Pendekezo kwa Rais Kikwete kuhusu wanafunzi waliofeli...

Pendekezo kwa Rais Kikwete kuhusu wanafunzi waliofeli...

Ninaelewa sympathy ya Mwanakijiji. Lakini kama mtoto kweli alipata sufuri ni pale mtoto hakufundishwa au hakujifunza au wasahihishaji wamesahihisha isivyo. Kama ni wasahihishaji wainue marks zao lakini kama ni vinginevyo kwamba walipata sufuri ya kweli hata ukiongeza marks bado ni sufuri, yaani chuo kikuu au kozi stahili ya ex-form IV hafundishiki, mwisho wa kozi ni sufuri kuongeza tatizo katika shughuli za maendeleo yetu. Ninachoshauri angalau ni kurudia form IV kwa gharama ya serikali kwa ajili ya kupewa cheti cha Division IV mwisho wa mwaka isipokuwa kwa wale watakaorudia kufanya mtihani watapewa stahili yao.

Makucha,

Swala la kujiuliza ni kwa nini wengine wafeli na wengine wafaulu? Hata darasani huwepo wa kwanza na wa mwisho hivo tunahitaji kujikita zaidi na tuwe wa kweli bila kumnyoshea kidole mtu kutafuta chanzo cha tatizo
 
serikali na Necta wanafanya biashara ya mitihani kwani orodha ya watu wengi waliofanya PC Tanzania nzima hawa wamefeli zaidi ya miaka yote , hivyo wanafelishwa makusudi ili serikali iendelee kupata fedha. Mfano Tegeta High School walifaul ni 74 daraja la mwisho div.4 kati ya 200 na kwa wakati huo huo Center nyingi zimetoka mswaki, hivyo nao wanategemea kurudia. Hiii kweli si biashara maana kuomba kufanya mtiani ni 100,000.00 unafikiri PC wako wangapi, siku hizi pc wako wengi kuliko wanafunzi wa kawaida, hivyo serikali inapata mabillioni kupitia balaza la mitihani.
 
nakumbuka meku mmoja aliyepata zero form four akarudia form one once again na alipomaliza form akapata one na kuendelea form five. tatizo wabongo hako tayari kujikana nafsi zao hawataki kukubali ukweli . ni heri mtu apoteze miaka minne kuliko kupoteza maisha yake yote. huo ndo ukweli ambao wengi hawapendi kusikia kabisa wanataka short cuts including ktk sekta michezo. watu wanaambiwa body structure, size , physical health and strengths, psycological treatment, individual , excercises and training for team work are keys for success in soccer game. tunarudirudia ujinga uleule as aresult team yetu ya taifa imeshindwa kuingia kwenye fainali za AFCON 32 YEARS NOW! THIS IS the CRUX of the problem in tanzania. politicians with poor academic background ndio waliotufikisha hapa, to equalise opportunity in watu wawe na mentality kuwa wamefika secondary ingawa hawakustahili na wala hawakufanya juhudi yoyte kurekebisha hali yao ya udhaifu ktk masomo. there is too much assumptions and too much interference with the natural course of how things should happen.
 
kwakweli kwahili la sasa si watoto wenye matatizo bali naona serikali imekua na mchango mkubwa sana kwenye hili hasa pale wanapowatret walimu kama mbwa ambao hawana haki ya kusikilizwa mfano ni mara ngapi walimu wameomba hata kuongezewa hata 40 elfu kwenye mshara na kudharauliwa wakati huo mkuu mwenyewe anapendekeza kuongeza malipo ya wabunge ambao wanapata milions of money?yaan hata ingelikua mimi lazima cwez kuwa na moyo wa kujitolea kabisa!:bange:
 
Mimi nadhani tatizo ni kubwa kuliko linavofikiriwa. Kwa kiasi kikubwa(mawazo yangu) mmomonyoko wa maadili katika jamii una mchango mkubwa sana katika hili, wanaofeli sio sekondari tu bali hatu vyuoni na huko kuna baraza la mitihani?

