Pasco - Unawezaje kusema maneno kama haya ?

Pasco - Unawezaje kusema maneno kama haya ?

31525_20130201_132641_life_quotes_03.jpg
 
Waarabu wote wameshindwa
kuwapoteza Jews siyo Iran, Iraq, Afghanstan na hata wakiungana
wameshindwa!! Wamebaki "kutamani tu" kama wewe!!

niongezee kidogo, hakuna popote mauaji ya kimbari yaliwahi fanikiwa, hata herode alijaribu bado hakufanikiwa kuwaangamiza wayahudi, wahutu vilevile.
 
Tatizo ndugu mleta mada imani yako yote umeiweka kwa Pasco...

Huo ni mtazamo wake na sio kila mtazamo wa Pasco ni sahihi...
 
Last edited by a moderator:
Nilikuwa napitia posts hapa JF na nikakutana na hii statement aliyoitoa Pasco (rangi nyekundu hapa chini)....I was shocked !.

" Moja ya makosa makubwa sana Hitler aliyoyafanya, na kuwabakiza baadhi ya hawa jamaa!, walipaswa wote kabisa wawe wiped kwenye uso wa dunia ndipo asamani ya kudumu ingepatikana enero la Mashariki ya Kati "


Pasco wewe hapa JF, kwa watu wengi unajulikana ni mtu mwenye upeo mkubwa na vile vile kama sijakosea ni mwandishi wa habari. Kama mtu kama wewe ambaye kwa uelewa wako, utakuwa unajua genocides zote huwa zinaanza na propaganda za chuki na hatimaye zinawaingia watu mpaka wanakuwa kama wanyama na kuanza kuua watu wengine kwa sababu tu ya race zao, unawezaje kusema maneno kama haya !!!????

Miaka kama kumi hivi iliyopita, kuna wakati fulani, nilispend kama week nzima kusoma history ya vita kuu ya pili na niliposoma mauaji aliyokuwa anayafanya Hitler ya kuchukua watu na kuwaingiza kwenye gas chambers na kuua mamilioni ya watu kwa njia hiyo, nikajaribu kujiuliza, Hitler aliwezaje kuwashawishi na kuwafanya wajerumani wakubali kuwa wanyama kiasi hiki !. Lakini leo nilipoona statement yako hii, nikawaza, kama mtu kama Pasco anaweza akatamka maneno kama hayo, then kitu kama hiki kikianza kutokea duniani atakisupport na kama mtu wa uelewa wako Pasco atasupport kitu kama hiki, mbona ni rahisi kwa wengine wenye uelewa mdogo kukitekeleza....Probably hata wewe unaweza ukajikuta uko mstari wa mbele kutekeleza.....Ndio maana kwa wajerumani sasa hivi, manano kama hayo uliyoyasema yangekupeleka selo ! Wanajua problem ya statement za chuki kwani wame-experience first hand, na mpaka sasa hivi, wengi wao bado wana wakati mgumu kui-face history yao kama taifa !

Hakuna mtu anayezaliwa mnyama, tunabadilika na kuwa kama wanyama kwa kudharau vitu vidogo kama hivi na kutojifunza kutokana na history ! Baada ya hitler, bado genocides zimeendelea kutokea duniani (mojawapo ni kwa majirani zetu Rwanda) na kwa mtindo kama wa kwako Pasco ninalazimaka kwa masikitiko makubwa kuamini kwamba zitatokea tena na tena na tena.....

Wakati wewe, unafurahia kwamba Hitler alijitahidi kuangamiza race fulani hapa duniani, na wakati huo huo kusikitika kwamba alishindwa kumaliza kazi, Wajerumani, ambao Hitler alikuwa kiongozi wao, wameweka sheria kwamba kumshabikia hitler ni kosa kubwa kwa mujibu wa sheria zao !

Kwa kweli leo nimeamini usemi huu maarufu : "We learn from history that we never learn anything from history".

