Pendekezo kwa Rais Kikwete kuhusu wanafunzi waliofeli...

Pendekezo kwa Rais Kikwete kuhusu wanafunzi waliofeli...

Ni kweli inawezekana hukuchangia ila uliwasoma wachangiaji wengi walivyokuja na majibu ya kashfa; kisa nini Waislamu walilalamika dhidi ya utendaji wa Wizara na Baraza; suala kubwa lilikuwa ni hili la kufeli wangi walichukulia kama dhihaka; kuna watu nawasubiri nisikia majibu yao ila nina uhakika wanakumbuka walichosema hawatatia mguu humu!

Chama
Gongo la mboto DSM

Chama, tatizo la watoto wetu kufeli siyo suala la Waislamu tu. Mwaka jana katika mjadala kama huu ambapo baadhi ya watu walionesha jinsi shule za Waislamu zilivyokuwa zimefeli mimi nilionesha jinsi ya shule zenye majina ya Kikristu nazo zilifelisha. Watu wengine wanapoona majina ya seminari za Kikatoli zinapofanya vizuri wanaweza kufikiria kuwa shule zote za Kikristu watoto wake wanafaulu kwa sababu ni za Kikristu na za Waislamu wanafeli kwa sababu watoto ni WAislamu. Matokeo ya mwaka huu kwa mfano shule ya TAQWA ya Mwanza ina watoto wamefanya vizuri kuliko shule nyingi za "St. Nanino".

Hata hivyo tukiangalia kwa kutazama 'dini' tunaweza tukakosa kabisa. Ni lazima tuangalie kuwa hawa watoto wa Kiislamu ni watoto wa Kitanzania. Kufeli kwao ni hasara kwa Taifa siyo kwa Uislamu! Wanapofeli watoto wa Kikristu Muislamu hapaswi kufurahia (kwamba we are even) bali kusikitika pia kwa sababu wanaofeli ni watoto wa Kitanzania. Hatuwezi kulitatua tatizo la elimu while holding parochial sentiments...

Ni tatizo letu, na linatuhusu sote equally.
 
Unaweza kuwa sahihi lakini mimi siamini kuwa watoto hawa hawana akili ya kufundishika. KUna tatizo kubwa sana ambalo ni lazima tulishughulikie... labda hata kuangalia mitihani. Fikiria tunasema hakuna "mitaala"; Baraza la Mitihani linatunga mitihani kwa kuangalia mitaala yake; halijali wanafunzi wamejifunza nini au hata kama wamejifunza wanachotakiwa kujifunza. Sasa unamtahini vipi mtoto kwa kitu ambacho hakufundishwa?

Beleive me,hali katika shule za sekondari za kata ni mbaya sana!
Nimebahatika kufundisha kama part time shule kadhaa za sekondari za kata jijini Mbeya.
Vitabu vya rejea ni vichache sana!
Lakini pia,most of the students uelewa wao ni mdogo sana;na nadhani hii inachangiwa pia na marks ambazo wanachukuliwa toka darasa la saba ambapo sasa hadi mwenye average ya 22% anachukuliwa!
Really,watoto wengi uelewa wao ni finyu mno,na hii inachangia janga hili la matokeo.
Kuhusu suala la mitaala,ipo;na baraza la mitihani halitungi mitihani nje ya mitaala ya kufundishia.

MAPENDEKEZO YANGU:
1/Average ya ufaulu darasa la saba kwenda kidato cha kwanza iongezwe hadi walau 50%.
2/Mazingira ya kufundishia ya shule za kata yaboreshwe.
Miundombinu kama maabara na maktaba za kujisomea ijengwe.
3/Maslahi ya walimu yatazamwe upya.
 
Bila kumung'unya maneno, serikali imeshindwa katika jukumu lake la kumuelimisha kijana wa Kitanzania.

Serikali inatekeleza tu sera za Chama cha Mapinduzi. Bunge ni la CCM na wao ndio wenye kupitisha mipango ya maendeleo kila mwaka. Mwaka huu tumeona Bungeni japo kanuni zinataka kikao cha Februari kijadili na kupitisha mpango wa maendeleo, hawakufanya hivyo mwaka huu.. Tunavuna matunda ya kazi za CCM.
 
