Padre amwagiwa Tindikali huko Zanzibar

Padre amwagiwa Tindikali huko Zanzibar

Status
Not open for further replies.
Haya yanatokea katikati ya mhemko wa Katiba mpya ya Muungano na Muundo wa Muungano huo,

Zingatieni matukio ya nyuma kisha ulizeni serikali ya Zanzibar na ya Jamhuri zimefikia wapi katika kuchukua hatua?

Mkikosa jibu rudini chini kwa tafakuri pembuzi, kisha ulizeni nani yupo juu ya serikali mpaka akatamalaki katika uga huo?

Mkimaliza yote utulieni na serikali, muiulize lengo lake litatimia kama jamii fulani imekataa ukandamizwaji?

Inauma sana, inauma sana,

Inauma hasa unapomuina muuaji akikufumba macho kwa bakuli la tume,

Kama Mungu ulivyo wa haki, na iwe vile upendavyo katika ardhi ya Zanzibar na katika Ardhi ya Tanganyika,

Watawala wakaidi na useme nao kwakufungua fikra za watu wako na wawe huru chini ya uvuli huu wa mauti!

Zanzibar ikiwa huru hakuna shehe wala kasisi atakaejeruhiwa ama kumwagwa damu,

Uhuru wa Zanzibar upo chini ya Serikali TATA chini ya Shirikisho la Jamhuri ya Watu wa Tanzania

Tanganyika huru inaewezekana na Zanzibar huru inawezekana, Tanzania itasimama imara kutokana na nchi hizo mbili kuwa huru!
 
lakini jamani itumike busara kwa matokeo yanayoendelea tanzania, kuuwawa kwa padri, bomu arusha na mauaji arusha, kumwagiwa tindikali wazungu, nina wasiwasi sana kuna mkono wa mtu, nikiwa na maana kuwa kwa hali ya siasa inavyoendelea lazima yatokee haya. Kwa sababu Itafanywa lolote lile ili cuf, chadema wasiungane. Hivi ni vitu vimepangwa kimkakati nadhani.hebu tujiulize kwanini hawa wahalifu hawakamatwi?
 
Tunalea ujinga na Kanisa linaendelea kuomba serikali dhaifu kuchukua hatua!! Kanisa lichukue hatua ngumu kidogo kukomesha hili! Nikisema hatua ngumu kidogo najua jinsi Kanisa linachoweza kufanya ktk mazingira hatarishi kuinjilisha au hata imani za waamini kuwa mashakani na hofu kuu.

Mlinzi wetu ni mlokole,akimuona mwizi anaingia kuiba anamwambia"wee iba tu,Mungu anakuona" ndiyo maana Dr slaa alisema wazi,kumuacha mhalifu akiendelea na uhalifu kisha sisi walinzi tunaitana pembeni eti kumuomba mungu aepushe uhalifu ni UJINGA.
 
Nina mashaka na Mungu anayeabudiwa na Waislamu. Sithani kama ni Mungu yule tuaminiye ndo Muumba Mbingu na Dunia. Nadhani hawa jamaa wana Mungu wao


Acha hizo mambo wewe,
why are you so judgmental?
Umeambiwa waliofanya ivo ni waislam?
Huku bara hakuna waislam na uislam?mbona hayo matukio hatuyaskii?
Watu kama wana ajenda zao,wahukumiwe kwa hizo ajenda zao,usije toa maoni kwa kuwa umeona population kubwa ya huko ni muslims,acha kabis mawazo ya kunyoosheana vidole,tuheshimiane,tuchunge mihemko ya iman zetu
 
Ni muda mwafaka Polisi kubadilika. Matukio haya yanaendelea kutokea kwa sababu hawakamatwi na kuchukuliwa hatua mwafaka za kisheria. Ninashangaa uongozi wa Polisi Zanzibar hauwajibishwi. Watu tunaanza kufikiria wanayafumbia macho matukio haya au wanahusika nayo!
 
Wazanzibar ni watu wa amani sana na huu utakuwa ni mchezo wa wale wanaogogopa kuiona ZNZ ikiwa huru. Hatuwezi kumeza propaganda za kijinga kama hizi, haingii akilini mtu mwenye akili timamu akammwagia tindikali au kufanya jaribio lolote la kutaka kumdhuru kiongozi wa kidini au yeyote yule.

Nadhani ni muda muafaka kwa wananchi kuilazimisha serikali kuweka wazi uchunguzi na uwajibishaji wa wanaofanya hivi vitendo kama kweli haya yanafanywa na wananchi wa kawaida!

vipofu mabubu viziwi ndio wanaweza kudanganyika na expenderble way of tactics.
1.si muda mrefu tangia freeman mbowe kutolewa nje bungeni.ambapo ilipekea wabunge wa cuf na nccr kutoka nje kwa vurugu.
2.the main issue ilikuwa zanzibar kutoshirikishwa katika mabadiliko ya rasimu
3.huu uwasi wa uamsho hauendani na recent event yoyote ya hivi karibuni.
namalizia kwa kusema msidandie treni kwa mbele kwa lile msilo lijuwa.
 
attachment.php
 
Mungiki walikuwa wengi sana lakini Kibaki alipoanza kuwachapa risasi bila mjadala, haikupita mda wakapoa kama makondoo... Nadhan Shein anawalea UAMSHO...
 
>Mkristo kamwe hawezi kupata haki zanzibar...!Wazanzibar ni watu waajabu wasio na upendo.. Mungu wao hana upendo kwa wanadamu wenzao.. Mungu wao anawataka kuwauwa wasiofungamana nao! NADHANI HIZI NI DINI ZA IBILISI...
 
zanzibar hawautaki ukafiri
Niliwahi kusikia kipindi kimoja kwenye runinga kuhusu historia ya mtume muhamad ya kuwa kipindi chake cha kueneza dini alitafutwa na maadui zake ili auwawe kwa kujiepusha alikimbilia ethiopia wakati huo na ilikuwa nchi inayoongozwa na wakristo,je kama wakristo ni makafiri,mtume alifata nini ethiopia,sidhani kama haya ni maagizo ya mtume bali haya sio maagizo ya mtume bali wanachokifanya sasa ni tofauti na kile alichoagiza mtume,kwa sasa hadi watoto tunawafundisha kuwa wakristo ni makafiri,je tunawalea katika misingi ipi watoto wetu kama sio ya chuki na uuaji.
 
Ni muda muafaka wafanyakazi waliopo zanzibarkutokea bara kulipwa posho ya kufanya kazi mazingira hatarishi “risk allowance”
 
Padri wa kanisa katoliki Parokia ya Cheju wilaya ya kati mjini Zanzibar Joseph Onesmo Mwangamba, amejeruhiwa usoni na kifuani baada ya kumwagiwa tindikali. Wahusika wamekimbia baada ya tukio hilo Source: RADIO 1 STEREO
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom