Patrobas Katambi: Vijana 1,732,509 hawana ajira Nchini

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,812
11,987
Fuatilia yanayojiri Bungeni leo, Februari 3, 2023 Kwenye Bunge la 10, Kikao cha 4



Serikali yasema Vijana 1,732,509 hawana ajira
Akizungumza Bungeni, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Paschal Katambi amesema:

“Utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa Mwaka 2021 unaonesha kuwa vijana wenye umri wa miaka 15-35 ambao wanaukosefu wa ajira ni 1,732,509 sawa na 12% ya nguvu kazi ya vijana wenye umri huo ambao hawana ulemavu unaowazuia kufanya kazi.

“Katika kuhakikisha vijana wanaendelezwa ili kushindana katika soko la ajira ndani na Nje ya Nchi, Serikali imeweka mkakati wa kitaifa wa kukuza ujuzi wa miaka 10 ambapo imefanya maboresho ya mitaala katika elimu ya juu na ya kati kwa mafunz ya stadi ya ufundi.

Pia kuna maboresho kwa vijana walio nje ya mafunzo rasmi kama uanagenzi, mafunzo ya uzoefu kazini (internship) na mafunzo ya kilimo cha kisasa.


MBUNGE APENDEKEZA MAWAZIRI WAPATIKANE KWA KUOMBA KAZI
Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina akiwa Bungeni amehoji “Kwanini Serikali isiache utaratibu wa ajira kwa njia ya uteuzi ili kupata watu wenye uwezo ambao hawatiliwi mashaka, ajira ipatikane kwa njia ya ushindani iwe kwa viongozi, watendaji, Mawaziri, Wakurugenzi, Makatibu Wakuu na watendaji wengine Serikalini.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Paschal Katambi akajibu “Kwa sasa Katiba yetu ya Mwaka 1977 inaeleza mfumo wa uendeshaji wa Serikali na inatambua mifumo ya uteuzi na ushindani kulingana na nafasi zinazohitajika.”
 
Kikao Cha chama chama pinduzi mkuu
Wanapeana mipasho tuu... Badala ya kujadili maslahi ya taifa
 
Fuatilia yanayojiri Bungeni leo, Februari 3, 2023 Kwenye Bunge la 10, Kikao cha 4



Serikali yasema Vijana 1,732,509 hawana ajira
Akizungumza Bungeni, Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Paschal Katambi amesema:

“Utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa Mwaka 2021 unaonesha kuwa vijana wenye umri wa miaka 15-35 ambao wanaukosefu wa ajira ni 1,732,509 sawa na 12% ya nguvu kazi ya vijana wenye umri huo ambao hawana ulemavu unaowazuia kufanya kazi.

“Katika kuhakikisha vijana wanaendelezwa ili kushindana katika soko la ajira ndani na Nje ya Nchi, Serikali imeweka mkakati wa kitaifa wa kukuza ujuzi wa miaka 10 ambapo imefanya maboresho ya mitaala katika elimu ya juu na ya kati kwa mafunz ya stadi ya ufundi.

Pia kuna maboresho kwa vijana walio nje ya mafunzo rasmi kama uanagenzi, mafunzo ya uzoefu kazini (internship) na mafunzo ya kilimo cha kisasa.


MBUNGE APENDEKEZA MAWAZIRI WAPATIKANE KWA KUOMBA KAZI
Mbunge wa Kisesa, Luhaga Mpina akiwa Bungeni amehoji “Kwanini Serikali isiache utaratibu wa ajira kwa njia ya uteuzi ili kupata watu wenye uwezo ambao hawatiliwi mashaka, ajira ipatikane kwa njia ya ushindani iwe kwa viongozi, watendaji, Mawaziri, Wakurugenzi, Makatibu Wakuu na watendaji wengine Serikalini.

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu), Patrobas Paschal Katambi akajibu “Kwa sasa Katiba yetu ya Mwaka 1977 inaeleza mfumo wa uendeshaji wa Serikali na inatambua mifumo ya uteuzi na ushindani kulingana na nafasi zinazohitajika.”

sawa waendelee na mipasho yao huko dodoma ccm hawana nia ya dhati kumkwamua mtanzania kutoka kwenye lindi la umasikini, ngoja niende yutube nikasikilize hoja za Lisu na clouds 360
 
“Utafiti wa watu wenye uwezo wa kufanya kazi wa Mwaka 2021 unaonesha kuwa vijana wenye umri wa miaka 15-35 ambao wanaukosefu wa ajira ni 1,732,509 sawa na 12% ya nguvu kazi ya vijana wenye umri huo ambao hawana ulemavu unaowazuia kufanya kazi.
Takwimu za michongo tupu.
 
Takwimu za ujanjaujanja tu!. Eti uanagenzi! Kwa nn usiwe uanazengo!.

Mwigulu Nchemba anafisidi nchi halafu anajificha kwenye kivuli Cha Rais Cha madarasa elfu 8 kwa BILIONI 160!. BILIONI 160!. BILIONI 160!. NARUDIA Tena BILIONI 160!.
 
Back
Top Bottom