Tindo
Platinum Member
- Sep 28, 2011
- 69,547
- 122,980
Mtikisiko wa dr slaa matokeo yake ndio haya chama kupoteza watu muhimu kwa kukosa dereva!
Kipara kipya si vibaya wewe kama mwanaccm kujifariji, tuliowengi na post zetu zipo hapa jukwaani toka alipochaguliwa kwamba huyo Patrobas sio aina ya viongozi wanaofaa kuendesha Bavicha. Kuna waliomtetea, leo tulioona uzito wa utendaji wake tuna raha ya ajabu kwa kuondoka kwake. Pia kuondoka kwa Masha ni faraja ya ajabu tunaomba na mamvi naye achape mwendo tufurahi zaidi. Tunamtakia Patrobas maisha mema huko ccm kuliko mlivyotarajia eti litakuwa pengo. Alipokuwa chamani ukiacha sura yake hata mchango wake ulikuwa mdogo sana, kwa maneno marahisi yeye alikuwa pengo tayari kwa kuwa mwenyekiti wa Bavicha. Sio kwamba hakuwa na sifa nyingine lakini nilimkubali sana kwenye uwezo wake wa kujenga hoja na sio utendaji wake. Kwa jinsi mlivyomfurahia huko ccm kwamba mmepata kifaa, na sisi huku cdm tumefurahi sana kuvuja kwa pakacha.