Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 19,768
- 49,934
Nilipoona kuwa shetani alikuwa akitenda kazi ndani yake ni pale alipoanza kuuua watu, kuteka, kubambikia watu kesi.Yule jamaa kosa lake aliwachukia Sana CHADEMA. Tatizo lilianzia Hapo ila mengine alijitahidi kwa uwezo wake. Baya moja hufuta mazuri yote.
Binadamu wengi tu wadhambi, lakini pamoja na dhambi zetu, hatujawa watumishi wa shetani. Ukiona mtu anaua, anadhulumu iwe mali au uhai wa watu, tambua kuwa huyo ni mtumishi/agent wa shetani. Na mtu wa namna hiyo, hawezi kudumu maana kumwacha adumu ni kukubali kuwa utawala wa shetani umeshinda.
Wa namna hiyo huwa hawadumu. Wanakuwepo kwa muda tu, kisha Mungu hukatisha utawala wao ili watu wake wasiendelee kuangamia. Ndivyo ilivyokuwa kwa Hitler, Mussolin, Stallin, Nguema.
Tunaweza kuwa na kasoro na mapungufu mengi lakini tusifikie kuua, kuwapoteza au kuwadhulumu wenzetu. Siku zote, kudhulumu uhai au mali za watu, huzaa laana kubwa. Hakuna zuri unaloweza kufanya likasafisha uovu wako wa kuua watu.