Kuna mchangiaji mmoja ameshauri wazazi wawajibike kuwaondelea starehe watoto wao ikiwemo pamoja na maTV simu watoto wanalala usiku mwingi si kwa ajili ya kusoma bali kufanya mambo ya hovyo hovyo,hata mwanasiasa mmoja karibuni aliyekuwa anamtukana mwanasiasa mwingine ambaye aweza kuwa mzazi wake ni zao la mmomonyoko wa maadili, turudishe maadili hili la kufaulu litawezekana.

Haki Elimu nao watusaidie katika hili walikuja wakapiga kelele walimu wanawatenda wanafunzi sasa imefika hatua walimu hawana mamlaka juu ya wanafunzi tena hivi karibuni huko Pwani walimu wa kike walikimbia shule baada ya kutishiwa kubakwa na wanafunzi wao sasa hapo unategemea kuna kufundishana kweli? au kutakuwa na mwalimu mwenye nia ya dhati ya kumsaidia mwanafunzi ambaye tayari anajiona ni mkubwa mwenzie?

Mkuu haswa hii yote inatokana na athali za utandawazi na baadhi ya wazazi/walezi kulichukulia suala la elimu kama ni fasheni tu katika rika fulani.

Kikubwa ni Wazazi/Walezi kubadilika na kuwaambia ukweli vijana wao kwamba elimu ni kazi iliyo kubwa sana na mshahara wake unapatikana tu pale unapoondokana na umaskini wa kifikra na utegemezi wa kulishwa,kuvishwa,kunyweshwa,kudekezwa na kubembelezwax2.

Upande wa Serikali nao una wajibu mkubwa wa kuhakikisha walimu wanapewa stahiki zao,sambamba na hilo walimu nao wadhibitiwe kutoroka vipindi vyao madarasani na kwenda ama kwenye ulevi au kufundisha shule nyingine za binafsi.
 
Nilitaka kuandika
makala ndefu lakini nimeona niende moja kwa moja na kusema
ombi/pendekezo langu kama litampendeza Rais Kikwete.

KWA KUWA, matokeo ya kidato cha nne ambayo yametoka hivi karibuni
yameonesha kufeli kwa kutisha kwa watoto wetu katika mtihani wao;

KWA KUWA
, kufeli huko kuna matokeo ya moja kwa moja katika maisha ya
wanafunzi hawa, familia zao na kwa taifa kwa u jumla;

KWA KUWA
, matokeo hayo ni hasara kubwa kwa wazazi waliowekeza kwa
miaka minne ya elimu ya watoto hawa na kwa taifa katika kuwekeza vifaa,
walimu na miundo mbalimbali;

KWA KUWA, kuacha kundi kubwa la watoto hawa kurudi katika maisha
ya uraiani kutaongeza jamii ya watu ambao hawana elimu ya kutosha na
wasioweza kuajiriwa hata katika mifumo isiyo rasmi (pamoja na kushindwa
kujiajiri wenyewe);

KWA KUWA, kufeli kwa watoto hawa ninaamini siyo kosa lao peke yao
bali pia ni kosa la utawala na uongozi wetu, wazazi na jamii kwa
ujumla;

NINAAMINI KUWA, kutokuchukua uamuzi wa makusudi na wa lazima
kuwasaidia watoto hawa kuwapa nafasi nyingine ni kuwahukumu katika
maisha duni na kuwanyima kimsingi nafasi ya kuinuka wakati tayari
wameshaanguka

NINAAMINI KUWA, matokeo haya ni dhambi na aibu ya taifa letu hasa
katika nchi ambayo inajivunia kuwa ina 'shule nyingi, vyuo vingi,
walimu wengi, na teknolojia ya kisasa katika elimu;

NINAAMINI KUWA, Ni jukumu la uongozi wa kisiasa wa taifa kuchukua
hatua za haraka na za lazima kuwapa nafasi nyingine watoto hawa kuweza
kutengeneza waliposhindwa.

NINAAMINI KUWA, Taifa lina deni kwa watoto hawa, lina deni kwa
historia, lina deni kwa familia zao na kwa hakika kabisa lina deni kwa
maisha ya watoto hawa. Deni hili tusiliache likue lije kushindwa
kulipika. Naamini tunaweza kulilipa kabla halijaanza kuwa na riba
isiyokamatika!

