Panya Road wavamia Chamazi

Panya Road wavamia Chamazi

tpaul

Platinum Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
25,995
Reaction score
25,392
Kwa mujibu wa taarifa za kiintelijensia nilizopenyezewa na raia wema ni kwamba genge hatarishi la Panya Road limefanya uhalifu usiku huu katika maeneo ya Chamazi (Jimbo la Mbagala) na sasa wamekusanyika karibu na eneo la chuo cha afya cha Muhimbili lililopo Chamazi, wakilenga kuendelea na uhalifu wao kama kawaida. Hivi sasa wananchi wako roho juu wakihimizana kufunga milango ya nyumba zao na kuepuka kutoka nje ili kujilinda na uhalifu wa genge hili la kimafia linalozidi kutikisa jiji la Dar es Salaam siku hadi siku.

Nimeuweka uzi huu hapa kwa makusudi. Panya Road wametufikisha hapa baada ya kushindwa kudhibitiwa kikamilifu na vyombo vya ulinzi.

Tutapeana taarifa baadaye kadri ninavyozipata kutoka eneo la tukio. Wananchi wanaishi kwa hofu kubwa kufuatia kundi hili linalojibadilisha kila kukicha kutoka genge la wahalifu na kuwa kundi la kigaidi. Serikali inapaswa kuchukua hatua kuwalinda raia na mali zao na ikibidi wananchi wamilikishwe silaha nzito kwa ajili ya kujilinda wao wenyewe na mali zao. Kuna haja ya kuanzisha mafunzo ya lazima ya kijeshi kwa wananchi ili kuwajengea uwezo wa kujilinda.
majeruhi%20issa%20joseph.jpg
 
Mzunguko mdogo wa hela mitaani ni moja ya kichocheo cha matukio haya
Ni kweli. Hili kundi hata sijui limeibukaje wakati Dar ilikuwa imenza kuwa tulivu. Serikali inapaswa kuwapa wananchi mafunzo ya kijeshi na kuwamilikisha silaha kwa ajili ya kujilinda na makundi ya kipuuzi kama hili la Panya Road.
 
Wanavamia Mitaa ya walalahoi tu, waje huku Mitaa ya Miande waone cha moto
mkuu, lakini nadhani pia tangu polisi walipoacha kukaa vituoni usiku kundi hili limepata kasi ya kuendelea kuwatesa raia na kuwanyima raha kabisa. serikali inapaswa kufikiria upya uamuzi wake wa kufunga vituo ili polisi wachache waliopo washirikiane na wananchi kutokomeza kundi hili la kigaidi.
 
Nadhani pale Chamazi kuna kituo cha polisi. Vipi huna namba zao uwapigie wachukue hatua za haraka? Hilo eneo la Muhimbili hakika ni hatarishi sana. Lipo wazi kwa vile halijajengwa ijapokuwa limezungukwa na makazi ya watu. Nakumbuka pia jirani na hilo eneo kuna Bar nadhani inaitwa Last Card. Mliopo Chamazi mtanisahihisha
 
Chamazi kuna kituo cha polisi kidogo ambacho hufungwa nyakati za usiku na polisi kurejea majumbani mwao.
Hapana Mkuu. Kile kituo kipo wazi masaa 24. Jirani ya hicho kituo kuna Bar Maarufu inaitwa Chamazi Pub. Fanya hima kufikisha taarifa ili hao wahuni washughulikiwe
 
Mkuu kwann huku mbezi beach hawaji? Huku si ndio kwa matajiri? Waje hapa tangi bovu kwa chini..tena huku hamna ujirani kila mtu na geti lake? Wakija ni kukata na kuiba tu...kwann wanaiba uswahilini ..? Nawakaribisha mbezi beach....huku kuna wanaume wa dar tu lege lege na watoto wa mama! (Kama wa mkoani wanavyosema)

Glock 17
Berretta
Pump Action
.45 colt

And so forth..
Karibuni tunawasubiri.
 
Back
Top Bottom