PC na QT Special Thread

Unataka usome ili badae uje kuwa nani(kufanya kazi gani)? labda tuanzie hapo.
 
Sio kweli niliwah ambiwaa kua alama za ufaulu kwa wote ni sawaa
Japo nikadokezewa kua usahihishaji wa PC sio mzuri saaana (hii sina uhakika)
Kumbuka wale madogo wa Continous Assesment afu PC hana. Wasahihishaji wa PC wako makini maana wanajua PC kajipanga kutusua kwa hiyo yakupasa PC uchimbe mara 4 zaidi ya SC
 
Mimi naishi DSM, ila kwa sasa nipo Zenji mara moja!
 
Dah kwel mkuu inaumiza sana me kila nikitaka kurisit nakuwa mzito napokutana namada kama hizi
 
Cha kwanza fanya maamuzi magumu..!
Lakini wanasema ukitaka upate kitu zaidi ya ulichokipata sasa hivi itakubidi kufanya zaidi ya ulivofanya kupata ulichokipata sasa hivi..!
Chamsingi ni kugundua unapokesea mara zotee sahihisha then jitume kweli kweli lazma umove..!
Mimi mwenyew shahidi sikua serious mara ya kwanza nlivokua SC lakin nlivoshindwa nikaangalia wapi nlipoteleza nikasoma mwaka mmoja tuu kama PC na nikapata nlichokitaka..!
Lazima ujitoee
 
Hongera
 
Ina maana unawatushauri tununue vitabu vyenye maswali na majibu ili tuhipime c ndio au
 
Ina maana unawatushauri tununue vitabu vyenye maswali na majibu ili tuhipime c ndio au
Mara nyingi unavorudia mtihani kama hivo ni vigumu kupitia topic zote kutokana na muda uliopo lakini kupitia maswali mbali mbali itakusaidia kuelewa mengi kwa muda mchache..
Unaweza ukanunua vitabu lakin pia past papers toka shule nyingine zinazofanya vizuri jaribu kupata maswali yao na kussolve itakusaidia sanaa
 
Shukran sana
 
Nilifeli mwaka 2012, mwaka ambao walitangaza matokekeo Mara mbili, nikakata tamaa ya kuendelea na shule, nikaingia mtaani nikapata kazi kwenye kampuni mmoja, kwa kubebwa tu, manyanyaso na nikajiuliza nini hatima ya maisha yangu bila Elimu Maana sikupata hata Cheti, japo ninakazi naendesha maisha yangu niliamua kurudia mtihani mwaka Jana, kutokana na Majukumu nikajisemea moyoni wacha nirudie haya matano, kweli nilirudia na namshukuru Mungu nimepata kitu ninachokitaka, naomba mtumie thl wanamaswali zaidi ya elfu KUmi, ilinisaidia sana ukizingatia sikuwa na mda wa kutosha wa kujisomea na kutafuta material
 
Uko sahihi mkuu wale jamaa wana maswali na notes nzuri kweli yani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…