Kutokana na mambo yote hayo juu na mengine ambayo nimeyaadhania,
ninaamini Utawala wa Rais Kikwete unaitwa na historia, unadaiwa na haki,
na unalazimishwa na wajibu kuwapa watoto hawa nafasi nyingine ya
kurudia mitihani ya kidato cha nne ili kuweza kuinua alama zao za
kufaulu, kusahihisha makosa yao na kuwapa nafasi ya kuweza kuendelea na
elimu ya kidato cha tano na cha sita. Kutokana na hili:

HIVYO BASI, Baraza la Mawaziri lifanye kikao cha dharura
kuhusiana na matokeo haya ya mitihani ambapo uamuzi wa kutengua matokeo
yote ya mtihani uchukuliwe na kuyafuta kabisa matokeo hayo;

NA HIVYO BASI
, Baada ya kufuta matokeo hayo serikali iamue kuwa
watoto wote waliofanya mtihani huu uliopita watarudia mitihani yote ya
kidato cha nne ndani ya mwaka mmoja pamoja na watoto watakaokaa katika
mtihani wa mwaka huu au katika mtihani mwingine tofauti

NA HIVYO BASI
, Watoto wote ambao katika mtihani huu wamepata daraja
la I na II watakuwa na uhuru wa ama kurudia mtihani wao ili kuthibitisha
kufaulu kwao au kuendelea na matokeo waliyonayo. Wakiamua kurudia basi
kama watafaulu alama za juu zaidi ya sasa watashika alama hizo kama
watapata alama za chini watashika alama zao za sasa;

NA HIVYO BASI
, Wanafunzi waliopata daraja III na 0 nao itakuwa hivyo
hivyo, watapewa nafasi moja ya kurudia mitihani yote kuiinua viwango
vyao na wale watakaopata viwango vya juu kuliko vya sasa basi watasika
viwango hivyo na wale ambao watapata viwango vya chini kuliko sasa
watashika viwango vya sasa.

NA HIVYO BASI, Wanafunzi ambao sasa wamepata daraja la III na 0
endapo watarudia mitihani ijayo na wakainua viwango vyao na kuwa kati ya
daraja la I na II basi SERIKALI itawapa nafasi ya kusoma bore kidato
cha tano na cha sita katika shule za Sekondari za Serikali. Hii iwe
'AHADI YA TAIFA' (National Promise)

NA HIVYO BASI, ili kutoa motisha kwa shule na walimu ambao
wanawafundisha wanafunzi hawa na wengine basi serikali ianze kutoa
motisha kwa shule zote (zenye watahiniwa wengi) ambazo zitafaulisha
watoto wengi kwenye madaraja ya I na II. Motisha huu utakuwa kwa shule
na kwa jopo la walimu wa kidato cha nne.

- Shule ambayo haitatoa daraja 0 kuanzia sasa itapata zawadi ya shilingi
milioni 50 kwa matumizi ya sule
- Shule ambayo haitatoa daraja IV kuanzia sasa itapata zawadi ya silingi
milioni 75 kwa matumizi yake
- Walimu wanaofundisha shule hizo zikiwa na matokeo hayo watagawana
zawadi ya nusu ya tuzo hizo (Milioni 25 kama hakuna 0, milioni 37.5 kama
hakuna daraja la IV)

Tuzo hizo zinaweza kurudiwa kila mwaka endapo viwango hivyo vitaendelea.


NA HIVYO BASI, Mwalimu Mkuu wa shule ambazo zinafanya vibaya
zaidi watafukuzwa kazi, Afisa Elimu wa Wilaya yenye shule nyingi
zilizofanya vibaya nao watafukuzwa kazi.

NA HIVYO BASI, kuanzia sasa wanafunzi wote wanaopata daraja la IV
na 0 watakuwa wanapata automatic resit ya mtihani katika mwaka
unaofuatia. Na katika hili napendekeza wanafunzi wote waliopata madaraja
hayo katika miaka
big up sana mkubwa!
 
