivyo,so inawezekana pia hata wewe huna informations za kutosha kuhusu why cdm walipoteza tarime,ipo sababu lakini huifahamu kwa kuwa huishi tarime.

Pia hoja ya kusema ni ngumu mtu kutoka jimbo lingine kwenda kushinda ugenini sikubaliani nayo sana,tanzania hatujafikia hivyo kaka,hayo mambo yapo kwa jirani zetu huko si tz.Nilitoa mfano wa mrema but inaonesha hukuupenda sana,lakini tunae sugu huyu wa mby mjini,hamna sehemu iliyoaminika korofi kwa mambo ya ubunge kwa mzawa kama mbeya,watu walimini pale lazima uwe 'mwa" ndio utapata ubunge,sugu kawaprove wrong sio!pia huko babati hali ilikua hivyo hivyo kwa mgeni kupewa ubunge,ndio maana nasema kwa slaa ambae ni heavy weight pale arumeru asimame kama kweli cdm wanataka lile jimbo,mwanasiasa uliekomaa lazima uchukue risk tangiapo!

Mambo ya elimu tuyaache,namstahi chairman ni mtu wangu,but elimu yake kwa kweli hapana..na sijui kwanini hataki kujiendeleza,wewe unajua sababu labda?nilisikitika sana na kutamani kuingia uvunguni alipokabiliana na Hamad Rashid kwenye mahojiano,ilikua aibu,nadhani watu wengi wa cdm hawapendi kuikumbuka siku ile,hali ingekua tofauti kama wangesimama slaa na hamad rashid,hata hamad rashid anajua hilo!
 

Bado hujaona sio!basi una tatizo la kusoma!
 
sasa mkuu huoni akianza kuwatumikia wana arumeru sisi wa huku mabwepande tutakosa utumishi wake?
alipokuwa akiwatumikia wana karatu uliukosa utumishi wake?ndio mana nikakwambie yule ni heavy weight kwanini sikusema mbowe ni heavy weight?
 
Dr W.Slaa,
Umejijengea heshima kubwa ndani ya nchi hii, umejijengea uaminifu mkubwa kwetu wananchi aidha tuwe ni wanachama wa Chadema au la, heshima uliyonayo sasa itunze na isikuponyoke.
Itakuwa ni busara saana iwapo utatulia na kufanya uchambuzi yakinifu ya namna gani atapatikana mgombea kwa jimbo hilo la Arumeru, heshima yako itazidi pale unapoonekana kuwasapoti wale mliowateua katika vinyang'anyiro tofauti. Wewe ni mtu mzima na mwenye busara, chonde sikia vijana wanachopendekeza kwa kuwapa nafasi zaidi. Daima, mapendekezo ya vijana ndio moyo wa amani na utulivu wa vijana, iwapo tu si yenye madhara.
Kuwa ni mwenye subra njema, subiri uchaguzi wa 2015 ujipange vema kwa dosari mlizozibaini kisha karata ichezwe vema na uwe jemedari mkuu wa taifa hili Inshallah. Fuatilia kwa umakini uchaguzi mkuu wa ndani wa chama tawala mwaka huu, kupitia hao watakaoshindwa...utapata mengi watakayotapika kutoka chamani.
Ni ushauri binafsi kwako dr. Slaa.
 
Kim, unatumia nguvu nyingi sana ktk hoja zako! hivi hujui kwamba tatizo la nchi hii ni system nzima ya uongozi? hivi wewe unaamini DR akirudi mjengoni ndio Tanzania itageuka kuwa paradise?. Binafsi sijaona fursa ambayo DR kaipoteza kwa kutokuwa mbunge kama ni nyaraka za serikali amezidaka anaweza kufanya kama alivyofanya wakati alipoitoa kwa umma ile LIST OF SHAME. Na je hakuna mbunge wa CDM unayemuamini kwamba akitumwa na DR kitu fulani akakiseme /kukifanya bungeni atakifanya? Na je DR hawezi akaitisha press conference na waandishi wa habari na akanena lake jambo? Na je unaimani/evidence kwa kiasi gani kwamba hitaji la wana Arumeru ni DR kuwa mbunge wao? Nina wasiwasi na uelewa wako kuhusu watu na demokrasia na muktadha wa siasa kwa ujumla.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…