Issue ni POOR GOVERNMENT POLICY ktk elimu haiwezekani mtoto akafaulu kujiunga kidato cha kwanza halafu hawezi kuandika wala kusoma hata kitabu cha hadithi cha darasa la tatu! Huyo hata akirudia mtihani mara 100 ni kazi bure! Kwa mfano mkuu wa wilaya moja uko mkoa wa Mbeya alisema kwamba ktk wilaya yake kuna wanafunzi walioanza kidato cha kwanza mwaka huu zaida ya elfu saba (7000) hawajui kusoma wala kuandika.
Hii yote inatokana na mipango mibovu ya serikali ktk elimu. Suluhisho la haya yote ni serikali kuacha kuingiza siasa ktk elimu. Mfano hizi shule zote za kata zilianzishwa kisiasa tu ndio maana watoto wa viongozi wa serikali hawasomi ktk hizi shule za kata. E.g mh. rais J.K Kikwete watoto wake karibia wote wamesoma hizi shule tunazoziita international mfan,mwanahawa kikwete FEZA GIRLS ​.kwanini sio GONGOLAMBOTO SEC?
 
Pendekezo lako ni zuri kwa asilimia kubwa ila bado halijaangalia kiini cha tatizo na linakimbilia kulekule kwenye kutafuta suluhu ya haraka ambayo bado haitatufaa kwa kujenga taifa la wasomi imara.

Haiingii akilini kuona hakuna mtoto mwenye akili wa kupata Div I ya point 7 au 8 kufikia mwanafunzi bora kuanza na point 9. Kwanza hapa napata shaka na aina ya mtihani waliofanya. Haiwezekani kama mtaala ni uleule uliotumika miaka 2 iliyopita huwezi kuniambia hawa wa mwaka huu ni vilaza kiasi hiki. Shule ni mazingira bora ya kusomea na ubora wa walimu shule ambazo zimekuwa vinara ktk matokea hasa za private zinajitahidi sana kuboresha mazingira lazima kuna shida ya mtihani wa mwaka huu.

Pili hizi shule zetu nyingine hata kama leo hii tukisema watoto wetu warudie masomo katika mwaka huu kama amekaa darasani kwa miaka 4 bila ya kuona mwalimu wa masomo kama hisabati, biology, chemistry na physics itakuwa ngumu kwake leo kuota na kwenda kufaulu katika mwaka wake mmoja. Hii ni moja ya sababu iliyotolewa na Mtendaji mkuu wa Necta ambayo kwangu inamashiko makubwa sana kwa mustakabali wa elimu. Watoto watafaulu vipi kama hawajawahi kufundishwa somo hili hivyo walichofanya ni kuingia na kuandika namba za mitihani kisha kutoka na kuondoka zao hapa nani wa kulaumiwa kama sio wizara ya elimu na serikali kwa ujumla wake?

Yapo mengi ambayo tunatakiwa kuyatanabaisha likiwemo pia tatizo la wanafunzi kutopenda kujifunza wao wenyewe hawasomi na wanafikiri shule ni lelemama unakwenda tu kisha muda ukifika utaondoka umefaulu bila kuweka jitihada. watoto hawa jitihada kubwa kwao ni kwenye muziki wa kizazi kipya na mitandao ya kijamii kama facebook. Tunahitaji kongamano la kitaifa kujadili namna bora ya kuweka mazingira ya kuinua kiwango chetu cha elimu na kujenga taifa la wasomi wenye maarifa ya kutosha kwa sasa tunajenga taifa la kijinga. Tunazidi kutizama katika wingi wa wanafunzi wanaomaliza kama mafanikio na kusahau wamemaliza kwa ufaulu upi.
 
Ni LAZIMA yatenguliwe kama tunaamini katika utu, usawa na haki kwa watoto wetu.
Mkuu yakishatenguliwa nini kifuate? Mitihani isahihishwe upya au itungwe mitihani mingine?

Kusema mitihani isahihishwe upya, matokeo yatakuwa yale yale au pengine mabaya zaidi maana wengi waliopata zero hawakujaza kitu kabisa.

Tukisema mtihani utungwe mwingine halafu vijana wafanye upya nalo bado ni tatizo maana kwa mujibu wa Ndalichako ni kuwa wakati wanasahihisha walistushwa hadi ikabidi wawapigie walimu wa hao wanafunzi kuulizia kulikoni...jibu walilopewa ni kuwa hapakuwa na walimu wa hayo masomo husika kwa miaka yote kwa hizo shule.

Nadhani hapo tumeshaujua mzizi wa tatizo. Mbatia alikuwa sahihi ilaa tu hawa jamaa wanaleta sifa za kipuuzi huku wakitutengenezea taifa la wajinga.
 
