Fumbokhan
Member
- Jan 16, 2021
- 6
- 20
Kuna watu mitaani wameharibikiwa na hawapo kabisa mitandaoni. Kuna vijana wengi walilelewa geti Kali tena familia za kidini lakini bado wameharibikiwa kwa vitendo vya umalaya na madawa ya kulevya. Kwahiyo si kila wakati mzazi Ni wa kutupiwa lawama, Kuna wakati mtu mwenyewe anatakiwa kujitambua kujua zuri na baya. Kuna watu wazazi wao walikuwa makahaba ila wao wamejikuza katika maadili
Tukiachana na hayo, upande mwingine wa Paula ni binti mdogo lakini yupo potential sana katika glamour world/entertainment world
Ikiwa atapata usimamizi mzuri kuanzia wazazi na na usimamizi wa kikazi. Paula ametokea kupata attention mapema hata kabla hajamaliza shule na bila kuanza kuonesha kipaji
Watu wanaenda shule ili kuelimika na kuwa na kazi au maisha mazuri, Paula ameanza kuvutia makampuni
awatangazie bidhaa zao hivyo asivunjwe moyo bali awekwe sawa potential yake isipotee sababu hata akimaliza shule atahitaji kazi kupata pesa maisha yaende. Kuna wasomi wengi na degree zao bado ajira kwao imekuwa shida kupata hivyo Paula asikatishwe sana tamaa hata kwenye fursa
Lulu alipitia changamoto kubwa katika umri mdogo lakini wazazi walimuweka sawa bila kumkatisha tamaa ya kile alichokipenda zaidi(Sanaa) na Leo amekuwa role model na fursa kupitia Sanaa zimempa fursa nzuri lakini majaribu mazito aliyopitia wazazi wake wasingeangalia upande wa pili wangemkataza asiendelee na sanaa
Jenifer Kanumba alipata usimamizi mzuri wa wazazi na Sasa yupo chuo kikuu bila kuacha Sanaa ambayo inamuwezesha kujikimu.
Kylie Jenner aliacha shule akiwa na miaka 17 ili kuipa attention career ya reality star na fashion. Akapata usimamizi mzuri na Sasa Ni billionea kabla hajafikisha miaka 25. Biashara ya vipodozi kupitia mitandaoni ndio imempa hadhi ya bilionea
Wanamitindo wengi wa kimataifa husainiwa wakiwa na miaka 14 kuanza kazi huku wakiwa bado wanasoma shule kwa kupewa uangalizi mzuri. Ryan Kaji mtoto wa miaka 10 mwaka 2020 pekee aliingiza dola million 29.5 zaidi ya billion 60 za kitanzania kupitia YouTube na mwaka 2019 yeye pia ndie alikuwa mtu aliyeingiza pesa nyingi duniani kupitia YouTube. Hayo yamewezekana kupitia usimamizi mzuri wa wazazi baada ya kuona kipaji Cha mtoto wao wakaona wamtumie vizuri katika mitandao aingize pesa
Kwahiyo hata Paula asikatishwe tamaa upande mwingine ambao ana potential kubwa ya kuanza kuingiza pesa ikiwa atapata usimamizi mzuri huku anaendelea na shulen