Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 34,240
- 44,485
- Thread starter
- #21
Ni kweli inawezekana hukuchangia ila uliwasoma wachangiaji wengi walivyokuja na majibu ya kashfa; kisa nini Waislamu walilalamika dhidi ya utendaji wa Wizara na Baraza; suala kubwa lilikuwa ni hili la kufeli wangi walichukulia kama dhihaka; kuna watu nawasubiri nisikia majibu yao ila nina uhakika wanakumbuka walichosema hawatatia mguu humu!
Chama
Gongo la mboto DSM
Chama, tatizo la watoto wetu kufeli siyo suala la Waislamu tu. Mwaka jana katika mjadala kama huu ambapo baadhi ya watu walionesha jinsi shule za Waislamu zilivyokuwa zimefeli mimi nilionesha jinsi ya shule zenye majina ya Kikristu nazo zilifelisha. Watu wengine wanapoona majina ya seminari za Kikatoli zinapofanya vizuri wanaweza kufikiria kuwa shule zote za Kikristu watoto wake wanafaulu kwa sababu ni za Kikristu na za Waislamu wanafeli kwa sababu watoto ni WAislamu. Matokeo ya mwaka huu kwa mfano shule ya TAQWA ya Mwanza ina watoto wamefanya vizuri kuliko shule nyingi za "St. Nanino".
Hata hivyo tukiangalia kwa kutazama 'dini' tunaweza tukakosa kabisa. Ni lazima tuangalie kuwa hawa watoto wa Kiislamu ni watoto wa Kitanzania. Kufeli kwao ni hasara kwa Taifa siyo kwa Uislamu! Wanapofeli watoto wa Kikristu Muislamu hapaswi kufurahia (kwamba we are even) bali kusikitika pia kwa sababu wanaofeli ni watoto wa Kitanzania. Hatuwezi kulitatua tatizo la elimu while holding parochial sentiments...
Ni tatizo letu, na linatuhusu sote equally.