Pamoja na Bodi kumpendekeza, Dk Rashid aweka sharti la kurudi TANESCO!

Mag3

Platinum Member
May 31, 2008
13,064
22,757

Ni mara chache nakosa la kusema lakini leo hakika sina la kusema, niseme nini ? Ni mtu mmoja tu Tanzania anayeweza kuiendesha TANESCO hata kama mtu huyo kachafuka namna gani ! Jamani kuendesha nchi si mchezo, Mungu inusuru Tanzania !
 
Hii nchi inasikitisha sana.Ngoja wamrudishe akaikamilishe 'kazi' aliyoianza...Sasa sijui ilikuwa na maana gani kutangaza nafasi hiyo na watu wakaaply.Au sheria zao za mapendekezo zinaruhusu kumpendekeza hata asiyeshiriki kwenye mchakato?
 
Dont tell me hatuna watu wa kuongoza Tanesco isipokuwa Dr Rashid tu!
 
Kama ni body iliyo jaa vilafi wale wale kweli tunategemea watampendekeza mtu atakae watolea mlo wao. Tazama alafu pendekezo lake asiingilwe kwenye kuwapatia mlo body members, chanzo hicho hicho kilicho watoa imani nae hata hao wazembe huko bungeni. I mean kwenye mchi ambayo utapeli unatendeka kila kukicha hadi wabunge waseme ujue jamaa alizidi. Aendelee tu kula pension labda wa change na body yenyewe yote guarantee tutapata kiongozi mpya.
 
he is the best in pool :gossip:

Hata mimi labda ningesema hivyo. Wakati wa kuchagua kuna vitu vingi vinaangaliwa na mojawapo ni maslahi ya mwenye kuchagua. Kama ndiye pekee anaweza kulinda maslahi yangu then he is the best.

... Kwani tumesahau kuwa katika TZ hakuna tena kitu kinaitwa maslahi ya umma?
 
Haya mambo yameanza
Kuna ile miradi mikubwa ya umeme ya mabilioni iliyotangazwa na serikali hivi karibuni, yaonekana hakuna mwingine bali Dr. Idris Rashidi kuisimamia. Sababu ziko nyingi lakini kubwa ni ile ya historia kujirudia. Kwanza huu ni mwaka wa uchaguzi na pili kuna chama kinatafuta na kimepanga kutumia bilioni 50 katika kampeni zake.

Hosea yuko pale pale, Ndullu kishawekwa mfukoni, Dr. Dau azidi kumwagiwa sifa na timu inamkosa tu mtu moja, Dr. Idris. Shemeji zao EPA na Richmond nao wamekaa mkao wa kula - kweli mwaka wa uchaguzi una mambo !
 
Haya ni matusi makubwa sana kwa wasomi wengine wa kitanzania. Hivi kweli bila Idris Rashid kuwepo Tanesco hilo shirika litakufa??!! Jamani wakati mwingine wawe wanajua kuchagua aina ya matusi, haya si mazuri kabisa. Tuna vichwa kibao vya kuweza kuendesha hata nchi ije kuwa Tanesco.
 
Mbali ya Peter Ngumbulu hivi hii bodi ya Tanesco wajumbe wengine ni akina nani?............mwenye kujua please anisaidie kunipa majina yao hapa bodini JF
 
Haya ni matusi makubwa sana kwa wasomi wengine wa kitanzania. Hivi kweli bila Idris Rashid kuwepo Tanesco hilo shirika litakufa??!!
Ni yeye tu anayeweza kulinda maslahi yao kwa ufanisi wa hali ya juu potelea mbali hata nchi ikiingia gizani. Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC), Mh. Zitto Kabwe, mbunge wa Kigoma, yasemekana anakubaliana nao kwamba Dr. Rashidi is the Best CEO ever - hakuna kama yeye nchini.

Jamani wakati mwingine wawe wanajua kuchagua aina ya matusi, haya si mazuri kabisa. Tuna vichwa kibao vya kuweza kuendesha hata nchi ije kuwa Tanesco.
Hivyo vichwa vingine yasemekana havina nguvu na jeuri ya Dr. Rashidi aliyetaka kulazimisha ununuzi wa mitambo ya Dowans la sivyo nchi ikumbwe na giza totoro. Yasemekana kwa hili nalo aliungwa mkono na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) na sasa katoa sharti lingine la kutoingiliwa katika utendaji wake - mmh, kazi kweli kweli.
 
Tangu wakati ule alipolazimisha zinunuliwe la sivyo tungeingia katika giza, mbona hazijanunuliwa na hatupo kwenye giza? na akirudi zisiponunuliwa tutaingia kwenye giza kweli.
 
natafuta jeshi la uasi la Tanzania nijiunge nalo maana hivi nilivyo CCM wananiua na uchaguzi ni wizi mtupu si bora nijaribu kuwatoa huenda nikafanikiwa
 
Hata kwa kutumia ufahamu wangu mdogo wa taaluma ya nishati, nafikiri TANESCO ni moja ya mashirika magumu sana kuyaendesha Tanzania. sio kwamba kwa sababu ni kubwa, lakini kutokana na kuingiliwa sana na wanasiasa wakiwa na agenda zao za siri. Hakuna ubishi kuwa ni shirika kubwa ambalo kiutendaji linafaa kuvunjwa na kuwa kampuni tatu, uzalishaji, usafirishaji na ugawaji, na mwisho ufungaji kwa wateja. I hope haya ndio mapendekezo yaliyokuwa yamewasilishwa na Net Group.
 
Watu zaidi ya 50 wajitokeza kuwania ukurugenzi Tanesco
WATU zaidi ya 50 wamejitokeza kuomba nafasi ya Mkurugenzi Mkuu Tanesco iliyotangazwa Septemba 18, mwaka huu na Bodi ya Wakurugenzi wa shirika hilo.


Source Mwananchi 16th October 2009
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…