Tatizo kadri siku zinavyosonga mbele, swala la elimu tunalifanya la kisiasa zaidi. Kukabiliana na hili tatizo la elimu lazima serikali itafute ufumbuzi wa matatizo ya walimu. Walimu (sijui kwa sababu ya wingi wao na wengi kufanya kazi katika mazingira magumu vijijini) wamekuwa watu wakupuuzwa tuu. Ni vema watanzania tukae chini tufanye national dialogue kuhusu mstakabali wa elimu yetu. Tunashindwa kujua kila kitu kina 'elastic limits'. Unakivutaa mwishoni kitakatika tuu. Walimu wamepuuzwa kwa mda mrefu and we have started paying dividends albeit in a negative way.

Kazi yoyote ile inahitaji motisha. Haiwezekani mwalimu umpe kipato kidogo as if yeye hana familia ya kutunza na mahitaji mengineyo kama watumishi wengine. Otherwise, tuwe tayari kuona traditional school za makanisa zikiendelea kufanya vizuri at the expense ya shule za kata (perhaps tujiulize kwa nini hizi shule za misheni zinafanya vema?). Na tunakoelekea ni kubaya zaidi maana shule nyingi za kanisa zimekuwa zikitoa fursa sawa kwa wanafunzi wa imani zote...sasa na huu ukabila na ukanda na udini unaohubiriwa na akina Nape majukwaani..tutafika level..hata mfano waislamu wakienda kwenye hizi shule they dont feel confortable.

Bila kukaa chini kama watanzania wa taifa hili tukajadili tofauti zetu..Nina hakika watoto wetu hatutawaachia Tanzania tuliyoachiwa na akina Nyerere.


Hatujachelewa kila mtu atimize wajibu wake.
 
Mwanakijiji, kurudia mitihani ni solution ya muda hiyo ninakubaliana na wewe, ili watoto wapate last chance kwa kuwa failure yao ina makando kando mengi yaliyokuwa juu ya control yao.Fikiria mwalimu anayesahihisha mtihani amekasirika mwanafunzi hana control kwa hilo.

Lakini baraza likikaa likubali mjadala wa kujadili mgomo wa waalimu uliowasilishwa mwaka jana na mh.Mnyika bunge letu DHAIFU chini ya spika DHAIFU na msaidizi DHAIFU na katibu DHAIFU likubali sasa kujadili ili kuwapa pia nafasi waalimu wawakilishi kuwasilisha madai yao.
Pamoja na kutokuwepo mtaala kama walimu watakuwa wametulia kiakili na wakapata recognition from serikali DHAIFU nadhani something fruitful could be delivered.
 
Hivi ile mifuko ya jimbo ina kazi gani wajameni. Pengine kazi yake ingekuwa kuboresha elimu tu na si vinginevyo ingesidia sana.
 
Serikali inatekeleza tu sera za Chama cha Mapinduzi. Bunge ni la CCM na wao ndio wenye kupitisha mipango ya maendeleo kila mwaka. Mwaka huu tumeona Bungeni japo kanuni zinataka kikao cha Februari kijadili na kupitisha mpango wa maendeleo, hawakufanya hivyo mwaka huu.. Tunavuna matunda ya kazi za CCM.

Hapo kwenye RED. kusema bunge ni la CCM ni kutumia lugha za kisiasa ili kupotosha maana nzima ya Bunge. Bunge ni la wananchi kwa maana kuwa, Wabunge wanapokuwa Bungeni, hawawakilishi chama bali wananchi bila kujali vyama vyao.

Ni kweli wa kulaumiwa ni CCM na serikali yake kwa kushuka kwa kiwango cha elimu kama kilivyonyambulishwa na kuanikwa na matokeo ya kidato cha nne mwaka huu pamoja na kwamba budget ya elimu iko kwenye ration ya 17-21% ya budget ya nchi.

Mawazo yako ni mazuri lakini yanalenga kutatua tatizo kwa sasa (in the short run) lakini siyo kwa milele (in the long run).

Ninakubaliana na wewe, kama ilivyo kwa wenzetu wa nchi za magharibi (UK), mfumo wa elimu uko decentralized na elimu ya msingi iko chini ya uangalizi wa serikali za mitaa.