Makucha,

Swala la kujiuliza ni kwa nini wengine wafeli na wengine wafaulu? Hata
darasani huwepo wa kwanza na wa mwisho hivo tunahitaji kujikita zaidi na
tuwe wa kweli bila kumnyoshea kidole mtu kutafuta chanzo cha
tatizo

kwa ushauri bora wangerudia tu mtihani.
 
serikali na Necta
wanafanya biashara ya mitihani kwani orodha ya watu wengi waliofanya PC
Tanzania nzima hawa wamefeli zaidi ya miaka yote , hivyo wanafelishwa
makusudi ili serikali iendelee kupata fedha. Mfano Tegeta High School
walifaul ni 74 daraja la mwisho div.4 kati ya 200 na kwa wakati huo huo
Center nyingi zimetoka mswaki, hivyo nao wanategemea kurudia. Hiii kweli
si biashara maana kuomba kufanya mtiani ni 100,000.00 unafikiri PC wako
wangapi, siku hizi pc wako wengi kuliko wanafunzi wa kawaida, hivyo
serikali inapata mabillioni kupitia balaza la mitihani.

mara nyingi hawa pc huonewa katika usahishaji wa mitihani yao!
 
Nilitaka kuandika
makala ndefu lakini nimeona niende moja kwa moja na kusema
ombi/pendekezo langu kama litampendeza Rais Kikwete.

KWA KUWA, matokeo ya kidato cha nne ambayo yametoka hivi karibuni
yameonesha kufeli kwa kutisha kwa watoto wetu katika mtihani wao;

KWA KUWA
, kufeli huko kuna matokeo ya moja kwa moja katika maisha ya
wanafunzi hawa, familia zao na kwa taifa kwa u jumla;

KWA KUWA
, matokeo hayo ni hasara kubwa kwa wazazi waliowekeza kwa
miaka minne ya elimu ya watoto hawa na kwa taifa katika kuwekeza vifaa,
walimu na miundo mbalimbali;

KWA KUWA, kuacha kundi kubwa la watoto hawa kurudi katika maisha
ya uraiani kutaongeza jamii ya watu ambao hawana elimu ya kutosha na
wasioweza kuajiriwa hata katika mifumo isiyo rasmi (pamoja na kushindwa
kujiajiri wenyewe);

KWA KUWA, kufeli kwa watoto hawa ninaamini siyo kosa lao peke yao
bali pia ni kosa la utawala na uongozi wetu, wazazi na jamii kwa
ujumla;

NINAAMINI KUWA, kutokuchukua uamuzi wa makusudi na wa lazima
kuwasaidia watoto hawa kuwapa nafasi nyingine ni kuwahukumu katika
maisha duni na kuwanyima kimsingi nafasi ya kuinuka wakati tayari
wameshaanguka

NINAAMINI KUWA, matokeo haya ni dhambi na aibu ya taifa letu hasa
katika nchi ambayo inajivunia kuwa ina 'shule nyingi, vyuo vingi,
walimu wengi, na teknolojia ya kisasa katika elimu;

NINAAMINI KUWA, Ni jukumu la uongozi wa kisiasa wa taifa kuchukua
hatua za haraka na za lazima kuwapa nafasi nyingine watoto hawa kuweza
kutengeneza waliposhindwa.

NINAAMINI KUWA, Taifa lina deni kwa watoto hawa, lina deni kwa
historia, lina deni kwa familia zao na kwa hakika kabisa lina deni kwa
maisha ya watoto hawa. Deni hili tusiliache likue lije kushindwa
kulipika. Naamini tunaweza kulilipa kabla halijaanza kuwa na riba
isiyokamatika!

Kutokana na mambo yote hayo juu na mengine ambayo nimeyaadhania,
ninaamini Utawala wa Rais Kikwete unaitwa na historia, unadaiwa na haki,
na unalazimishwa na wajibu kuwapa watoto hawa nafasi nyingine ya
kurudia mitihani ya kidato cha nne ili kuweza kuinua alama zao za
kufaulu, kusahihisha makosa yao na kuwapa nafasi ya kuweza kuendelea na
elimu ya kidato cha tano na cha sita. Kutokana na hili:

HIVYO BASI, Baraza la Mawaziri lifanye kikao cha dharura
kuhusiana na matokeo haya ya mitihani ambapo uamuzi wa kutengua matokeo
yote ya mtihani uchukuliwe na kuyafuta kabisa matokeo hayo;

NA HIVYO BASI
, Baada ya kufuta matokeo hayo serikali iamue kuwa
watoto wote waliofanya mtihani huu uliopita watarudia mitihani yote ya
kidato cha nne ndani ya mwaka mmoja pamoja na watoto watakaokaa katika
mtihani wa mwaka huu au katika mtihani mwingine tofauti

