Ngalikivembu
JF-Expert Member
- Oct 6, 2010
- 1,959
- 872
Kwa wana jf wote jina la Padre Baptist Mapunda si geni. Leo alikuwa anahubiri hapa kanisa la Mjimwema Songea mjini. Bahati nzuri leo hii ni sherehe za CCM kutimiza miaka 38.
Alisema leo wana sherehekea miaka ya 38 ya kuwatesa na kuwanyanyasa nyie wananchi. Hawa ni wauaji na nyie mnawa shangilia. Kuendelea kuichagua ni kujichoma sindano ya sumu. Unakufa taratibu. Anasema najua mpo wana CCM hapa nendeni mkamwambie Kikwete nipo hapa leo.
Katiba inayopendekezwa. Akauliza mnataka kuipigia kura ya ndiyo mmeisoma? Anauliza wangapi wanayo? Akanyosha mtu mmoja tu kanisa nzima. Mnaona umati wote huu anayo mmoja tu? Halafu unashabikia CCM. Kwanini hawasambazi mkaipata? Kimya kanisa lote.
Escrow na Askofu. Alimponda askofu aliyechukua milioni 80. Anasema yule askofu hana maadili. Unachukuaje hela usiyoijua wala usiyofanyia kazi,?
Hitimisho; CCM kuendelea kuiweka madarakani ni kujilisha sumu mwilini mwisho itakuua mwenyewe.
Hakika Padre huyu mahubiri yake unaweza kuyaogopa kama una moyo mwepesi
Alisema leo wana sherehekea miaka ya 38 ya kuwatesa na kuwanyanyasa nyie wananchi. Hawa ni wauaji na nyie mnawa shangilia. Kuendelea kuichagua ni kujichoma sindano ya sumu. Unakufa taratibu. Anasema najua mpo wana CCM hapa nendeni mkamwambie Kikwete nipo hapa leo.
Katiba inayopendekezwa. Akauliza mnataka kuipigia kura ya ndiyo mmeisoma? Anauliza wangapi wanayo? Akanyosha mtu mmoja tu kanisa nzima. Mnaona umati wote huu anayo mmoja tu? Halafu unashabikia CCM. Kwanini hawasambazi mkaipata? Kimya kanisa lote.
Escrow na Askofu. Alimponda askofu aliyechukua milioni 80. Anasema yule askofu hana maadili. Unachukuaje hela usiyoijua wala usiyofanyia kazi,?
Hitimisho; CCM kuendelea kuiweka madarakani ni kujilisha sumu mwilini mwisho itakuua mwenyewe.
Hakika Padre huyu mahubiri yake unaweza kuyaogopa kama una moyo mwepesi