Pemba: Viongozi wa ACT, Maalim Seif na Salim Bimani waitwa Polisi. Washutumiwa kufanya mkutano bila kibali, waachiwa kwa dhamana

beth

JF-Expert Member
Aug 19, 2012
3,877
6,326
1578994364451.png

Mshauri mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Kamati ya Itikadi na Uenezi wa ACT Wazalendo Salim Bimani wameripoti katika Kituo cha Polisi Wete Pemba asubuhi ya leo.

Viongozi hao wa ACT Wazalendo wameitwa na Mkuu wa Upelelezi wa Jinai (RCO) Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Wananchi na Wanachama wa ACT - Wazalendo wamekuwa nje ya maeneo ya karibu ya jengo la Polisi la Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa lengo la kujua hatma ya viongozi wao wanaohojiwa na inadaiwa wamejiandaa na kuwachukulia dhamana ikibidi.

1578993907233.png



1578993934479.png


UPDATE:
Mshauri Mkuu wa ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Salim Bimani wameshutumiwa kufanya mkutano bila kibali mwezi Desemba 2019 huko Micheweni Zanzibar.

Hata hivyo, Viongozi hao wameachiwa kwa dhamana na kupitia Mtandao wa Twitter Chama chao kimedai kuwa walifanya mkutano wa ndani usiohitaji kibali.

1578998744657.png
Jeshi la Polisi limewachia kwa Dhamana Mshauri Mkuu wa Chama @ACTwazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na M/kiti wa kamati ya Itikadi na uenezi wa Chama hicho Salim bimani Baada ya hii leo kuitwa kufanyiwa mahojiano na Jeshi hilo katika kituo cha Polisi mkoa wa kaskazini Pemba.
 
January 14, 2020
Wete, Pemba
Tanzania

Wakaazi wa mji wa Wete, kaskazini Pemba, wamejitokeza mitaani kumpokea na kumsindikiza Maalim Seif Sharif Hamad, ambaye alikwenda polisi kuitikia wito wa kuhojiwa na jeshi hilo leo.

Kulikuwepo na nyimbo nyingi za kutiana hamasa ya mshikamano kuwa kiongozi wao alipo wapo na hawawezi kurudi nyuma kimsimamo kuacha kumsindikiza kipenzi chao Maalim Seif kwenda mwenyewe kuitikia wito Polisi


Source: Weyani TV
 
Hahaha walianzishe mapema kabla ya October 2020, tuko nyuma yao.

Mbona wanampenda kuliko Magufuli na Shein, wao hawa wananchi hawaogopi kupotezwa?!

Alisema mwenyewe mkipotezwa msiwahusishe usalama.

Ccm wakiona hivyo roho zinauuma.
 
Hahaha walianzishe mapema kabla ya October 2020, tuko nyuma yao.

Mbona wanampenda kuliko Magufuli na Shein, wao hawa wananchi hawaogopi kupotezwa?!

Alisema mwenyewe mkipotezwa msiwahusishe usalama.

Ccm wakiona hivyo roho zinauuma.
Ukiona hivo ujue haki ilikuwa kwenye sanduku la kura
 

Mshauri mkuu wa Chama cha ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Kamati ya Itikadi na Uenezi wa ACT Wazalendo Salim Bimani wameripoti katika Kituo cha Polisi Wete Pemba asubuhi ya leo.

Viongozi hao wa ACT Wazalendo wameitwa na Mkuu wa Upelelezi wa Jinai (RCO) Mkoa wa Kaskazini Pemba.

Wananchi na Wanachama wa ACT - Wazalendo wamekuwa nje ya maeneo ya karibu ya jengo la Polisi la Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa lengo la kujua hatma ya viongozi wao wanaohojiwa na inadaiwa wamejiandaa na kuwachukulia dhamana ikibidi.

UPDATE:
Mshauri Mkuu wa ACT Wazalendo Maalim Seif Sharif Hamad na Mwenyekiti wa Itikadi na Uenezi wa chama hicho, Salim Bimani wameshutumiwa kufanya mkutano bila kibali mwezi Desemba 2019 huko Micheweni Zanzibar.

Hata hivyo, Viongozi hao wameachiwa kwa dhamana na kupitia Mtandao wa Twitter Chama chao kimedai kuwa walifanya mkutano wa ndani usiohitaji kibali.

Nchi inawenyewe na wenyewe ni CCM.
 
Kule Pemba JESHI LOTE LA POLISI NI WAFUASI WA MAALIM nyie maccm amri Zenu Kwa jeshi la polisi fanyeni huku bara wasikojitambua kule Wana itikadi tofauti ndiyo amepewa dhamana fasta na yupo nje anapiga zake siasa
 
Kule Pemba JESHI LOTE LA POLISI NI WAFUASI WA MAALIM nyie maccm amri Zenu Kwa jeshi la polisi fanyeni huku bara wasikojitambua kule Wana itikadi tofauti ndiyo amepewa dhamana fasta na yupo nje anapiga zake siasa

January 14, 2020
Wete, Pemba

Maalim Seif akitoka kituo cha Polisi mara baada ya kuitikia wito na kulakiwa kwa shangwe, bashasha, vifijo na wananchi wa Wete, Pemba
 
Back
Top Bottom