NA HIVYO BASI
, Watoto wote ambao katika mtihani huu wamepata daraja
la I na II watakuwa na uhuru wa ama kurudia mtihani wao ili kuthibitisha
kufaulu kwao au kuendelea na matokeo waliyonayo. Wakiamua kurudia basi
kama watafaulu alama za juu zaidi ya sasa watashika alama hizo kama
watapata alama za chini watashika alama zao za sasa;

NA HIVYO BASI
, Wanafunzi waliopata daraja III na 0 nao itakuwa hivyo
hivyo, watapewa nafasi moja ya kurudia mitihani yote kuiinua viwango
vyao na wale watakaopata viwango vya juu kuliko vya sasa basi watasika
viwango hivyo na wale ambao watapata viwango vya chini kuliko sasa
watashika viwango vya sasa.

NA HIVYO BASI, Wanafunzi ambao sasa wamepata daraja la III na 0
endapo watarudia mitihani ijayo na wakainua viwango vyao na kuwa kati ya
daraja la I na II basi SERIKALI itawapa nafasi ya kusoma bore kidato
cha tano na cha sita katika shule za Sekondari za Serikali. Hii iwe
'AHADI YA TAIFA' (National Promise)

NA HIVYO BASI, ili kutoa motisha kwa shule na walimu ambao
wanawafundisha wanafunzi hawa na wengine basi serikali ianze kutoa
motisha kwa shule zote (zenye watahiniwa wengi) ambazo zitafaulisha
watoto wengi kwenye madaraja ya I na II. Motisha huu utakuwa kwa shule
na kwa jopo la walimu wa kidato cha nne.

- Shule ambayo haitatoa daraja 0 kuanzia sasa itapata zawadi ya shilingi
milioni 50 kwa matumizi ya sule
- Shule ambayo haitatoa daraja IV kuanzia sasa itapata zawadi ya silingi
milioni 75 kwa matumizi yake
- Walimu wanaofundisha shule hizo zikiwa na matokeo hayo watagawana
zawadi ya nusu ya tuzo hizo (Milioni 25 kama hakuna 0, milioni 37.5 kama
hakuna daraja la IV)

Tuzo hizo zinaweza kurudiwa kila mwaka endapo viwango hivyo vitaendelea.


NA HIVYO BASI, Mwalimu Mkuu wa shule ambazo zinafanya vibaya
zaidi watafukuzwa kazi, Afisa Elimu wa Wilaya yenye shule nyingi
zilizofanya vibaya nao watafukuz
hilo wazo ningependa limfikie kikwete ni zuri kwa kweli
 
Si kweli hawaonewi ila wao hawajiandai vizuri.

hapana,!nasema hivyo kwa sababu,kwa nini NECTA wameweka passmark za juu kuliko hawa s.c? maana passmark ya pc ni 50% na sc ni 41% na ukiangalia matokeo ya pc ni aibu,kwa hiyo unataka kusema wote hawakujiandaa effectively?
 
serikali na Necta
wanafanya biashara ya mitihani kwani orodha ya watu wengi waliofanya PC
Tanzania nzima hawa wamefeli zaidi ya miaka yote , hivyo wanafelishwa
makusudi ili serikali iendelee kupata fedha. Mfano Tegeta High School
walifaul ni 74 daraja la mwisho div.4 kati ya 200 na kwa wakati huo huo
Center nyingi zimetoka mswaki, hivyo nao wanategemea kurudia. Hiii kweli
si biashara maana kuomba kufanya mtiani ni 100,000.00 unafikiri PC wako
wangapi, siku hizi pc wako wengi kuliko wanafunzi wa kawaida, hivyo
serikali inapata mabillioni kupitia balaza la mitihani.

Big up sana mkubwa! yaani ukiangalia matokeo ya PC ni aibu na inasikitisha,NECTA wamelaaniwa! haiwezekani pc wote kufeli kiasi hicho! ngoja tuone wanao resit tena,halafu hili liwaziri la elimu linalopoka"NITAJIUZULU KWA MATOKEO HAYA KUWA MABAYA"
 
Back
Top Bottom