Mjadala kama huu unakuja katika kipindi kizuri kwa jamii kujua vizuri sera za vyama vya siasa kuhusu elimu na utekelezaji wake, ili kufikia mwaka 2015, wananchi watakuwa wamefahamu ni chama kipi cha kukikabidhi mstakabali wa elimu nchini.
 
Naogopa kusema utakimbilia kuniban kwenye thread yako ila akili za kibinadamu kidogo zimeanza kurudi; najua huu ni msiba wa wengi mtakuja na kila aina ya suluhisho; kama unakumbuka mwaka jana waislamu walilamika sana kuhusu Wizara ya elimu na Baraza la mitihani; kama wengi wenu humu JF mngeelewa kilichokuwa kinalalamikiwa labda matokeo ya leo div 0 zingekuwa 1000 tu; ila nashukuru Mungu ukweli umeanza kujionesha.

Chama
Gongo la mboto DSM

Mtu ambae hajishughulishi kufikiri ndie atakaeamini kuwa KINGEFANYWA KITU MWAKA JANA MATOKEO YA MWAKA HUU YASINGEKUWA HIVI YALIVYO.

Waathirika wa matokeo ya mwaka huu hawakuanza kusoma mwaka jana, na ni uvivu wa kufikiri kuamini kuwa matokeo haya si matokeo ya mambo ya hovyo yaliyofanyika kwa miaka 12 ya elimu ya watahiniwa ambao matokeo yake tunayajadili leo. Ukichukua hatuaa leo, athari (mbaya au kinyume) zitaanza kuonekana si mwakani bali at least five years to come.
 
Mwanakijiji,
Nadhani kuna mambo ambayo yanapindishwa hapa.
1. Wizara ya elimu ndiyo yenye wajibu wa kuhakikisha watoto wanafundishwa kwa kuzingatia mitaala iliyokubaliwa. Wizara ndiyo inayojua(au inapaswa kujua) shule zenye walimu na ambazo hazina, na pia ni wizara yenye wajibu wa kutoa suluhisho la upungufu wowote kwenye elimu (maana wizara ina wakaguzi wa mashule wanaolipwa mishahara nk. Hivyo kuongelea baraza la mitihani katika dhahama hii ni kupotosha hoja.
2. Hatuwezi kuendelea kupoteza muda kutafuta sababu za watoto kufeli. Tuangalie ni sababu zipi zitawafanya wafaulu - na kujenga uwezo wetu wa kufanya mapinduzi kufikia lengo hili. Hatutabadili hali hii kwa kutoa hoja na maelezo rahisi, hali hii itabadilishwa kwa kufanya mapinduzi katika fikra na tabia zetu (hasa watu wazima wenye wajibu na dhamana juu ya mustakabali wa maisha ya watoto hawa na taifa kwa ujumla.

3. Moja ya pendekezo la haraka haraka ni hili: Katika kambi zetu za JKT ziwe ni taasisi za kijeshi za elimu, ambazo wanafunzi wooote waliopata daraja la 3, 4, 0 watakwenda moja kwa moja matokeo yao yakitoka. Na ni kutokea katika makambi haya ya jeshi - taasisi kama vyuo vya waalimu, VETA, na shule za juu za sekondari zitawachukulia wanafunzi wao. Ni hapa mitihani itarudiwa, ufundi wa kila aina watajifunza - na wakitoka watatoka watu wenye VISION AND PURPOSE IN LIFE.
* Makambi ya JKT viwe vituo vya kuandaa vijana hawa.
*Tukiwekeza kwenye makambii haya yatakuwa ni alternative nzuri, badala ya kuwapeleka wanafunzi wooote Alevel wawe wananyooshwa na makambi haya.
*Pia badala ya kuwapeleka wabunge kwenye makambi haya, wapelekwe hawa watoto, wapikwe, wanyooshwe, waelekwezwe.

4.Baraza la mitihani liendelee kuwa na wajibu wa kutoa mitihani kwa kuweka viwango vya juu ambavyo ni lazima wanafunzi wafanye kazi kubwa kuvifikia. Mitihani isirahisishwe kamwe.


Unaweza kuwa sahihi lakini mimi siamini kuwa watoto hawa hawana kili ya kufundishika. KUna tatizo kubwa sana ambalo ni lazima tulishughulikie... labda hata kuangalia mitihani. Fikiria tunasema hakuna "mitaala"; Baraza la Mitihani linatunga mitihani kwa kuangalia mitaala yake; halijali wanafunzi wamejifunza nini au hata kama wamejifunza wanachotakiwa kujifunza. Sasa unamtahini vipi mtoto kwa kitu ambacho hakufundishwa?
 
