Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 877
- 4,105
Huduma ya usafiri wa ndege kwenda Mwanza imeimarika sana. Ndege zipo nyingi na zinatoa huduma masaa ishirini na nne kwa kupishana anagani.
Wageni wengi wanaingia Mwanza sasa hivi, baadhi ya wasafiri kutoka nchi jirani wanapandia ndege Mwanza.
Kila ninapopita katika uwanja huu napatwa na msongo wa mawazo! Sijui ni nani alitoa vibali vya ujenzi mbele ya uwanja. Mbele ya uwanja kuna vibanda vya chakula, ofisi, vyoo nk ambavyo vimejengwa bila kuzingatia masharti ya ujenzi wala ubora.
Niombe mtu akipita uwanja wa Mwanza ahesabu makontena madogo madogo yaliyowekwa nje, ahesabu vibanda vidogovidogo vilivyo jengwa like kila ukitaka kujenga unapewa Sehemu yako.
Hali ya uchafu uwanjani inatia aibu na kutatiza juhudi za Mhe. Rais. Viongozi wa uwanja na jiji la Mwanza mnasubiri hadi Mhe Rais aje awaeleze chakufanya? Kwanini msibomoe hivi vibanda kama mnavyowabomolea machinga stendi na mjini?
Mhe. Makala tembelea uwanjani, may be unapita ukiwa ndani ya gari pamoja na viongozi wenzako. Nenda kesho kakague pale naamini utapavunja na kujenga au kubipanga vyema vibanda huku ukisimamia usafi.
Kumbuka hii hoja tuliwahi kuileta kwenu sisi watu wa sekta ya utalii mwaka juzi na mliweka ahadi yakupapanga upya ila bado kimya.
Wageni wengi wanaingia Mwanza sasa hivi, baadhi ya wasafiri kutoka nchi jirani wanapandia ndege Mwanza.
Kila ninapopita katika uwanja huu napatwa na msongo wa mawazo! Sijui ni nani alitoa vibali vya ujenzi mbele ya uwanja. Mbele ya uwanja kuna vibanda vya chakula, ofisi, vyoo nk ambavyo vimejengwa bila kuzingatia masharti ya ujenzi wala ubora.
Niombe mtu akipita uwanja wa Mwanza ahesabu makontena madogo madogo yaliyowekwa nje, ahesabu vibanda vidogovidogo vilivyo jengwa like kila ukitaka kujenga unapewa Sehemu yako.
Hali ya uchafu uwanjani inatia aibu na kutatiza juhudi za Mhe. Rais. Viongozi wa uwanja na jiji la Mwanza mnasubiri hadi Mhe Rais aje awaeleze chakufanya? Kwanini msibomoe hivi vibanda kama mnavyowabomolea machinga stendi na mjini?
Mhe. Makala tembelea uwanjani, may be unapita ukiwa ndani ya gari pamoja na viongozi wenzako. Nenda kesho kakague pale naamini utapavunja na kujenga au kubipanga vyema vibanda huku ukisimamia usafi.
Kumbuka hii hoja tuliwahi kuileta kwenu sisi watu wa sekta ya utalii mwaka juzi na mliweka ahadi yakupapanga upya ila bado kimya.