Mkuu jebibay, hiki ulichokiandika hapa yafaa Pasco aombe radhi, kwani kushabikia genocide ni tatitizo kubwa sana. Leo hii tunashuhudia propaganda za CCM na "ukaskazini"...watu wanadhani ni jambo dogo, lakini ukweli umedhihirika pale sasa kuwa Mchagga ni kosa la kutokupewa uongozi. Tunashuhudia watu wakibagua waziwazi kwamba Raisi hawezi kutoka Kaskazini, na Pasco ambaye ni mwandishi wa habari alitakiwa asaidie kuelimisha jamii juu ya ubaya wa kuwatenga watu kwa makabila, na maeneo. Ni vizuri umelileta hili ili watu walijadili kwa mapana, na kwa kuwa Pasco ni mtu mwelewa pengine atakuja hapa aeleze alikuwa na maana gani?
 
Last edited by a moderator:
Pasco kashajibu kwa like za kutosha ungekuwa umesoma comment zote kabla ya ku comment usinge comment..

Sishabikii ubaguzi wa ki itikadi, mazingira, imani, rangi wala aina yoyote itakayo wabagua watu. ila tusimbague kwa imani yake au kwa sababu anaamini genocide whatever...

Mkuu jebibay, hiki ulichokiandika hapa yafaa Pasco aombe radhi, kwani kushabikia genocide ni tatitizo kubwa sana. Leo hii tunashuhudia propaganda za CCM na "ukaskazini"...watu wanadhani ni jambo dogo, lakini ukweli umedhihirika pale sasa kuwa Mchagga ni kosa la kutokupewa uongozi. Tunashuhudia watu wakibagua waziwazi kwamba Raisi hawezi kutoka Kaskazini, na Pasco ambaye ni mwandishi wa habari alitakiwa asaidie kuelimisha jamii juu ya ubaya wa kuwatenga watu kwa makabila, na maeneo. Ni vizuri umelileta hili ili watu walijadili kwa mapana, na kwa kuwa Pasco ni mtu mwelewa pengine atakuja hapa aeleze alikuwa na maana gani?
 
Tukirejea ''hansadi'' za JF-.https://www.jamiiforums.com/member.php?u=12004
Pasco
si mpenda vurugu za aina yoyote ile
[h=2]1.Vurugu Bungeni-"Blessing in Disguise!"- "Ni Kitendo cha Kishujaa! Kinachostahili Kupongezwa!".

[/h] Kwa kuanzia, japo siungi mkono vurugu za aina yoyote,......
Pasco ni mpenda ''umoja''
....ni kiashiria cha kwanza cha mwanzo mzuri wa a "United We Stand!" na mwisho wa "Divided we Fall!".


2.Pasco alipokuwa akimsifu marehemu Regia(R.I.P)
Kumbukumbu ya Regia:"She was No Nonsense Lady!" Mwenye"Upendo" Jee Wewe Unamkumbuka Kwa Lipi?.!
Regia alikuwa ni mtu wa maneno mafupi na vitendo virefu, ila kubwa kuliko yote ni alikuwa ni mtu wa Alikuwa ni mtu wa upendo na kusamehe, asiye na kinyongo wala kuweka vitu moyoni!
3.Pasco AKIZUNGUMZIA UDINI NA UKABILA...
Sumu ya Siasa za Udini, Ukanda na Ukabila, "Is It

Jee mbegu hii ya sumu kaipanda nani?, jee tunaweza kuipiga vita kwa kuikanusha tuu (denial) au tunatakiwa kuubali ukweli mchungu na kukabiliana nao (facing the problem)!.

Nauliza tuu?

Pasco

4.Pasco ALIPOTOA TANGAZO LA MEDITATION
[h=3]Mafunzo ya Meditation Bure. Ni Kupitia Brahima Kumaris Meditation Centre!.
Started by Pasco, 25th April 2012 17:08[/h]The term meditation refers to a broad variety of practices (much like the term sports) that includes techniques designed to promote relaxation, build internal energy or life force (qi, ki, prana, etc.) and develop compassion,[SUP][3][/SUP] love, patience, generosity and forgiveness.


MY TAKE: Pasco,UBAYA WA MTU/WATU SI JUSTIFICATION YA KU'ERASE'' RACE NZIMA....
 
Back
Top Bottom