A TREND OF FORM FOUR RESULTS SINCE 2009

2012 Form 4 results

DIV 1: 1,641 (0.4%)
DIV 2: 6,453 (1.6%)
DIV 3: 15,426 (3.9%)
DIV 4: 103,327 (26.0%)
DIV 0: 240,903 (60.1%)

2011 Form 4 results

DIV 1: 3,671 (1.09%)
DIV 2: 8,112 (2.41%)
DIV 3: 21,794 (6.84%)
DIV 4: 146,639 (43.60%)
DIV 0: 156,085 (46.41%)

2010 Form 4 results

DIV 1: 5,363 (1.53%)
DIV 2: 9,944 (2.83%)
DIV 3: 25,107 (7.14%)
DIV 4: 136,777 (38.9%)
DIV 0: 174,407 (49.60%)

2009 Form 4 results


DIV 1: 4,419 (1.78%)
DIV 2: 10,493 (4.21%)
DIV 3: 27,310 (11.2%)
DIV 4: 130,651 (52.61%)
DIV 0: 65,708 (26.46%)
 
NA KWAKUWA kuna watoto wengine walipata Daraja la IV na O kutokana na kuchora kina Messi na Zombie, hao nao wapelekwe kwenye vyuo maalumu vya Sanaa wakajifunze "U -Masudi Kipanya" na Utungaji wa Tamthilia kwani wameonyesha vipaji vya hali ya juu kwenye Mitihani, HIVYO BASI wasiachiwe akapotelea mitaani.

ndalichako.jpg
 
Nafahamu watoto waliopata div 0 wakarudia kuanzia kidato cha 3, na naona wamepata div 0 tena. Hao waliopata div 0 au div 4 wakirudia watapata hizo hizo.

Huwezi kutakata kwa kuoga mara ya pili kwenye maji machafu.

We need to go back to basics. Timu iliyotufikisha hapa haina uwezo wa kuhuisha Elimu yetu.

Njia za kuhuisha Elimu yetu zipo na zinajulikana. Kinachokosekana ni utashi wa kuzitekeleza.
 
What if mwakani mambo yakawa hivi hivi? kwa watoto wakishaona kuna second chance....ndo watafanya vibaya zaidi...kwa matarajio kuwa wanayo nafasi nyingine...al in al ni mchango mzuri.


bado nichangamoto.. ila wale ambao kweli wamedhamiria kusoma wakipewa nafasi nyingine wanaweza kufanya vizuri.
sijui wale kina Kikwete na kinalowasa waliokuwa wanafanya bidii na matunda ya kusoma yakapatikana watatokea wapi.. ukifaulu siku hizi shule ya Kata mwisho wake nyumbani..
 
A TREND OF FORM FOUR RESULTS SINCE 2009

2012 Form 4 results

DIV 1: 1,641 (0.4%)
DIV 2: 6,453 (1.6%)
DIV 3: 15,426 (3.9%)
DIV 4: 103,327 (26.0%)
DIV 0: 240,903 (60.1%)

2011 Form 4 results

DIV 1: 3,671 (1.09%)
DIV 2: 8,112 (2.41%)
DIV 3: 21,794 (6.84%)
DIV 4: 146,639 (43.60%)
DIV 0: 156,085 (46.41%)

2010 Form 4 results

DIV 1: 5,363 (1.53%)
DIV 2: 9,944 (2.83%)
DIV 3: 25,107 (7.14%)
DIV 4: 136,777 (38.9%)
DIV 0: 174,407 (49.60%)

2009 Form 4 results


DIV 1: 4,419 (1.78%)
DIV 2: 10,493 (4.21%)
DIV 3: 27,310 (11.2%)
DIV 4: 130,651 (52.61%)
DIV 0: 65,708 (26.46%)

Watanzania wasitishe kuzaa kwa sasa.. Hiyo ndo suluhisho la kwanza.. Tuwaepushe watoto kuja kuwa mazezeta..
 
Mawazo yako ni mazuri, lakini sikio la kufa halisikii dawa. jk na serikali yake ya ccm wanajulikana kwa kukataa ushauri wa aina yoyote wenye tija na maslahi kwa wananchi wa hali ya chini. Watalichangamkia tu suala ambalo mwisho wa siku maslahi makubwa zaidi yako kwao wenyewe.
 
Back
Top Bottom